BIBLIOTEKE YA KU ENTERNETE Watchtower
Watchtower
BIBLIOTEKE YA KU ENTERNETE
Swahili (Katanga)
  • BIBLE
  • BITABU
  • MA RENION
  • w25 Octobre pp. 6-11
  • Jeova anezi kutusaidia tukuwe na “furaa ya bya kweri”

Akuna video nju ya iyi selection.

Pardon, kurikuwa erreur mu chargement ya video.

  • Jeova anezi kutusaidia tukuwe na “furaa ya bya kweri”
  • Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
  • Sous-titres
  • Ya kufanana na iyi
  • KULE FURAA YA BYA KWERI INATOKAKA
  • USHIACHE ATA KINTU KIMOYA KIKUPOTESHEE FURAA YAKO
  • Endelea kuwa na furaa ata kama unazeka
    Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
w25 Octobre pp. 6-11

ABARI YA KUFUNDA YA 40

MWIMBO 111 Mambo Yenye Kufanya Tukuwe na Furaha

Jeova anezi kutusaidia tukuwe na “furaa ya bya kweri”

‘Mitakuya . . . kwa Mungu . . . kwake kunatoka furaa yangu ya mingi sana.’​—ZB. 43:4.

MU KIFUPI

Tutaona bile binezi kutupoteshea furaa na tutaona mambo ile inezi kutusaidia tupate tena furaa yetu kama tushakuipotesha.

1-2. (a) Leo, bantu bamingi beko najishikia je? (b) Tutafunda nini mu iyi abari?

LEO, bantu banafanyaka yabo yote nju ya kuwa na furaa. Ata vile, abekalake na furaa ya bya kweri. Lakini, bantu bamingi leo beko njo na uzuni, na abana ata na kitumaini asema batapataka furaa. Ata na batumishi ba Jeova nabo banezi kujishikia vile. Nju tuko naishi mu “mashiku ya mwisho,” na shiye tunezi kupata magumu ile inezi kufanya tupoteshe furaa yetu.​—2 Ti. 3:1.

2 Mu iyi abari, tutaona mambo ile inezi kufanya tupoteshe furaa yetu na mambo ile tunezi kufanya nju tupate tena furaa kama tushakuipotesha. Mbele ya kufika kule, mwache tuone mbele kule furaa ya bya kweri inatokaka.

KULE FURAA YA BYA KWERI INATOKAKA

3. Bintu bile Jeova ariumba binatufundisha nini? (Angaria na mafoto.)

3 Jeova ashiyakosaka furaa ata shiku moya. Na anapenda na shiye tukuwe na furaa ya bya kweri. Tunayuwa vile je? Ariumba bintu bya mingi nju tukuwe na furaa. Kwa mufano, tunashikiaka furaa sana saa tunaona marangi ya kwacha-achana ile iko mu dunia, saa tunaona banyama beko nacheza na saa tunakurya byakurya bile tunapendaka. Bile byote binaonesha asema Mungu anatupendaka sana na anapenda tukuwe na furaa.

Foto: Banyama bamingi banapendaka kucheza. 1. Katoto ka ntembo keko nachezea mu mayi. 2. Tu ba penguin tuko nachezea mu ma neige. 3. Tutoto twa mbuji tuko nacheza na kuluka-luka mu mashamba. 4. Ba dauphin beko naluka mu mayi.

Katoto ka ntembo: Image © Romi Gamit/​Shutterstock; tu ba penguin tutoto: Vladimir Seliverstov/​500px via Getty Images; tutoto twa mbuji: Rita Kochmarjova/​stock.adobe.com; ba dauphin bawiri: georgeclerk/​E+ via Getty Images

Saa tunaona banyama beko nacheza, inatukumbusha asema Jeova ni Mungu wa furaa (Angaria mu paragrafe 3)


4. (a) Nju ya nini Jeova ashipoteshake furaa yake ata kama eko naona bantu beko nateswa? (b) Jeova anatupachiaka nini? (Zaburi 16:11)

4 Ata kama Jeova ni “Mungu wa furaa,” anayuwa muzuri mateso na mambo ile iko naangaisha bantu mu dunia leo. (1 Ti. 1:11) Lakini, ashiachake ata kiloko ile mambo imupoteshee furaa yake. Nju ya nini? Nju anayuwa asema mateso ni ya wakati kiloko. Na ni ye mwenyewe njo ashakuwekaka shiku ile itaishaka. Lakini leo, anaangaikiaka vile tunarishiaka. Na kama tuko nateswa, anekalaka pale nju ya kutusaidia. Sasa, anatusaidiaka je? Anatupachiaka furaa. (Soma Zaburi 16:11.) Tuone vile arimupachiakayo Yesu.

