-
Jihadharini na Walimu Wasio wa Kweli!Mnara wa Mlinzi—1997 | Septemba 1
-
-
3. Ni jambo gani lililotukia wakati uliopita ambalo Petro asema litatukia tena?
3 Baada ya Petro kuwahimiza ndugu zake wakazie uangalifu unabii, yeye asema hivi: “Hata hivyo, kulikuja pia kuwa na manabii wasio wa kweli [katika Israeli la kale], kama pia kutakavyokuwa na walimu wasio wa kweli miongoni mwenu.” (2 Petro 1:14–2:1) Watu wa Mungu wa nyakati za kale walipokea unabii wa kweli, lakini pia walilazimika kushindana na mafundisho yenye kufisidi ya manabii wasio wa kweli. (Yeremia 6:13, 14; 28:1-3, 15) “Katika manabii wa Yerusalemu,” akaandika Yeremia, “nimeona neno linalochukiza sana; hufanya zinaa; huenenda katika maneno ya uongo.”—Yeremia 23:14.
4. Kwa nini walimu wasio wa kweli wanastahili uangamizo?
4 Akifafanua yale ambayo walimu wasio wa kweli wangefanya katika kutaniko la Kikristo, Petro asema hivi: “Hawahawa wataleta ndani kimya-kimya mafarakano yenye kuangamiza na watakana hata mmiliki [Yesu Kristo] aliyewanunua, wakijiletea wenyewe uangamizo wa kasi.” (2 Petro 2:1; Yuda 4) Tokeo la mwisho la ufarakano huo wa karne ya kwanza ni Jumuiya ya Wakristo kama tunavyoijua leo. Petro aonyesha sababu inayofanya walimu wasio wa kweli wastahili sana uangamizo: “Wengi watafuata matendo yao ya mwenendo mlegevu, na kwa sababu ya hao njia ya kweli itasemewa kwa maneno yenye kuudhi.”—2 Petro 2:2.
-
-
Jihadharini na Walimu Wasio wa Kweli!Mnara wa Mlinzi—1997 | Septemba 1
-
-
Kuanzisha Mafundisho Yasiyo ya Kweli
6. Ni nini huwachochea walimu wasio wa kweli, nao hujaribuje kupata wanachotaka?
6 Kwa hekima, twaona jinsi ambavyo walimu wasio wa kweli huanzisha kufikiri kwao kulikofisidiwa. Kwanza Petro asema kwamba wanafanya hilo kimya-kimya, au katika njia ya kujificha, ya hila. Aongeza hivi: “Kwa tamaa watawatumia nyinyi kujifaidi kwa maneno bandia.” Tamaa yenye ubinafsi huwachochea walimu wasio wa kweli, kama ikaziwavyo na The Jerusalem Bible: “Kwa hamu watajaribu kuwahonga kwa faida yao kwa kutumia semi za werevu.” Vivyo hivyo, tafsiri ya James Moffatt yasema hivi hapa: “Katika uchu wao watawatumia kwa kujifaidi kwa mabishano ya ujanja.” (2 Petro 2:1, 3) Huenda maneno ya walimu wasio wa kweli yakaonekana kuwa yenye kustahili kuaminiwa kwa mmoja ambaye hayuko chonjo kiroho, lakini maneno yao yamebuniwa kwa uangalifu ‘ili kuhonga’ watu, kuwashawishi watimize makusudi yenye ubinafsi ya wadanganyaji.
-