Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Biblia Ni Ujumbe Kutoka kwa Mungu
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 1. Ikiwa Biblia iliandikwa na wanadamu, kwa nini tunasema ni Neno la Mungu?

      Biblia iliandikwa na watu 40 kwa kipindi cha miaka 1,600 hivi, kuanzia mwaka wa 1513 K.W.K. hadi 98 W.K. Waandikaji hao walitoka katika malezi mbalimbali. Ingawa hivyo, ujumbe walioandika unapatana. Linawezekanaje? Hilo linawezekana kwa sababu Mungu ndiye Mtungaji wa Biblia. (Soma 1 Wathesalonike 2:13.) Waandikaji hao hawakuandika mawazo yao wenyewe. Badala yake, “walisema yaliyotoka kwa Mungu kama walivyoongozwa na roho takatifu.”a (2 Petro 1:21) Mungu alitumia roho yake takatifu kuwaongoza au kuwachochea watu hao waandike mawazo yake.​—2 Timotheo 3:16.

  • Yehova Ana Sifa Gani?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 4. Roho takatifu ni nguvu ya Mungu ya utendaji

      Picha: Mambo yaliyotimizwa na roho takatifu ya Mungu. 1. Sayari na ulimwengu. 2. Mwandikaji wa Biblia akiandika mawazo yaliyoongozwa na Mungu kwenye kitabu cha kukunjwa.

      Kama vile ambavyo sisi hutumia mikono kufanya kazi, Yehova hutumia roho yake takatifu kutimiza mambo. Biblia inaeleza kwamba roho takatifu si mtu, bali ni nguvu ambayo Mungu hutumia kufanya kazi zake. Soma Luka 11:13 na Matendo 2:17, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Mungu ‘ataimimina’ roho yake takatifu juu ya wale wanaomwomba. Basi, unafikiri roho takatifu ni mtu au ni nguvu ya Mungu ya utendaji? Kwa nini unajibu hivyo?

      Yehova hutumia roho yake takatifu kutimiza mambo mengi mazuri. Soma Zaburi 33:6 na 2 Petro 1:20, 21, kisha mzungumzie swali hili:

      • Yehova ametumia roho yake takatifu katika njia gani?

      Picha: Mambo yaliyotimizwa na roho takatifu ya Mungu. 1. Sayari na ulimwengu. 2. Mwandikaji wa Biblia akiandika mawazo yaliyoongozwa na Mungu kwenye kitabu cha kukunjwa.
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki