-
“Ukombozi Wenu Unakaribia”!Mnara wa Mlinzi—2015 | Julai 15
-
-
16, 17. Ni nini kitakachotokea kabla ya ndoa ya Mwana-Kondoo?
16 Baada ya washiriki wote 144,000 kwenda mbinguni, matayarisho ya mwisho kwa ajili ya ndoa ya Mwana-Kondoo yanaweza kuanza. (Ufu. 19:9) Lakini jambo fulani litatokea kabla ya tukio hilo lenye kusisimua. Kumbuka kwamba kabla ya watiwa-mafuta walio duniani kuchukuliwa kwenda mbinguni, Gogu atawashambulia watu wa Mungu. (Eze. 38:16) Kutakuwa na matokeo gani? Watu wa Mungu walio duniani wataonekana hawana ulinzi. Watatii maagizo yaliyotolewa katika siku za Mfalme Yehoshafati: “Hamtahitaji kupigana katika kisa hiki. Simameni mahali penu, simameni tuli, mkauone wokovu wa Yehova kwa ajili yenu. Ee Yuda na Yerusalemu, msiogope wala msiwe na hofu.” (2 Nya. 20:17) Muda fulani baada ya shambulizi la Gogu kuanza watiwa-mafuta wote walio duniani watachukuliwa kwenda mbinguni. Andiko la Ufunuo 17:14 linaeleza jambo litakalotokea mbinguni ili kujibu mashambulizi ya Gogu. Maadui wa watu wa Mungu “watapigana na Mwana-Kondoo, lakini, kwa sababu yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme, Mwana-Kondoo atawashinda. Pia, wale walioitwa na waliochaguliwa na walio waaminifu pamoja naye watawashinda.” Hivyo, Yesu atakuja pamoja na watawala wenzake 144,000 kuwaokoa watu wa Mungu walio duniani.
17 Jambo hilo litaanzisha vita vya Har–Magedoni ambavyo vitalitukuza jina takatifu la Yehova. (Ufu. 16:16) Wakati huo, wale walio mfano wa mbuzi “watakatiliwa mbali milele.” Kisha uovu wote utaondolewa duniani, na umati mkubwa utaokoka Har–Magedoni. Baada ya matayarisho yote kukamilika tutafikia upeo wa kitabu cha Ufunuo, yaani, ndoa ya Mwana-Kondoo. (Ufu. 21:1-4)d Wote watakaookoka Har–Magedoni watafurahia kibali na upendo wa Mungu kwa njia nyingi. Itakuwa ndoa yenye kusisimua kwelikweli! Je, unatazamia kwa hamu wakati huo?—Soma 2 Petro 3:13.
-
-
“Ukombozi Wenu Unakaribia”!Mnara wa Mlinzi—2015 | Julai 15
-
-
d Zaburi ya 45 inaonyesha pia mfuatano wa matukio. Kwanza Mfalme anapigana vita, na kisha ndoa inafungwa.
-