-
Jinsi Gayo Alivyowasaidia Ndugu ZakeMnara wa Mlinzi (Funzo)—2017 | Mei
-
-
Inawezekana Gayo alikuwa mzee wa kutaniko, lakini barua hiyo haisemi hivyo kihususa. Yohana alimsifu Gayo kwa kuwakaribisha akina ndugu ingawa hakuwafahamu. Yohana aliona jambo hilo kuwa uthibitisho kwamba Gayo alikuwa mwaminifu, kwa kuwa sikuzote ukarimu huwatambulisha watumishi wa Mungu.—Mwa. 18:1-8; 1 Tim. 3:2; 3 Yoh. 5.
Yohana alithamini ukarimu ambao Gayo aliwaonyesha akina ndugu, na maneno yake yanathibitisha kwamba Wakristo walisafiri mara nyingi kutoka mahali ambapo Yohana aliishi kwenda kwenye makutaniko mbalimbali, na inaonekana wasafiri hao walimwambia Yohana kuhusu safari zao. Inaelekea Yohana alipata habari kuhusu makutaniko kwa njia hiyo.
Kwa kweli, waangalizi wanaosafiri walipenda kuishi na waamini wenzao. Nyumba za wageni zilikuwa na sifa mbaya sana, ziliwahudumia watu vibaya, na zilikuwa na upotovu mwingi wa maadili. Kwa hiyo, ilipowezekana, wasafiri wenye hekima waliishi na rafiki zao na waangalizi wanaosafiri waliishi na Wakristo wenzao.
-
-
Jinsi Gayo Alivyowasaidia Ndugu ZakeMnara wa Mlinzi (Funzo)—2017 | Mei
-
-
Tatu, Wakristo wenzetu wanaomtumikia Yehova kwa ushikamanifu licha ya upinzani wanahitaji kuthaminiwa na kupongezwa kwa uchangamfu kwa sababu ya uaminifu wao. Ni wazi kuwa mtume Yohana alimtia moyo Gayo na kumhakikishia kwamba alikuwa akifanya yaliyo sawa. Vivyo hivyo leo, wazee wa kutaniko wanapaswa kufuata mfano wa Yohana kwa kuwatia moyo ndugu na dada zao ili ‘wasizimie.’—Isa. 40:31; 1 The. 5:11.
-