5-6. Ni nini njo inafanyaka Yesu akuwe na furaa?

5 Mu biumbe byote bya Jeova, Yesu njo anekalaka na furaa sana kupita biumbe byote. Nju ya nini? Tuone iyi ma rezon mbiri. Ni nju (1) “Yeye ni mufano wa Mungu ule ashionekanake,” ni kusema, eko tu paka sa Baba yake na njo pale eko na furaa sana. (Kol. 1:15; 1 Ti. 6:15.) (2) Yesu njo ashakwikalaka wakati ya mingi sana kupita muntu mwingine wowote pamoya na ule anapachianaka furaa ya bya kweri, ni kusema, Baba yake Jeova.

6 Tena, Yesu anekalaka kila shiku na furaa nju anafanyaka paka bile Baba yake anapendaka afanye. (Mez. 8:30, 31; Yoh. 8:29) Njo pale Jeova anamupendaka sana na ile inamuongezeaka tena Yesu furaa.​—Mt. 3:17.

7. Tunezi kufanya nini nju tupate furaa ya bya kweri?

7 Na shiye tunezi kupata furaa kama tunaendelea kuwa karibu na Jeova, nju ye njo analetaka furaa. Kama tunanza kupitisha wakati ya mingi mu kufunda nju ya Jeova, na kama tunanza kumufwatirisha, na shiye tutakuwa na furaa ya bya kweri. Tutapata tena furaa kama tunafanya mambo ile Mungu anapendaka, na kama tunakumbuka asema Mungu anatupendaka sana.a (Zb. 33:12) Kusema tu bya kweri, saa ingine tunezi kushikia uzuni na kuona sa mambo aiendeke. Na ile uzuni inezi kufanya mashiku kiloko ao inezi ata kukawia sana. Kama tunanza kujishikia vile, ni kusema Jeova ashitupende tena? Apana, aina vile! Shiye bote atukamilike. Njo maana, saa ingine tunezi kushikia uzuni ku roo ao kupata ata dépression. Jeova anatuyuwa muzuri na anatukomprandraka. (Zb. 103:14) Tuone sasa mambo ile inezi kutupoteshea furaa yetu na tuone kile tunezi kufanya nju ya kupata tena furaa yetu.

Mambo ile tunezi kufanya nju Jeova atupachie furaa

Umulombe Jeova akupachie roo yake takatifu. Tunapashwa kumulomba Jeova atupachie furaa nju furaa ni kipande kya tunda ya roo takatifu. (Gal. 5:22) Kama tuko na roo takatifu ya Jeova, tunezi ‘kuchunga na kuvumiria sana na tuko na furaa’ ata kama tuko na magumu.​—Kol. 1:11.

Weka kaji ya Jeova pa fashi ya kwanza mu maisha yako. Soma sauti ya Mungu kila shiku na bitabu byetu. Ujitoe mu kaji ya kuubiri “abari njema ile inaleta furaa” kupatana na uwezo yako. (Lu. 2:10) Bantu bale banekalaka na furaa sana mu iyi dunia ni bale banekaka kaji ya Jeova pa fashi ya kwanza mu maisha yabo.​—Zb. 65:4.

Umushikie Jeova kila wakati. Kumbuka asema mambo ile Jeova anakulomba ufanye ni nju ya faida yako. Jeova ashikutupachiake masheria yake nju ya kutufunga-funga. Lakini kama tunaifwata, tutakuwa na furaa.​—Lu. 11:28.

USHIACHE ATA KINTU KIMOYA KIKUPOTESHEE FURAA YAKO

8. Magumu ya mu maisha inezi kufanya tujishikie je?

8 Kintu kya kwanza kile kinezi kutupoteshea furaa yetu ni magumu ya maisha. Eske, beko nakuteswa nju uko namutumikia Jeova? Ao uko nateswa nju ya ma catastrophe naturel, bumashikini, malari, ao nju ya buzee? Iyi magumu yote inezi kutupoteshea furaa yetu na kutufanya twanze kuuzunika sana, surtout saa atuna na kile tunezi kufanya nju ya kwisha ile magumu. Bible inasema, magumu inezi kutufanya tukuwe na uzuni sana na kutufanya tuwaze asema atutapataka tena furaa. (Mez. 15:13) Nduku Babis, muzee moya wa mu kutaniko, arifwishaka mukubwa yake na bazazi yake bote bawiri mu miaka 4. Kisha kupata ile magumu, arisemaka ivi: “Nirishikiaka sa niko mi moya na akuna muntu ule anezi kunisaidia. Nirishikiaka mubaya sana nju niripendaka kupitisha wakati ya mingi pamoya na bazazi yangu na mukubwa yangu mbele bakufwe. Lakini, mishikuwezake kufanya vile.” Sa ile mambo irimupata ule muze, na shiye magumu ya maisha inezi kutuchokesha na kufanya tujishikie mubaya.

9. Tunezi kufanya nini nju tupate tena furaa? (Yeremia 29:4-7, 10)

9 Ni nini inezi kutusaidia tupate tena furaa? Kama auna na kintu kile unezi kufanya nju ya kwisha magumu yako, acha kuwaza nju ya ile mambo. Lakini umupikie tu Jeova merci nju ya bile uko nabyo. Ukifanye vile, utapata tena furaa. Mu iyi dunia, bantu banawazaka asema nju ya kuwa na furaa ailombe kuwa na magumu mu maisha. Lakini ile ni bongo! waza nju ya iyi mufano, saa batoto ya Israel barikuwaka mu butumwa kule ku Babilone. Jeova aribaoneshaka bafuraie maisha ata kama barikuwa batumwa. (Soma Yeremia 29:4-7, 10.) Ile inatufundisha nini? Wakati ya magumu, apana tu kwangaria paka bibaya bile biko mu maisha yako. Angariako na bizuri bile uko nabyo na umupikie Jeova merci. Kumbuka asema Jeova ashitakwacha, atakusaidia. (Zb. 63:7; 146:5) Dada Effie, arifanyaka aksidan ile irifanyaka abakie wa kupoza. Arisemaka ivi: “Jeova, famiye yangu, na banduku na badada mu kutaniko, barinisaidiaka sana. Niriwaza asema kama minabakia tu na uzuni, mitaonesha asema byote bile barinifanshia ni bya bule. Nju ya kubapikia merci, mirifanya nguvu yangu yote nju nishikuwe tena wa mauzuni-uzuni.”

10. Nju ya nini tunezi kuwa paka na furaa ata kama tuko na magumu?

10 Ata kama maisha yetu aina vile turipendaka ikuwe, ao ata kama magumu ya mingi inatufikia mu famiye, tunezi tu kuwa paka na furaa.b (Zb. 126:5) Nju ya nini tunasema vile? Ni nju, mambo ile inatupataka mu maisha aina ile njo inatuleteaka furaa ya bya kweri. Ona vile Maria, painia moya, arisema: “Kama unabakia na furaa ata wakati uko na magumu, aina kusema ile magumu aikufanye kintu, lakini ni kusema auyasabu bile Jeova ashakukulaka. Baba yetu Jeova atatusaidia nju tushipoteshe furaa yetu.” Ata kama bushiku bunakawia je, bipande bishuke, paka butakachika. Njo pamoya na weye! Ata kama mambo inakupitia je, kumbuka asema, bipande bishuke, paka itaisha. Mu mashiku kiloko, Jeova atatosha magumu yote ile iko natwangaisha.

11. Mufano ya Paul inakusaidia je?

11 Wakati ingine, magumu inezi kutupitia mu maisha na tunanza kuwaza asema Jeova ashakututupa. Eske ni bya kweri? Kama njo vile uko nawaza, mifano ya batumishi ba Jeova ba nzamani bale baripataka magumu ya nguvu, inezi kukusaidia. Ona mufano ya Paul. Yesu ye moya njo arimuchakulaka nju aubiri abari njema “ku bantu ba mataifa, na ku bafalme, na ku batoto ba Israel.” (Mdo. 9:15) Ile irikuwaka kaji ya maana sana! Ata vile, Paul aripata magumu ya mingi na pengine ashikuwaziake ata asema inezi kwisha. (2 Ko. 11:23-27) Sasa, vile aripataka ile magumu yote, ni kusema Jeova arikuwaka ashakumutupa? Apana! Nju Paul ariwezaka kuvumiria ile magumu yote, ile irionesha asema Jeova ashikumutupe lakini arianza kumusaidia. (Ro. 5:3-5) Sasa uriangarie na weye. Ata kama uko na magumu leo, na weye uko nendelea kumutumikia Jeova. Na weye ukuwe sire asema Jeova ashiyakutupa, eko nendelea kukusaidia.

