Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuhuisha Mashahidi Wawili
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 23. (a) Inakuwaje kwa mashahidi wawili baada ya siku tatu na nusu, na tokeo ni nini kwa maadui wao? (b) Ni lini Ufunuo 11:11, 12 na unabii wa Ezekieli kuhusu Yehova akipulizia bonde la mifupa mikavu ulipopata utimizo wa ki-siku-hizi?

      23 Vichapo vya umma vilijiunga na viongozi wa kidini katika kuharibu sifa ya watu wa Mungu, nyusipepa moja ikisema: “Tamati ya The Finished Mystery imetolewa.” Ingawa hivyo, hilo lilikuwa mbali sana na ukweli! Wale mashahidi wawili hawakubaki wakiwa wafu. Tunasoma: “Na baada ya siku tatu na nusu roho ya uhai kutoka kwa Mungu iliingia ndani yao, na wao wakasimama kwa nyayo zao, na hofu kubwa ikaanguka juu ya wale waliokuwa wakiona wao. Na wao wakasikia sauti kubwa kutoka mbingu ikisema kwao: ‘Njooni juu huku.’ Na wao wakaenda juu ndani ya mbingu kwa wingu na maadui wao wakaona wao.” (Ufunuo 11:11, 12, NW) Hivyo, wao walikuwa na ono kama lile la mifupa mikavu katika bonde ambalo Ezekieli alitembelea katika njozi. Yehova alipuliza juu ya hiyo mifupa mikavu, nayo ikawa hai, ikiandaa picha ya uzawa mpya wa taifa la Israeli baada ya miaka 70 ya utekwa katika Babuloni. (Ezekieli 37:1-14) Unabii huo muwili, katika Ezekieli na katika Ufunuo, ulikuwa na utimizo wao wa ki-siku-hizi wenye kutazamisha katika 1919, wakati Yehova aliporudisha mashahidi wake ‘waliokufa’ kwenye uhai wenye kusisimua.

      24. Mashahidi wawili walipokuja kwenye uhai tokeo lilikuwa nini kwa wanyanyasi wao wa kidini?

      24 Ulikuwa mshtuko kama nini kwa wanyanyasi hao! Ghafula maiti za mashahidi wawili zikawa hai tena na zenye kutenda. Viongozi wa kidini hao waliona uchungu sana, na zaidi hivyo kwa kuwa wahudumu hao Wakristo ambao walikuwa wametungia hila wawaweke katika gereza walikuwa huru tena, na baadaye wakaondolewa mashtaka kabisa. Mshtuko huo lazima uwe ulikuwa mkubwa hata zaidi wakati, katika Septemba 1919, hao Wanafunzi wa Biblia walipofanya mkusanyiko katika Sida Pointi Ohaiyo, U.S.A. Huko J. F. Rutherford, aliyeachiliwa karibuni, alichochea wakusanyikaji kwa hotuba yake “Kutangaza Ufalme,” iliyotegemea Ufunuo 15:2 na Isaya 52:7. Wale wa jamii ya Yohana wakaanza tena ‘kutoa unabii,’ au kuhubiri peupe. Walizidi kupata imara tena na tena, wakifichua kwa ujasiri unafiki wa Jumuiya ya Wakristo.

  • Kuhuisha Mashahidi Wawili
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • c Angalia kwamba katika kuchunguza yanayopata maono ya watu wa Mungu wakati huu, inaonekana kwamba ingawa miezi 42 huwakilisha miaka mitatu na nusu halisi, siku tatu na nusu haziwakilishi kipindi halisi chenye saa 84. Inaelekea kwamba, kipindi mahususi cha siku tatu na nusu kimetajwa mara mbili (katika mstari wa 9 na 11) kukazia kwamba kingekuwa kipindi kifupi tu kikilinganishwa na miaka mitatu na nusu ya utendaji inayokitangulia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki