-
Kushiriki Faraja Ambayo Yehova HuandaaMnara wa Mlinzi—1996 | Novemba 1
-
-
“Mungu wa Faraja Yote”
5. Pamoja na majaribu mengi ambayo Paulo alipatwa nayo, yeye alijionea nini pia?
5 Mmoja ambaye alithamini sana faraja ambayo Mungu hupa alikuwa mtume Paulo. Baada ya wakati wenye kujaribu hasa katika Asia na Makedonia, alipata kitulizo kikubwa aliposikia kwamba kutaniko la Korintho lilikuwa limeitikia vema barua yake ya karipio. Hilo lilimsukuma awaandikie barua ya pili, ambayo ina maneno yafuatayo ya sifa: “Na ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa rehema [“nyororo,” NW], Mungu wa faraja yote; atufarijiye katika dhiki zetu zote.”—2 Wakorintho 1:3, 4.
6. Twajifunza nini kutokana na maneno ya Paulo yapatikanayo kwenye 2 Wakorintho 1:3, 4?
6 Maneno hayo yaliyopuliziwa hutuandalia habari nyingi. Acheni tuyachunguze. Paulo atoapo sifa au shukrani kwa Mungu au kumwomba jambo fulani katika barua zake, kwa kawaida twapata kwamba yeye hutia ndani pia uthamini wenye kina kwa ajili ya Yesu, aliye Kichwa cha kutaniko la Kikristo. (Warumi 1:8; 7:25; Waefeso 1:3; Waebrania 13:20, 21) Kwa sababu hiyo, Paulo anamsifu “Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo.” (Italiki ni zetu.) Kisha, kwa mara ya kwanza katika uandikaji wake mbalimbali, anatumia nomino ya Kigiriki itafsiriwayo “rehema nyororo.” Nomino hiyo yatokana na neno litumiwalo ili kuonyesha huzuni kuelekea kuteseka kwa mwingine. Hivyo Paulo anafafanua hisia nyororo za Mungu kwa wowote wa watumishi Wake waaminifu wanaopatwa na dhiki—hisia nyororo ambazo humsukuma Mungu atende kwa rehema kwa niaba yao. Mwishowe, Paulo alimtegemea Yehova kuwa chanzo cha sifa hiyo yenye kutamanika kwa kumwita “Baba wa rehema [“nyororo,” NW].”—Italiki ni zetu.
7. Kwa nini yaweza kusemwa kwamba Yehova ndiye “Mungu wa faraja yote”?—Italiki ni zetu.
7 “Rehema nyororo” za Mungu hutokeza kitulizo kwa yule apatwaye na dhiki. Kwa hiyo, Paulo aendelea kumfafanua Yehova kuwa “Mungu wa faraja yote.” Hivyo, faraja yoyote tuwezayo kupata kutoka kwa fadhili ya waamini wenzetu, twaweza kumwona Yehova kuwa ndiye chanzo chayo. Hakuna faraja halisi, yenye kudumu ambayo haitokani na Mungu. Zaidi, yeye ndiye aliyemuumba mwanadamu katika mfano wake, hivyo akituwezesha kuwa wafariji. Na roho takatifu ya Mungu ndiyo huwahamasisha watumishi wake waonyeshe rehema nyororo kuelekea wale wanaohitaji kupata faraja.
-
-
Kushiriki Faraja Ambayo Yehova HuandaaMnara wa Mlinzi—1996 | Novemba 1
-
-
8. Ingawa Mungu siye chanzo cha majaribu yetu, kuvumilia kwetu dhiki kwaweza kuwa na tokeo jipi lenye manufaa juu yetu?
8 Ingawa Yehova Mungu huruhusu majaribu mbalimbali yawajiayo watumishi wake waaminifu, yeye hawi kamwe chanzo cha majaribu hayo. (Yakobo 1:13) Hata hivyo, faraja anayoandaa tuvumiliapo dhiki yaweza kutuzoeza kutambua upesi zaidi mahitaji ya wengine. Kukiwa na tokeo jipi? “Tupate kuwafariji wale walio katika dhiki za namna zote, kwa faraja hizo tunazofarijiwa na Mungu.” (2 Wakorintho 1:4) Hivyo Yehova hutuzoeza tuwe washiriki wenye matokeo wa faraja yake pamoja na waamini wenzetu na pamoja na wale tunaokutana nao katika huduma yetu tumwigapo Kristo na “kuwafariji wote waliao.”—Isaya 61:2; Mathayo 5:4.
-