Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ufalme wa Mungu Wazaliwa!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 17, 18. (a) Yohana anaripoti tendo-mwitikio gani kwa habari ya anguko la Shetani kutoka katika mbingu? (b) Ni jipi linaloelekea kuwa chimbuko la sauti kubwa anayosikia Yohana?

      17 Yohana anaripoti tendo-mwitikio kwa anguko hili kubwa mno la Shetani: “Na mimi nikasikia sauti kubwa katika mbingu ikisema: ‘Sasa kumetukia wokovu na nguvu na ufalme wa Mungu wetu na mamlaka ya Kristo wake, kwa sababu mshtaki wa ndugu zetu amevurumishwa chini, ambaye huwashtaki mchana na usiku mbele za Mungu wetu! Na wao walishinda yeye kwa sababu ya damu ya Mwana-Kondoo na kwa sababu ya neno la kushuhudu kwao, na wao hawakupenda nafsi zao hata usoni mwa kifo. Kwa minajili hii mwe na nderemo, nyinyi mbingu na nyinyi ambao hukaa ndani yazo!’”—Ufunuo 12:10-12a, NW.

  • Ufalme wa Mungu Wazaliwa!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 20. Wakristo waaminifu wamemshindaje Shetani?

      20 Wakristo wapakwa-mafuta, wanaohesabiwa kuwa waadilifu “kwa sababu ya damu ya Mwana-Kondoo,” wanaendelea kutoa ushuhuda kwa Mungu na kwa Yesu Kristo ijapokuwa minyanyaso. Kwa zaidi ya miaka 120, hii jamii ya Yohana imekuwa ikielekeza kwenye lile suala kubwa linalohusiana na kukoma kwa majira ya Mataifa katika 1914. (Luka 21:24) Na sasa umati mkubwa unatumikia kishikamanifu kando yao. Hakuna wowote wa hawa ‘wanahofu wale wanaoua mwili lakini hawawezi kuua nafsi,’ kama vile maono ya maisha halisi ya Mashahidi wa Yehova katika wakati wetu yameonyesha tena na tena. Kwa neno la kinywa na kwa mwenendo unaofaa wa Kikristo, wao wameshinda Shetani, wakithibitisha bila ugeugeu kwamba yeye ni mwongo. (Mathayo 10:28; Mithali 27:11; Ufunuo 7:9, NW) Wanapofufuliwa kwenda katika mbingu, ni lazima Wakristo wapakwa-mafuta wawe na furaha kama nini, kwa kuwa Shetani hayuko juu kule ili kushtaki ndugu zao! Kweli kweli, ni wakati wa wingi wote wa malaika, kuitikia kwa shangwe mwito: “Mwe na nderemo, nyinyi mbingu na nyinyi ambao hukaa ndani yazo!”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki