-
Toeni Dhabihu Ambazo Zampendeza YehovaMnara wa Mlinzi—1989 | Desemba 15
-
-
8. Wewe ungefafanuaje maneno ya Paulo kwenye Waebrania 13:9?
8 Kutobadilika kwa utu na mafundisho ya Yesu kwapasa kutufanye tushikilie yale ambayo yeye na mitume wake walifunza. Waebrania waliambiwa: “Msichukuliwe na mafundisho ya namna nyingine nyingine, na ya kigeni; maana ni vizuri moyo ufanywe imara kwa neema [fadhili zisizostahiliwa, NW], wala si kwa vyakula, ambavyo wao waliokwenda navyo hawakupata faida.”—Waebrania 13:9.
-
-
Toeni Dhabihu Ambazo Zampendeza YehovaMnara wa Mlinzi—1989 | Desemba 15
-
-
10. Kulingana na Waebrania 13:9, ni kitu gani huupa moyo uthabiti?
10 Basi Waebrania walihitaji kuepuka ‘kuchukuliwa na mafundisho ya namna nyingine nyingine, na ya kigeni’ ya watetezi wa mawazo ya dini ya Kiyahudi. (Wagalatia 5:1-6) Ili ubaki ukiwa thabiti katika ukweli, ‘moyo waweza kufanywa imara kwa neema ya Mungu’ wala si kupitia mafundisho hayo. Yaonekana watu fulani walitoa ubishi kuhusu vyakula na dhabihu, kwa kuwa Paulo alisema kwamba moyo haukufanywa imara ‘kwa vyakula, ambavyo wao waliokwenda navyo hawakupata faida.’ Manufaa za kiroho zatokana na ujitoaji kimungu na kuthamini ukombozi, si kutokana na kuhangaikia isivyofaa kula vyakula fulani na kushika siku fulani hususa. (Warumi 14:5-9) Tena, dhabihu ya Kristo ilifanya dhabihu za Walawi ziwe zisizofaa.—Waebrania 9:9-14; 10:5-10.
-