12. Tunezi kurishikia je kama tunashinda kufanya mambo ile turipenda kufanya mu kaji ya Jeova?

12 Kintu kya piri kile kinetupotesheaka furaa ni kushinda kufanya mambo ile turipenda kufanya mu kaji ya Jeova. (Mez. 13:12) Nju tushakumupenda Jeova sana na tunapenda kumupikia merci nju ya mambo yote ile eko natufanshia, njo pale tunapendaka kufanya mambo ya mingi sana mu kaji yake. Lakini, kama tunatafuta kufanya mambo ya mingi sana ile atutaweza nju ya sitwasion ile tukwamo, tunezi kujishikia mubaya sana. (Mez. 17:22) Dada Holly, mwenye ni painia, arisemaka ivi: “Niripendaka kwenda ku masomo ya EER, kwenda kuubiri mu pays ingine, ao kwenda kutumika ku chantier ya Ramapo. Lakini, mambo irishanjé mu maisha yangu, na shikuwezake kufanya byote bile miripendaka. Mirishikiaka mubaya sana. Kama unapenda kufanya mambo lakini unashinda kuifanya, inaumaka sana.” Njo vile batumishi bamingi ba Jeova banajishikiaka kama banashinda kufanya bile baripenda mu kaji ya Jeova.

13. Kama nju ya sitwasion yetu atutaweza kufanya byote bile tunapenda kufanya mu kaji ya Jeova, tunezi kujiwekea ma objektif kani?

13 Ni nini inezi kutusaidia tupate tena furaa? Kumbuka asema Jeova ashitulombake tufanye bile atutaweza. Aina bwingi bwa kaji ile tunamufanshiaka Jeova njo inafanyaka atuone kuwa ba maana ao bashipo maana. Jeova anapenda tukuwe baaminifu kwake na tumutumikie na nguvu ile tuko nayo. (Mik. 6:8; 1 Ko. 4:2) Jeova anaangaikiaka sana bumuntu bwetu bwa ndani kupita ata kaji ile tuko namufanshia. Kama Jeova ye mwenyewe ashitulombake tufanye bile atutaweza, eske ni muzuri twanze kuriangaisha na kufanya bile atutaweza?c Apana! Kama nju ya sitwasion yako autaweza kufanya bya mingi sana mu kaji ya Jeova, pima kufanya bile utaweza. Kwa mufano, unezi kwanza ku former babiyana na kuankurajé banduku na badada bale bashakuzeka. Tena, unezi kutembelea banduku na badada yako, kubaita ku telefone, ao kubatumia ata message nju ya kubaankurajé. Jeova atafurai sana kama unafanya bile unaweza na atakusaidia ukuwe na furaa. Na ushishabu asema, mu mashiku ile iko nakuya, pale tutaingia mu dunia mupya, tutakuwa na ma okazion ya mingi ya kumutumikia Jeova ile atuwazie ata! Dada Holly, ule turitaya ku mwanzo, anasema ivi: “Kama minanza kuwa dekurajé, minakumbukaka asema mu mashiku ile iko nakuya mitaishi milele na mitamutumikia Jeova milele na nguvu yangu yote. Pale njo mitafanyaka byote bile minapenda mu kaji yake.”

14. Ni mambo kani ingine ile inezi kutupoteshea furaa?

14 Kintu kya tatu kile kinezi kutupoteshea furaa ni kuwaza asema makuta na mambo ya kurifuraisha njo inezi kutuletea furaa ya bya kweri. Ku enternete, bantu bamingi banonekanaka sa beko na furaa nju beko naonekana sa vile abakosake ata kintu kimoya. Tunezi kwanza kuwaza asema, kama tunafanya bintu bile tunapendaka, tunauza bile tunapendaka, na tunenda kutembea mafashi ya kwachana-achana njo tutakuwa na furaa ya bya kweri. Aina mubaya kufanya ile mambo yote. Jeova arituumbaka nju tufurahie bintu bya muzuri. Kusema tu bya kweri, bantu bamingi bashakuvumbula asema bintu bile barianza kuwaza asema njo bitabaletea furaa, njo biko nabapoteshea ayo. Eva, dada moya painia, anasema ivi: “Kama mu maisha yako unaangaikiaka paka kujifuraisha, pa kwacha ile maisha binekalaka nguvu.” Kama tunabakia tu na maisha ya kujifuraisha, tutakuwa kuvumbula asema mu ile maisha amuna kintu, lakini iko naongeza tu maumivu.

