Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Habari Njema kwa Aina ya Binadamu Yote!
    Mnara wa Mlinzi—1990 | Januari 1
    • “MIMI nikaona malaika mwingine akiruka katika mbingu ya kati, na yeye alikuwa na habari njema za milele kujulisha wazi kuwa taarifa teremeshi kwa wale ambao hukaa juu ya dunia, na kwa kila taifa na kabila na ulimi na kikundi cha watu.” (Ufunuo 14:6, NW) Kwa maneno hayo, mtume Yohana mzee alieleza njozi yake ya kiunabii iliyovuviwa, njozi yenye kutimizwa katika siku yetu wenyewe. Ni kitulizo kama nini kujua kwamba kuna habari njema katika kipindi hiki cha uhalifu wenye kuongezeka, uchafuzi, uvamizi-haramu, vita, na mashaka yaliyoenea sana kuhusu hali ya uchumi! Lakini ni habari gani zingeweza kuwa njema sana hivi kwamba zahitaji malaika azitangaze? Ni taarifa gani zingeweza kuwa za kuteremesha kwa kiasi cha kustahili kujulishwa wazi kwa kila taifa na kabila na ulimi na kikundi cha watu?

  • Habari Njema kwa Aina ya Binadamu Yote!
    Mnara wa Mlinzi—1990 | Januari 1
    • Kule nyuma katika karne ya kwanza, Yesu alitimiza mengi ya makusudi ambayo Mungu alimkusudia, lakini hakutawazwa kuwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu wakati huo. Kama vile gazeti hili limeonyesha wazi mara nyingi, jambo hilo halikutukia mpaka 1914. Kama vile utimizo wa unabii uonyeshavyo wazi, katika mwaka huo Ufalme wa Mungu ulisimamishwa imara katika mbingu. (Ufunuo 12:10, 12) Ingawa zilikuwako habari mbaya sana katika 1914​—kutokea kwa Vita ya Ulimwengu 1​—uzaliwa wa Ufalme wa Mungu ulikuwa ndizo habari bora zaidi. Ndiyo sababu Yesu alitoa unabii huu kwa siku yetu: “Habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote.”​—Mathayo 24:14.

      Je! unabii wa Yesu umetimizwa? Jibu ni ndiyo! Na njozi ya kiunabii ya Yohana imetimizwa pia. Ni kweli kwamba sisi hatuwezi kumwona malaika asiyeonekana ambaye Yohana alimwona. Lakini Mashahidi wa Yehova wamekuwa wakionekana sana kwa kuwa wametangaza habari njema ambazo yule malaika anazo “kwa kila taifa na kabila na ulimi na kikundi cha watu.” Katika mabara 212 na visiwa vya bahari, sauti zao zimesikiwa. Na umati wa watu unaitikia. Maono ya baadhi ya watu hawa yataonyesha ni jinsi gani hasa habari njema kuhusu Ufalme wa Mungu zilivyo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki