Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Iga Imani ya Musa
    Mnara wa Mlinzi—2014 | Aprili 15
    • 1, 2. (a) Musa alifanya uamuzi gani alipokuwa na umri wa miaka 40? (Tazama picha kwenye ukurasa huu.) (b) Kwa nini Musa alichagua kutendewa vibaya pamoja na watu wa Mungu?

      MUSA alijua ufanisi ambao angepata nchini Misri. Aliona nyumba za kifahari za matajiri. Aliishi na familia ya kifalme. ‘Alifundishwa hekima yote ya Wamisri,’ ambayo huenda ilitia ndani sanaa, elimu ya nyota, hesabu, na mambo mengine ya kisayansi. (Mdo. 7:22) Angepata mali, mamlaka, na pendeleo ambalo Mmisri wa kawaida hangeweza kupata.

      2 Hata hivyo, Musa alipokuwa na umri wa miaka 40 alifanya uamuzi ambao bila shaka ulimshangaza Farao na familia ya kifalme iliyomlea. Hakuchagua tu maisha ya Wamisri wa kawaida, badala yake alichagua kuishi na watumwa. Kwa nini? Musa alikuwa na imani. (Soma Waebrania 11:24-26.) Kwa imani, Musa hakuona tu ufanisi ambao angepata ulimwenguni. Kwa kuwa Musa alithamini mambo ya kiroho, alikuwa na imani katika Yehova, ‘Yule asiyeonekana,’ na katika utimizo wa ahadi Zake.​—Ebr. 11:27.

  • Iga Imani ya Musa
    Mnara wa Mlinzi—2014 | Aprili 15
    • 4. Musa alitambua nini kuhusu “kufurahia dhambi”?

      4 Musa aliona kwa macho ya imani kwamba “kufurahia dhambi” ni jambo la muda mfupi tu. Huenda wengine wangesema kwamba Misri ilikuwa serikali kuu ya ulimwengu licha ya kwamba ibada ya sanamu na uchawi ulikuwa umeenea sana nchini humo na wakati huo watu wa Yehova walikuwa watumwa. Hata hivyo, Musa alijua kwamba Mungu angeweza kubadili mambo. Ingawa waovu walionekana wanafanikiwa, Musa alikuwa na imani kwamba wangeangamia. Kwa hiyo, hakushawishika “kufurahia dhambi kwa muda.”

      5. Ni nini kitakachotusaidia kukataa “kufurahia dhambi kwa muda”?

      5 Unawezaje kupinga kishawishi cha “kufurahia dhambi kwa muda”? Usisahau kamwe kwamba mtu hawezi kufurahia dhambi kwa muda mrefu. Kwa macho ya imani, ona kwamba “ulimwengu unapitilia mbali na pia tamaa yake.” (1 Yoh. 2:15-17) Tafakari kuhusu wakati ujao wa watenda-dhambi wasiotubu. Wako ‘kwenye udongo unaoteleza, watamalizwa kwa matisho!’ (Zab. 73:18, 19) Unaposhawishiwa kutenda dhambi, jiulize hivi: ‘Jambo hili litaathirije wakati wangu ujao?’

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki