-
Je, Unamwona ‘Yule Asiyeonekana’?Mnara wa Mlinzi—2014 | Aprili 15
-
-
10. (a) Yehova aliwapa Waisraeli maagizo gani katika mwezi wa Nisani, mwaka wa 1513 K.W.K.? (b) Kwa nini Musa alitii maagizo ya Mungu?
10 Katika mwezi wa Nisani, mwaka wa 1513 K.W.K., Yehova aliwaambia Musa na Haruni wawape Waisraeli maagizo haya yasiyo ya kawaida: Chagueni kondoo dume au mbuzi mwenye afya nzuri, mumchinje, na kuipaka damu yake juu ya milango yenu. (Kut. 12:3-7) Musa alitendaje? Baadaye mtume Paulo aliandika hivi kumhusu: “Kwa imani alifanya sherehe ya pasaka na upakaji wa damu, ili mwangamizaji asiwaguse wazaliwa wao wa kwanza.” (Ebr. 11:28) Musa alijua kwamba Yehova anategemeka, na hivyo alionyesha imani katika ahadi ya Yehova ya kuwaangamiza wana wazaliwa wa kwanza wa Wamisri.
11. Kwa nini Musa aliwaonya wengine?
11 Wana wa Musa walikuwa Midiani, mbali na “mwangamizaji.”a (Kut. 18:1-6) Hata hivyo, alitii na kuwapa maagizo hayo Waisraeli wengine ambao wana wao wazaliwa wa kwanza walikuwa hatarini. Uhai wao ulikuwa hatarini, na Musa aliwapenda wanadamu wenzake. Biblia inasema hivi: “Papo hapo Musa akawaita wanaume wote wazee wa Israeli na kuwaambia: ‘Mchinjeni mnyama wa pasaka.’”—Kut. 12:21.
12. Yehova ametuagiza tutangaze ujumbe gani muhimu?
12 Watu wa Yehova wanatangaza ujumbe huu muhimu wakiongozwa na malaika: “Mwogopeni Mungu na kumpa utukufu, kwa sababu saa ya hukumu yake imefika, na kwa hiyo mwabuduni Yeye aliyezifanya mbingu na dunia na bahari na chemchemi za maji.” (Ufu. 14:7) Huu ndio wakati wa kutangaza ujumbe huo. Ni lazima tuwaonye jirani zetu watoke katika Babiloni Mkubwa ili ‘wasipokee sehemu ya mapigo yake.’ (Ufu. 18:4) “Kondoo wengine” wanawasaidia Wakristo watiwa-mafuta kuwaomba wale waliotengwa mbali na Mungu ‘wapatanishwe’ naye.—Yoh. 10:16; 2 Kor. 5:20.
Imani katika ahadi za Yehova itakuchochea kuwa na hamu zaidi ya kuhubiri habari njema (Tazama fungu la 13)
13. Ni nini kitakachotuchochea kuwa na hamu zaidi ya kuhubiri habari njema?
13 Tunasadiki kwamba kwa kweli “saa ya hukumu yake imefika.” Pia, tuna imani kwamba Yehova hasemi uwongo kuhusu uharaka wa kazi yetu ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. Mtume Yohana aliona katika maono “malaika wanne wamesimama juu ya pembe nne za dunia, wakizishika sana zile pepo nne za dunia.” (Ufu. 7:1) Je, unawaona kwa imani malaika hao wakiwa tayari kuachilia pepo za uharibifu za dhiki kuu juu ya ulimwengu huu? Ukiona malaika hao kwa macho ya imani, utaweza kuhubiri habari njema ukiwa na uhakika.
-
-
Je, Unamwona ‘Yule Asiyeonekana’?Mnara wa Mlinzi—2014 | Aprili 15
-
-
a Hapana shaka kwamba Yehova aliwatuma malaika kutekeleza hukumu yake juu ya Wamisri.—Zab. 78:49-51.
-