BIBLIOTEKE YA KU ENTERNETE Watchtower
Watchtower
BIBLIOTEKE YA KU ENTERNETE
Swahili (Katanga)
  • BIBLE
  • BITABU
  • MA RENION
  • w25 Octobre pp. 12-17
  • Mungu ashitachaka kutupenda

Akuna video nju ya iyi selection.

Pardon, kurikuwa erreur mu chargement ya video.

  • Mungu ashitachaka kutupenda
  • Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
  • Sous-titres
  • JEOVA ANAKUPENDAKA SANA, ILE NI FUNDISHO YA MUNENE YA MU BIBLE
  • WAZA SANA NJU YA NAMNA JEOVA “ANAKUPENDA”
  • YUWA KULE MA DUTE YAKO IKO NATOKEA
  • BAKIA MWAMINIFU KWA JEOVA
Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
w25 Octobre pp. 12-17

ABARI YA KUFUNDA YA 41

MWIMBO 108 Mungu Iko na Upendo Mushikamanifu

Mungu ashitachaka kutupenda

“Mumupikie Jeova merci, nju eko muzuri; mapendo yake ya bya kweri ni ya milele.”​—ZB. 136:1.

MU KIFUPI

Jeova anatupendaka sana, ile ni fundisho ya munene ya mu Bible. Kukumbuka vile kutatusaidie tuvumirie ata kama tunapata magumu.

1-2. Bakristo bamingi banajishikiaka je wakati ya magumu?

WAZIA bato iko pa mayi na mpepo ya nguvu inanza, ile mpepo inanza kutupatupa bato. Kama abatupe kyuma kile kinashimamishaka bato, ile bato itaenda kote kule mpepo itaipeleka. Kile kyuma kitafanya bato ishitenke na ishende kule mpepo inaipeleka.

2 Kama na weye uko mu mateso unezi kujishikia sa ile bato. Mawazo yako aitakuwa fashi moya. Leo unezi kujishikia muzuri na uko sire asema Jeova anakupenda na eko nakwangaikia lakini kesho, unezi kujishikia mubaya na unanza kujiuliza: Eske Jeova eko naniona na eko naona ile mambo iko nanifikia? (Zb. 10:1; 13:1) Leo, rafiki yako anezi kuya kukwankurajé na unapatako ka nguvu. (Mez. 17:17; 25:11) Lakini kesho, ma dute inezi kukurudiria na unanza kujiuliza tu kama bya kweri Jeova eko nakwangaikia. Unezi ata kwanza kuwaza asema pengine Jeova ashakukwacha. Sa vile kile kyuma kinashimamishaka bato na weye utafanya nini nju ushianze kwangaika na mawazo? Ao tena ni nini inezi kukusaidia utoshe ma dute na uendelee kuwa sire asema Jeova anakupenda na eko nakwangaikia?

3. Zaburi 31:7 na 136:1, inatufundisha nini nju ya mapendo ya bya kweri ile Jeova eko nayo, na nju ya nini tunezi kusema kama akuna muntu ata moya anamupita Jeova mu kuonesha mapendo ya bya kweri? (Angaria na foto.)

3 Kintu kimoya kile kinezi kukusaidia ushiangaike na mawazo saa uko mu magumu, ni kukumbuka asema Jeova anekalaka na mapendo ya bya kweri. (Soma Zaburi 31:7; 136:1.) Mu Bible misemo “mapendo ya bya kweri,” inapenda kuonesha mapendo ile muntu anekalaka nayo kwa mwingine, na ile inafanyaka muntu alamatane na mwingine pashipo kumwacha ata shiku moya. Kusema tu bya kweri akuna ule anamupita Jeova mukonesha mapendo ya bya kweri. Njo pale Bible inasema Jeova eko na “mapendo ya mingi ya bya kweri.” (Kut. 34:6, 7) Bible inasema tena ivi nju ya Jeova: “Uko na mapendo ya mingi ya bya kweri ku bale bote beko nakuriria.” (Zb. 86:5) Njo kusema nini? Ni kusema Jeova ashitaachaka ata shiku moya batumishi bake baaminifu! Kukumbuka asema Jehova anakupendaka sana na ashitakwachaka, kutakusaidia ushiangaike na mawazo saa uko na magumu.​—Zb. 23:4.

Kyuma kile banashimamishaka nakyo bato, kiko mu mayi nju ya kusaidia bato ishitenke-tenke saa ya mpepo.

Sa vile kyuma kile banashimamishaka nakyo bato kinasaidiaka bato ishitenke-tenke sa kuko mpepo, na shiye kama tuko sire asema Jeova anatupenda atutangaika na mawazo wakati ya magumu (Angaria paragrafe 3)


JEOVA ANAKUPENDAKA SANA, ILE NI FUNDISHO YA MUNENE YA MU BIBLE

4. Taya mafundisho ya munene ya mu Bible, na nju ya nini bantu abezi tena kutulanda kama tushakwamini ile mafundisho?

4 Jeova anatupendaka sana. Kukumbuka ile fundisho ya munene ya mu Bible kunezi kutusaidia tushiangaike saa tunapata magumu. Mafundisho ya munene ya mu Bible njo nini? Pengine unakumbuka mambo ile unamini ile ushakufunda mu Bible. Kwa mufano urifunda asema njina ya Mungu ni Jeova, Yesu njo mutoto moya tu wa pekee wa Mungu, bafu abayuwake kintu, dunia itakuwa paradi mule bantu bataishi milele. (Zb. 83:18; Muh. 9:5; Yoh. 3:16; Ufu. 21:3, 4) Kisha tu kwamini ile mambo haikuwake teketeke tena muntu akuwe akulande. Nju ya nini? Nju urifikia kuvumbula asema ile mafundisho yote ni ya bya kweri. Mapendo ya Jeova nayo ni fundisho ya munene ya mu Bible. Tuone sasa namna kuyuwa vile kunezi kukusaidia ukuwe sire asema Jeova anayuwa magumu yako na atakusaidia.

5. Espliké vile muntu anezi kufikia kwachana na mafundisho ya bongo.

5 Saa urianzaka kufunda Bible, nini njo irikusaidiaka kwachana na mafundisho ya bongo? Pengine ni saa urikomparé mambo ile barikufundishaka mu kanisa yako na mambo ile Bible inafundisha. Tubebe mufano, tuseme urikuwa ushakwamini asema Yesu njo Mungu Mweza Yote. Saa urianza kufunda Bible pengine urijiulizaka ivi: Eske bile minamini ni bya kweri tu?’ Sa uriendelea kufunda Bible urifikia kuvumbula asema bile urikuwaka ushakwamini ni bya bongo. Sasa urifanya nini? Uriachana na mafundisho ya bya bongo ile urikuwa ushakwamini na uriamini sasa iyi mafundisho ya bya kweri ya mu Bible: Yesu njo “mutoto wa kwanza mu biumbe byote.” (Kol. 1:15; Yoh. 3:18) Kusema tu bya kweri, mafundisho ya bongo inaoteshaka mijiji na inekalaka nguvu kwa muntu kuitosha. (2 Ko. 10:4, 5) Lakini kama unaitosha, autairudiriaka tena.​—Flp. 3:13.

6. Nju ya nini tunezi kuwa sire asema Jeova ashitachaka kupenda batumishi bake?

6 Kama uko mu magumu na unanza kuwaza asema Jeova ashikupende tena unezi kufanya vile urifanyaka pale urianza kufunda Bible. Komparé mambo ile Bible inasema nju ya namna Jeova anakupenda na mawazo ile uko nayo. Ujiulize ivi: Eske bya kweri tu Jeova ashinipende?’ Komparé mawazo yako na mambo ile Zaburi 136:1 inasema, andiko ya munene ya iyi abari. Waza ni nju ya nini ile andiko inasema kama mapendo ya Jeova ni ya bya kweri, na nju ya nini Zaburi ya 136 inataya ile mapendo mala ya mingi. Sa vile turiona, mapendo ya bya kweri ile Jeova eko nayo nju ya batumishi yake ni fundisho ya munene ya mu Bible. Na iko pamoya na mafundisho ingine ya munene ya mu Bible ile ushakwamini. Kuwaza asema uko wa bule na Jeova ashikupendake ni mawazo ya bongo. Tosha ile mawazo mu kichwa sa vile uritoshaka mafundisho ya bongo ile haipatane na Bible!

7. Leta mufano ya mandiko ile inatusaidia tuyuwe asema Jeova anatupendaka sana.

7 Mu Bible muko mambo ingine ya mingi ile itatusaidia tukuwe sire asema Jeova anatupenda. Kwa mufano, Yesu arioneshaka banafunzi bake ivi: “Muko ba lazima sana kupita ba moineaux ba mingi sana.” (Mt. 10:31) Jeova ye mwenye arioneshaka batumishi bake ivi: “Mitakupachia nguvu, bya kweri tu mitakusaidia, mitakubamba nguvu na mukono yangu ya droite, mukono ile iko natenda na jistise.” (Isa. 41:10) Ile mandiko inaonesha muzuri sana vile Jeova na Yesu banatupendaka sana. Yesu ashikuseme ‘munezi kuwa balazima,’ na Jeova ashikuseme ‘minezi kumisaidia.’ Lakini Yesu arisema: “Muko balazima sana ” na Jeova arisema “mitakusaidia.” Kama mu magumu urishakujishikia sa vile Jeova ashikupende, ile mandiko aitakusaidia tu ujishikie muzuri, lakini itakusaidia ukuwe sire asema Jeova anakupendaka sana. Ile mandiko ailande apana, inasema mambo ya bya kweri. Kama unasali Jeova akusaidie utoshe ma dute na kama unawaza sana nju ya iyi mandiko, na weye utafikia kusema vile 1 Yohana 4:16 inasema: “Turifikia kuyuwa asema Mungu anatupendaka sana, na turifikia kwamini ile mambo.”a

8. Utafanya nini kama unanza kuwaza asema Jeova ashikupende?

8 Alafu kama ma saa moya, unaendele kuwaza paka asema Jeova ashikupendake? Kama bya vile binakufikia, komparé mawazo ile uko nayo na bile unayuwa nju ya Jeova. Mawazo inashanjaka, lakini mambo ya bya kweri yo aishanjake. Pale Bible inatufundisha asema Jeova anatupendaka inasema bya kweri ailande apana. Kama atwamini asema Jeova ashakutupenda iko sa atuyuwe muzuri sifa yake ya munene sana, ni kusema mapendo.​—1 Yo. 4:8.

WAZA SANA NJU YA NAMNA JEOVA “ANAKUPENDA”

9-10. Saa Yesu arisema mu Yohana 16:26, 27 asema: “Baba ye moya ashakumipenda sana.” Aripendaka kusema nini? (Angaria na foto.)

9 Kama tunawaza nju ya mambo ile Yesu arioneshaka banafunzi bake, tutafikia kuyuwa ya kusema Jeova anatupendaka sana. Yesu arisema: “Baba ye moya ashakumipenda sana.” (Soma Yohana 16:26, 27.) Yesu ashikusemake vile nju tu ya kufuraisha banafunzi bake. Kama tunasoma mandiko ile inatanguria ile andiko tutafikia kuona asema Yesu ashikwanzake kusemea namna banafunzi yake barianza kjishikia, lakini arianzaka kusema nju ya mambo ingine, na ile mambo irikuwaka ni sala.

10 Mu ile andiko, Yesu aritokea kuonesha banafunzi bake ya kusema banapashwa kuomba mu njina yake lakini abapashwe kumuomba yeye. (Yoh. 16:23, 24) Irikuwa kintu kya lazima sana bayuwe vile nju kisha Yesu kufufuka, banafunzi bake baripashwa kuwa tanté kwanza kumomba Yesu. Kusema tu bya kweri, barimuyuwa Yesu muzuri na arikuwa rafiki yabo. Pengine baripashwa kuwaza asema vile Yesu aribapenda, atapenda kushikia maombi yabo na ataipeleka kwa Baba yake. Lakini Yesu aribambia asema abapashwe kuwaza vile. Nju ya nini? Nju aribambia ivi: “Baba ye moya ashakumipenda sana.” Mambo ile Yesu arisemaka iko mu mafundisho ya munene sana ile Bible inafundisha nju ya sala. Kuyuwa vile kunezi kukusaidia je? Kufunda Bible kurikusaidia umuyuwe Yesu na umupende. (Yoh. 14:21) Lakini sa vile banafuzi ba wakati ya nzamani, ukuwe sire asema sa unamulomba Mungu atakushikia nju “ye mwenyewe anakupendaka sana.” Kila wakati ile unasali kwa Jeova, unaonesha asema unamini kama anakupendaka sana.​—1 Yo. 5:14.

