Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Wakumbukeni Wale Wanaoongoza Kati Yenu”
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • KWA NINI TUWAKUMBUKE “WALE WANAOONGOZA”?

      9 Tuna sababu nyingi za kuwakumbuka “wale wanaoongoza” na kuonyesha kwamba tunawatumaini. Tunafaidikaje kwa kufanya hivyo? Mtume Paulo alisema: “Wanaendelea kuwalinda ninyi kama wale watakaotoa hesabu, ili wafanye hivyo kwa shangwe na si kwa huzuni, kwa maana kufanya hivyo kungewadhuru ninyi.” (Ebr. 13:17) Ni muhimu sana tutii na kufuata maagizo ya wale wanaoongoza kwa sababu wanaendelea kutulinda ili tusipatwe na madhara ya kiroho.

      10 Katika andiko la 1 Wakorintho 16:14, Paulo alisema: “Mambo yote mnayofanya yafanyeni kwa upendo.” Maamuzi yanayofanywa kwa niaba ya watu wa Mungu hutegemea sifa hii bora ya upendo. Kuhusiana na upendo, andiko la 1 Wakorintho 13:4-8 linasema: “Upendo ni wenye subira na fadhili. Upendo hauna wivu, haujigambi, haujivuni, haujiendeshi bila adabu, hautafuti faida zake wenyewe, hauchokozeki. Hauweki hesabu ya ubaya. Haushangilii ukosefu wa uadilifu, bali hushangilia pamoja na kweli. Huhimili mambo yote, huamini mambo yote, hutumaini mambo yote, huvumilia mambo yote. Upendo haushindwi kamwe.” Kwa kuwa upendo ndio msingi wa maamuzi yote yanayofanywa ili kuwanufaisha watumishi wa Yehova, tuna hakika kwamba tutalindwa ikiwa tutatii mwongozo huo. Isitoshe, mwongozo huo ni uthibitisho wa upendo wa Yehova.

      11 Kama ilivyokuwa katika karne ya kwanza, Yehova anatumia wanaume wasio wakamilifu kuwaongoza watu wake. Hata zamani Yehova alitumia wanadamu wasio wakamilifu kutimiza mapenzi yake. Noa alijenga safina na kuhubiri kuhusu uharibifu uliokuwa ukikaribia siku hizo. (Mwa. 6:13, 14, 22; 2 Pet. 2:5) Musa aliteuliwa kuwaongoza watu wa Mungu kutoka Misri. (Kut. 3:10) Wanaume wasio wakamilifu waliongozwa na roho takatifu kuandika Biblia. (2 Tim. 3:16; 2 Pet. 1:21) Leo, ingawa Yehova anatumia wanaume wasio wakamilifu kuongoza kazi ya kuhubiri na kufundisha, hilo halifanyi tusilitumaini tengenezo la Mungu. Badala yake, tunaimarishwa kwa sababu tunajua kwamba bila msaada wa Yehova, tengenezo halingeweza kufanya mambo linayotimiza. Kupitia hali nyingi ngumu na mambo ambayo amejionea, mtumwa mwaminifu amedhihirisha kwamba roho ya Mungu inaongoza mambo. Sehemu inayoonekana ya tengenezo la Yehova imepata baraka nyingi. Kwa hiyo, tunaiunga mkono kikamili na kuitumaini kabisa.

  • “Wakumbukeni Wale Wanaoongoza Kati Yenu”
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • 14 Njia nyingine ambayo tunaonyesha kwamba tunaunga mkono tengenezo ni kwa kukubali maamuzi yanayofanywa. Hilo linatia ndani kufuata kwa unyenyekevu mwongozo wa ndugu waliowekwa rasmi, kama vile waangalizi wa mzunguko na wazee wa makutaniko. Ndugu hao ni miongoni mwa “wale wanaoongoza” ambao tunapaswa kuwatii na kuwanyenyekea. (Ebr. 13:7, 17) Ingawa huenda tusielewe kikamili sababu ya maamuzi fulani, tunajua kwamba tukiyaunga mkono, tutapata faida za kudumu. Matokeo ni kwamba Yehova hutubariki tunapotii Neno lake na tengenezo lake. Kwa kufanya hivyo, tunaonyesha kwamba tunamtii Bwana wetu, Yesu Kristo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki