-
Waroma Wapata Habari Bora KabisaMnara wa Mlinzi—1990 | Agosti 1
-
-
Kichwa kilichozungumzwa katika Waroma kilikuwa cha maana katika karne ya kwanza na kingali chapasa kupewa umuhimu leo. Uadilifu na uhai wa milele ni lazima vipendeze watumishi wote wa Yehova. Ni kweli kwamba Waroma kiliandikwa kwa kundi la Wakristo wapakwa-mafuta, hali leo walio wengi sana wa Mashahidi wa Yehova ni wa “umati mkubwa” na wana tumaini la kidunia. (Ufunuo 7:9, NW) Hata hivyo, barua hii ina ujumbe muhimu kwa hao pia. Ujumbe gani?
Kitabu cha Waroma huthibitisha kwamba Wakristo hujulishwa rasmi kuwa waadilifu kwa njia ya imani. Kwa wapakwa-mafuta, hiyo ni kwa tazamio la kuwa watawala-wenzi pamoja na Yesu katika Ufalme wa kimbingu. Hata hivyo, washiriki wa umati mkubwa hujulishwa rasmi pia kuwa waadilifu, lakini wakiwa ‘rafiki za Mungu,’ kama alivyokuwa Abrahamu mzee wa ukoo. (Yakobo 2:21-23) Uadilifu wao ni kwa tazamio la kuokoka dhiki kubwa, na msingi wao ni damu ya Yesu, kama vile ilivyo kwa habari ya wapakwa-mafuta. (Zaburi 37:11; Yohana 10:16; Ufunuo 7:9, 14) Hivyo, njia ya Paulo ya kusababu mambo katika Waroma ni ya kuhangaikiwa sana na kondoo wengine na pia wapakwa-mafuta. Na shauri zuri la kitabu hicho la kuishi kupatana na kujulishwa kwetu rasmi kwamba sisi ni waadilifu ni muhimu kwa Wakristo wote.
The Book of Life, kilichohaririwa na Madaktari Newton Marshall Hall na Irving Francis Wood, chataarifu hivi: “Kwa kuzungumzia juu ya upande ule wenye kubishaniwa na wa kimafundisho, [Waroma] chafikia kilele cha fundisho la Paulo lililovuviwa. Ni chenye hisani, busara, hata hivyo chenye mamlaka. . . . Kujifunza waraka huu kuna thawabu zao zilizo nyingi na tele.” Kwa nini usijisomee mwenyewe kitabu hicho na ushangilie katika “habari njema” zilizomo, ambazo ni “nguvu ya Mungu kwa ajili ya wokovu.”—Waroma 1:16, NW.
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 24]
-