Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jihadhari na Ukosefu wa Imani
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Julai 15
    • Mtu Mkuu Kuliko Musa

      8. Kwa kusema maneno yaliyorekodiwa kwenye Waebrania 3:1, Paulo alikuwa akiwahimiza Wakristo wenzake wafanye nini?

      8 Akitaja hoja muhimu, Paulo aliandika hivi: “Mfikirieni mtume na kuhani wa cheo cha juu ambaye twaungama—Yesu.” (Waebrania 3:1) ‘Kufikiria’ humaanisha “kutambua waziwazi . . . , kuelewa kikamili, kufikiri kwa makini.” (Kichapo Vine’s Expository Dictionary of Old and New Testament Words) Kwa hiyo, Paulo alikuwa akiwahimiza waamini wenzake wajitahidi sana kuthamini kikweli fungu la Yesu katika imani na wokovu wao. Kufanya hivyo kungetia nguvu azimio lao la kusimama imara katika imani. Basi, Yesu alikuwa na fungu gani, na kwa nini twapaswa ‘kumfikiria’?

      9. Kwa nini Paulo alimrejezea Yesu kuwa “mtume” na “kuhani wa cheo cha juu”?

      9 Paulo alimrejezea Yesu kwa kutumia maneno “mtume” na “kuhani wa cheo cha juu.” “Mtume” ni mtu atumwaye na hapa neno hilo larejezea njia ya Mungu ya kuwasiliana na wanadamu. “Kuhani wa cheo cha juu” ni mtu ambaye kupitia kwake wanadamu waweza kumfikia Mungu. Maandalizi hayo mawili ni ya muhimu kwa ibada ya kweli, na Yesu huchukua mafungu yote mawili. Yeye ndiye aliyetumwa kutoka mbinguni ili kuwafundisha wanadamu kweli juu ya Mungu. (Yohana 1:18; 3:16; 14:6) Pia Yesu ndiye aliyewekwa kuwa Kuhani wa Cheo cha Juu aliyefananishwa katika mpango wa hekalu la kiroho la Yehova kwa ajili ya msamaha wa dhambi. (Waebrania 4:14, 15; 1 Yohana 2:1, 2) Ikiwa kwa kweli twathamini baraka ambazo twaweza kupata kupitia Yesu, tutakuwa na moyo mkuu na tutaazimia kuendelea kuwa imara katika imani.

  • Jihadhari na Ukosefu wa Imani
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Julai 15
    • 11, 12. Paulo aliwahimiza Wakristo Waebrania washikilie nini “imara hadi mwisho,” nasi twaweza kutumiaje shauri lake?

      11 Kwa kweli, Wakristo Waebrania walikuwa na wadhifa uliopendelewa sana. Paulo aliwakumbusha kwamba walikuwa “washiriki wa mwito wa kimbingu,” pendeleo lililopasa kuthaminiwa sana kuliko kitu chochote ambacho mfumo wa Kiyahudi ungetoa. (Waebrania 3:1) Lazima maneno ya Paulo yawe yaliwafanya Wakristo hao watiwa-mafuta wawe na shukrani kwa sababu walitarajia kupokea urithi mpya badala ya kuhisi vibaya kwamba walikuwa wameacha vitu vilivyohusiana na utamaduni wa Kiyahudi. (Wafilipi 3:8) Akiwahimiza washikilie pendeleo lao na kutolipuuza, Paulo alisema hivi: “Kristo alikuwa mwaminifu akiwa Mwana juu ya nyumba ya [Mungu]. Sisi ndio nyumba ya Huyo, ikiwa twashikilia kwa imara hadi mwisho.”—Waebrania 3:6.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki