Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wachungaji, Waigeni Wale Wachungaji Wakuu Zaidi
    Mnara wa Mlinzi—2013 | Novemba 15
    • 4. Makala hii itazungumzia nini?

      4 Basi, wachungaji Wakristo wanatazamiwa kuwatendea namna gani kondoo? Washiriki wa kutaniko wanahimizwa ‘wawatii wale wanaoongoza’ katikati yao. Nao wazee Wakristo wanahimizwa waepuke “kupiga ubwana juu ya wale ambao ni urithi wa Mungu.” (Ebr. 13:17; soma 1 Petro 5:2, 3.) Basi, wazee wataliongozaje kundi bila kupiga ubwana? Yaani, wazee watawatunzaje kondoo bila kutumia vibaya mamlaka waliyopewa na Mungu ya kuwa waangalizi?

  • Wachungaji, Waigeni Wale Wachungaji Wakuu Zaidi
    Mnara wa Mlinzi—2013 | Novemba 15
    • 9. Yesu aliwashauri wanafunzi wake wawe na mtazamo gani?

      9 Maoni ya Yesu kuhusu daraka la mchungaji wa kiroho yalikuwa tofauti na maoni ya Yakobo na Yohana. Mitume hao wawili walitaka cheo kikubwa katika Ufalme. Lakini Yesu alirekebisha maoni yao aliposema hivi: “Mnajua kwamba watawala wa kigeni huwaamuru-amuru watu. Na viongozi wao wakuu wana mamlaka kamili juu ya watu wanaowatawala. Lakini msitende kama wao. Ikiwa unataka kuwa mkuu, ni lazima uwe mtumishi wa wengine wote.” (Mt. 20:25, 26, Contemporary English Version) Mitume walihitaji kushinda mwelekeo wa ‘kupiga ubwana juu ya’ wenzao au ‘kuwaamuru-amuru watu.’

      10. Yesu anataka wazee wawatendee kondoo jinsi gani? Paulo aliweka mfano gani katika jambo hilo?

      10 Yesu anatarajia wazee Wakristo walitendee kundi kama alivyolitendea. Ni lazima wawe tayari kuwa watumishi badala ya kuwa mabwana juu ya kundi. Mtume Paulo alikuwa mnyenyekevu. Aliwaambia hivi wanaume wazee wa kutaniko la Efeso: “Ninyi mnajua vema jinsi tangu siku ya kwanza niliyokanyaga wilaya ya Asia nilivyokuwa pamoja nanyi wakati wote, nikimtumikia Bwana nikiwa na unyenyekevu mkubwa zaidi wa akili.” Mtume Paulo alitaka wazee hao wawasaidie wengine kwa bidii na unyenyekevu. Alisema hivi: “Nimewaonyesha ninyi wazi katika mambo yote kwamba kwa kufanya kazi kwa bidii hivyo ni lazima mwasaidie wale walio dhaifu.” (Mdo. 20:18, 19, 35) Paulo aliwaambia Wakorintho kwamba hakuwa bwana juu ya imani yao. Badala yake, alikuwa mfanyakazi mwenzao mnyenyekevu kwa shangwe yao. (2 Kor. 1:24) Paulo aliwawekea wazee leo mfano mzuri katika kuwa wanyenyekevu na kufanya kazi kwa bidii.

  • Wachungaji, Waigeni Wale Wachungaji Wakuu Zaidi
    Mnara wa Mlinzi—2013 | Novemba 15
    • “VIELELEZO KWA KUNDI”

      [Picha katika ukurasa wa 29]

      Wazee huzisaidia familia zao kujitayarisha kwa ajili ya huduma (Tazama fungu la 13)

      13, 14. Ni lazima mzee aliwekee kundi mfano mzuri katika mambo gani?

      13 Baada ya kuwashauri wanaume wazee wa kutaniko ‘wasipige ubwana juu ya wale ambao ni urithi wa Mungu,’ mtume Petro aliwahimiza ‘wawe vielelezo kwa kundi.’ (1 Pet. 5:3) Mzee anawezaje kuwa kielelezo kwa kundi? Fikiria sifa mbili ambazo mwanamume ‘anayejitahidi kufikia cheo cha mwangalizi’ anapaswa kutimiza. Anahitaji kuwa “mwenye utimamu wa akili” na ni lazima awe ‘anaisimamia nyumba yake mwenyewe kwa njia nzuri.’ Ikiwa mzee ana familia, ni lazima aisimamie kwa njia nzuri, “kwa kweli ikiwa mtu yeyote hajui jinsi ya kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje kutaniko la Mungu?” (1 Tim. 3:1, 2, 4, 5) Ili mwanamume astahili kupata cheo cha mwangalizi, ni lazima awe na utimamu wa akili, yaani, awe anaelewa vizuri kanuni za Biblia na anajua kuzitumia maishani mwake. Ni mtulivu na hafanyi maamuzi haraka-haraka. Wazee wanapoonyesha sifa hizo, washiriki wa kutaniko watawaona kuwa wanategemeka.

      14 Wazee huwawekea Wakristo wenzao kielelezo kizuri wanapoongoza pia katika kazi ya kuhubiri. Yesu aliwawekea wazee kielelezo katika kazi hiyo. Kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme ilikuwa sehemu muhimu ya utendaji wa Yesu alipokuwa duniani. Aliwaonyesha wanafunzi wake jinsi ya kufanya kazi hiyo. (Marko 1:38; Luka 8:1) Leo, wahubiri wanatiwa moyo sana wanapohubiri na wazee, wanapoona bidii yao katika kazi hiyo inayookoa uhai, na wanapojifunza mbinu zao za kufundisha. Wazee wanapotumia wakati wao kuhubiri kwa bidii habari njema licha ya kuwa na shughuli nyingi, kutaniko lote linachochewa pia kuwa na bidii. Wazee wanaweza pia kuwawekea mfano mzuri ndugu zao kwa kutayarisha na kushiriki katika mikutano na utendaji mwingine kama vile kusafisha na kutunza Jumba la Ufalme.​—Efe. 5:15, 16; soma Waebrania 13:7.

      [Picha katika ukurasa wa 30]

      Wazee huweka mfano katika kazi ya kuhubiri (Tazama fungu la 14)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki