-
Ule Msafara Mrefu wa Serikali Kubwa za Ulimwengu Wakaribia MwishoMnara wa Mlinzi—1988 | Juni 1
-
-
Serikali hii hii ya Ulimwengu ya Uingereza-Amerika inasimuliwa katika kitabu cha Ufunuo kama hayawani mwenye “pembe mbili.” Serikali hii kubwa ya ulimwengu yenye sehemu mbili ‘inawaambia wakaao juu ya nchi kumfanyia sanamu’ hayawani wa kisiasa anayewakilisha serikali kubwa zote saba za ulimwengu.—Ufunuo 13:11, 14.
-
-
Ule Msafara Mrefu wa Serikali Kubwa za Ulimwengu Wakaribia MwishoMnara wa Mlinzi—1988 | Juni 1
-
-
Hofu kuu ya miaka minne ya Vita ya Ulimwengu ya kwanza ilipokaribia mwisho wayo, rais wa Amerika Woodrow Wilson na waziri mkuu David Lloyd George walikusudia kuwe na Ushirika wa Mataifa. Lengo layo lilikuwa “kupata amani na usalama wa kimataifa” na hivyo wazuie hofu kuu ya vita kama hiyo isitukie tena.
Ni jambo lenye kupendeza kujua ni nani aliyeanzisha jambo hili. Viongozi hawa wawili walikuwa vichwa vya Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza-Amerika katika historia ya Biblia. Katika njia yenye kustaajabisha sana, jambo hili na mambo mengine ya uhakika kuhusu tengenezo la amani na usalama wa kimataifa yanafaa sana yale ambayo kitabu cha Biblia cha Ufunuo kilikuwa kimesema juu ya “mfalme wa nane” ambaye angeinuka kwa muda mfupi na kuanguka katika siku zetu. Ni nini mengine ya mambo hayo yenye kupendeza yanayolingana?—Ufunuo 17:11, NW.
Unabii wa Ufunuo ulifunua kwamba “hayawani,” mwenye “pembe mbili mfano wa Mwana-Kondoo” ingewaambia “wale wanaokaa juu ya dunia wafanye mfano” kwa hayawani-mwitu, ambaye amekuwa akiongozwa na serikali kubwa saba za ulimwengu katika historia ya Biblia.
Hilo ndilo jambo hususa ambalo Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza-Amerika ilifanya. Iliwasihi “wale wanaokaa juu ya dunia” kufanya Ushirika ambao ulionekana na kutenda katika njia ile ile ambayo serikali kubwa zinatenda. Lakini kwa kweli ilikuwa “mfano wa hayawani-mwitu.” Haikuwa na nguvu yake yenyewe isipokuwa ile tu ambayo ilikuwa imepewa na mataifa mashirika yalo. Haielezwi kuwa huyo anaingia katika mamlaka kupitia ushindi fulani wa kijeshi, kama serikali kubwa za ulimwengu zilivyokuwa zimefanya. Badala yake, inatoka au kuja kutoka kwa zile serikali kubwa saba. Ipo si tu kwa sababu ya ile ya saba kati yazo bali pia kwa mataifa mashirika mengine yanayotia ndani mabaki ya zile sita zinazotangulia. Je! mfano huu wa kisiasa ungefikia ile miradi ya juu ambayo waanzilishi wayo walikuwa wametumainia?—Ufunuo 17:11, 14, NW.
-