-
Tatizo la KitheolojiaMnara wa Mlinzi—1995 | Machi 1
-
-
Catechism of the Catholic Church chasema hivi: “Ili tuinuke na Kristo, ni lazima tufe na Kristo: ni lazima ‘tusiwe katika mwili na kukaa pamoja na Bwana’. [2 Wakorintho 5:8] Katika ‘kuondoka’ huko ambako ni kifo, nafsi hutenganishwa na mwili. [Wafilipi 1:23] Itaunganishwa na mwili katika siku ya ufufuo wa wafu.” Lakini katika maandiko yaliyonukuliwa hapa, je, mtume Paulo asema kwamba nafsi huokoka kifo cha mwili na kisha kungojea “Hukumu ya Mwisho” ili iunganishwe tena na mwili?
-
-
Tatizo la KitheolojiaMnara wa Mlinzi—1995 | Machi 1
-
-
Katika Wafilipi 1:21, 23, Paulo asema hivi: “Kwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faida. Ninasongwa katikati ya mambo mawili; ninatamani kwenda zangu nikae na Kristo; maana ni vizuri zaidi sana.” Je, hapo Paulo arejezea ile “hali ya katikati”? Wengine hufikiri hivyo. Hata hivyo, Paulo asema kwamba alikuwa amesongwa na mawezekano mawili—uhai au kifo. Lakini “ninatamani,” yeye akaongezea, akitaja uwezekano wa tatu, “kwenda zangu nikae na Kristo.” Je, ni “kwenda” kuwa na Kristo mara tu baada ya kifo? Kama tulivyoona tayari, Paulo aliamini kwamba Wakristo watiwa-mafuta walio waaminifu wangefufuliwa wakati wa kuwapo kwa Kristo. Kwa hiyo, ni lazima alikuwa akisema juu ya matukio ya wakati huo.
Hilo laweza kuonekana kwa maneno yake katika Wafilipi 3:20, 21 na 1 Wathesalonike 4:16. “Kwenda” huko wakati wa kuwapo kwa Kristo Yesu kungewezesha Paulo kupokea thawabu ambayo Mungu alikuwa amemwekea. Uhakika wa kwamba hili lilikuwa tumaini lake laonekana katika maneno yake kwa kijana Timotheo: “Baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.”—2 Timotheo 4:8.
-