Foto: Nduku moya ashakwikala pa kichi inje ya nyumba yake na eko nasali nju ya mambo ya lazima mu maisha. 1. Anamuletea bibi yake ule eko malari byakurya. 2. Mutoto yake mwanamuke eko nafuraia kufunda Bible pamoya naye. 3. Eko nangaria makuta ile eko nayo na ma dépense ile anapashwa kufanya.

Unezi kuomba Jeova na uko sire asema “ye mwenyewe anakupendaka sana” (Angaria paragrafe 9-10)b


YUWA KULE MA DUTE YAKO IKO NATOKEA

11. Nju ya nini Shetani atafurai sana kama tunawaza asema Jeova ashitupendake?

11 Ni nini njo inezi kufanya tuduté asema Jeova anatupendaka? Kama unawaza asema ile ma dute inatoka kwa Shetani, aulande, njo kule inatokeaka. Shetani ‘eko natafuta kutumeza’ na anapenda tuwaze asema Jeova ashitupende. (1 Pe. 5:8) Waza ata weye, nju Jeova ashakutupenda sana, njo pale aritutolea bei ya ukombozi. Lakini Shetani anapenda tuwaze asema tuko na manzambi ya mingi sana, na atumerité ata ile bei ya ukombozi. (Ebr. 2:9) Lakini kama tunanza kuwaza asema Mungu ashitupende nani njo atafurai? Ni Shetani. Na nani njo atafurai kama tunakuwa dekurajé sana na tunacha kumutumikia Jeova? Ni Shetani. Waza ata weye, Shetani eko napenda tuwaze asema Jeova ashitupende. Ile ni bongo nju ni yeye njo Jeova ashipende. Lakini mu “matendo [yake] ya kulanda” anapenda tuwaze asema shiye njo Jeova ashipendake na tuwaze kama Jeova ashakututupa. (Efe. 6:11) Kuvumbula ya kusema ile njo mawazo Shetani anapenda tukuwe nayo kunatupachia nguvu ya “kujioposé kwa ibilisi.”​—Yak. 4:7.

12-13. Nzambi ile Adam na Eve barituachia inezi kufanya tujishikie je?

12 Kuko kintu kingine kile kinezi kufanya tuduté asema Jeova ashakutupenda. Ni kintu kani? Ni nzambi ile bazazi yetu ba kwanza barituachiaka. (Zb. 51:5; Ro. 5:12) Nzambi iriaribisha burafiki bwa muntu pamoya na Mungu. Lakini tena inafanyaka tukuwe na mawazo ya mubaya, twanze kujishikia mubaya ku roo na inaribishaka ata santé yetu.

13 Nzambi inafanyaka tujishikie mubaya. Tujishikie kuwa na nkosa, twangaike na mawazo, turione ba bule, na tushikie aya. Tunajishikiaka vile kisha kufanya nzambi. Tunajishikiaka tena vile saa tunakumbuka asema tuko batenda-nzambi. Lakini, Jeova ashikutuumbake nju twanze kujishikia vile. (Ro. 8:20, 21) Sa tu vile motoka ile iko na mupeto ya kutoboka aiwezi kutembea vile ule ariifanyaka aripendaka itembee; na shiye nju atukamilike, atuwezi kuwa sa vile Jeova aripendaka tukuwe sa arituumbaka. Njo pale saa moya tunanzaka kujiuliza asema: Eske Jeova anatupendaka? Kama tunanza kujiuliza vile, tunapashwa kukumbuka asema Jeova ni “Mungu mukubwa na wa kongopesha sana, Mungu ule aneshimiaka mapatano yake, na ule anaoneshaka mapendo ya bya kweri bale banamupenda na kufwata bile anasema.”​—Ne. 1:5.

14. Kuwaza sana nju ya bei ya ukombozi kunezi kutusaidia je tutoshe mawazo ya kusema Jeova ashiwezi kutupenda? (Waroma 5:8) (Angaria na mu ankadré “Pikanisha ‘nguvu ya nzambi ya kupotesha bantu.’”)

14 Saa moya, tunezi kushikia mubaya nju tunawaza asema Jeova ashipashwe ata kutupenda. Ku sema tu bya kweri akuna ule anastaili mapendo ya Jeova. Na ile njo inafanya mapendo ya Jeova ikuwe ya maana sana kwetu. Akuna ata kintu kimoya kile tunezi kufanya nju Jeova atupende. Ata vile Jeova aritoa bei ya ukombozi nju ya kututosha mu manzambi, na arifanya vile nju anatupenda. (1 Yo. 4:10) Tena, kumbuka asema Yesu ashikukuyake nju ya kusové bale bashakukamilika, lakini arikuya nju ya kusové batenda-nzambi. (Soma Waroma 5:8.) Kusema tu bya kweri, akuna ata muntu moya ule anezi kufanya paka bintu bya kunyoloka, Jeova ye mwenyewe ashichungake tufanya vile. Saa ali yetu ya nzambi inanza kufanya tuwaze ya kusema Jeova ashitupendake, tufanye nguvu yetu yote nju tutoshe ile mawazo mu akiri.​—Ro. 7:24, 25.

Pikanisha “nguvu ya nzambi ya kupotesha bantu”

Bible inasema nju ya “nguvu ya nzambi ya kupotesha bantu.” (Ebr. 3:13) Zaidi ya kutusukuma tufanye nzambi, kukosa kukamilika kunezi kutufanya twendelee kuduté asema Jeova anatupenda. Kusema tu bya kweri nzambi iko na ‘nguvu ya kupotesha bantu.’

Tunezi kuwaza asema bengine abawezi kutusukuma kufanya bibaya, kwa mufano unezi kuwaza pengine asema akuna ata muntu moya atawezaka kukurimba. Lakini kama atuna bakalamushi, muntu anezi kuturimba na tunapotesha makuta.

Njo pamoya na shiye, tunapashwa kuwa bakalamushi nju kukosa kukamilika kwetu kushitulande, ni kusema kushitufanye twanze kuwaza asema Jeova ashitupende. Kukosa kukamilika kunezi kutufanya twanze kuwaza sana nju ya mankosa yetu na buzaifu bwetu. Lakini ile njo “nguvu ya nzambi ya kupotesha bantu,” na tunapashwa kwachana na ile mawazo.

BAKIA MWAMINIFU KWA JEOVA

15-16. Tunezi kuwa sire na nini kama tunabakia baminifu kwa Jeova, na nju ya nini? (2 Samweli 22:26)

15 Jeova anapenda ‘tulamatane naye.’ (Kum. 30:19, 20) Ile njo desizion ya muzuri sana ile tunezi kubeba. Kama tunafanya vile Jeova ashitatwachaka ata shiku moya. (Soma 2 Samweli 22:26.) Kama tunendelea kubakia baminifu kwa Jeova, tunezi kuwa sire asema atatusaidia kuvumiria magumu yote ile inezi kutufikia mu maisha.

16 Saa vile turiona, kuko mambo mingi ile inezi kutusaidia tushiangaike na mawazo saa tunapata magumu. Tunayuwa asema Jeova anatupenda na atatusaidia. Njo vile Bible inafundisha. Kama tunanza kuwaza asema Jeova ashitupende, tukumbuke mambo ya bya kweri ile tunayuwa nju ya Jeova, kuriko vile tunajishikia ile wakati. Tukuwe sire asema Jeova ashitachaka kutupenda ata shiku moya, ile ni fundisho ya munene sana ya mu Bible.

UTAJIBU JE?

  • Kukumbuka asema Jeova anatupenda ni fundisho ya munene ya mu Bible kunezi kutusaidia je?

  • Nzambi ile Adam na Eve barituachia inezi kufanya twanze kuwaza nini nju ya mapendo ya Jeova?

  • Tunezi kufanya nini nju tutoshe mawazo ya kusema kama Jeova ashitupendake?

MWIMBO 159 Jeova merci!

a Mifano ingine iko mu Kumbukumbu la Torati 31:8, Zaburi 94:14, na mu Isaya 49:15.

b ESPLIKASION YA FOTO: Nduku moya eko nasali nju Jeova amusaidie kwangaikia bibi yake ule eko malari, kutumikisha muzuri makuta, na kufundisha mutoto yake nju amupende Jeova.

    Swahili (Katanga) Publications (2020-2026)
    Toka
    Ingia
    • Swahili (Katanga)
    • Partajé
    • Preferanse
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni ya kutumikisha
    • Règles de confidentialité
    • Paramètres de confidentialité
    • JW.ORG
    • Ingia
    Partajé