15. Maisha ya mufalme Salomon inezi kutufundisha nini?

15 Maisha ya mufalme Salomon inezi kutusaidia kuyuwa kule muntu ule anapendaka maisha ya kujifuraisha anaiishiaka. Mu maisha yake, aripenda kufanya kintu kyote kile roo yake iripenda na ariwaza asema, kufanya vile kutamuletea furaa ya bya kweri. Arikurya byakurya bya butamu, arifuraia miziki ya muzuri, na ariuza kintu kyote kile aripenda kuuza ile wakati. Lakini ku mwisho, bile byote abikumuleteake furaa ya bya kweri. Arisemaka ivi: “Rincho arichokake kwangaria na rishikio arichokake kushikia.” (Muh. 1:8; 2:1-11) Bantu bengine banawazaka asema kukuwa na makuta na kufanya kintu kyote kile unapenda njo kutakuletea furaa ya bya kweri. Lakini, ile ni bongo! Iko sa kuwa na faux billet. Inonekanaka tu sa inezi kukusaidia. Lakini kusema tu bya kweri, autauza nayo kintu.

16. Unawaza kusaidia bengine kunezi kufanya tukuwe tena na furaa? Espliké. (Angaria na mafoto.)

16 Ni nini njo inezi kutusaidia tupate tena furaa? Yesu aritufundisha ivi: “Kupachiana kunaletaka furaa sana kupita kupokea.” (Mdo. 20:35) Muze moya ule njina yake ni Alekos arisemaka ivi: “Minajikazaka kufanshia bengine mambo ya kiloko-kiloko. Kama minasaidia bantu, ile inanisaidiaka nishiwaze sana nju ya mambo ile minapenda na kufanya vile kunanileteaka furaa.” Na weye unezi kufanya nini nju ya kusaidia bengine? Kama unaona muntu eko na uzuni, pima kumuankurajé. Pengine autezi kwisha magumu ile eko nayo. Lakini kama unamushikia, unarieka pa fashi yake na unamukumbusha amutupie Jeova maangaiko yake, ile inezi kumupachia nguvu. (Zb. 55:22; 68:19) Tena, unezi kumusaidia akumbuke asema Jeova ashiyamwachiria. (Zb. 37:28; Isa. 59:1) Na tena, unezi kufanya kintu kingine nju ya kumusaidia, sa vile kumutembelea kwake. Unezi kupanga ata kuubiri naye, nju kuubiri kunasaidiaka muntu akuwe na furaa. Acha Jeova akutumikishe nju ya kuankurajé bengine. Kama tunatumikisha wakati yetu nju ya kusaidia bengine, ile itatuletea furaa ya bya kweri!​—Mez. 11:25.

Foto: 1. Dada ashakwikala ye moya mu restora na eko navinya telephone yake. 2. Anashikiya furaa saa anenda kumutembelea dada wa kuzeka na anamupelekea fleur.

Kuriko tu kwangaikia mambo ile uko nayo besoin, saidiako na bengine (Angaria mu paragrafe 16)d


17. Kama tunapenda kuwa na furaa ya bya kweri, tunapashwa kufanya nini? (Zaburi 43:4)

17 Kama tunendelea kuwa karibu na Baba yetu wa ku mbingu Jehova, tutakuwa na furaa ya bya kweri. Bible inatuonesha asema, kwa Jeova, njo ‘kunatoka furaa mingi’ yetu. (Soma Zaburi 43:4.) Njo maana, ata nini itufikie mu maisha, atutongopa. Kama Jeova anabakia rafiki yetu wa karibu sana, tutakuwa na furaa ya bya kweri milele!​—Zb. 144:15.

UTAJIBU JE?

  • Nju ya nini Jeova na Yesu banekalaka paka na furaa?

  • Ni mambo kani njo inezi kutupoteshea furaa?

  • Tunezi kufanya nini nju tupate tena furaa kama turiipotesha?

MWIMBO 155 Furaha Yetu ya Milele Inatoka kwa Yehova

a Angaria ankadré “Mambo ile tunezi kufanya nju Jeova atupachie furaa.”

b Angaria mufano ya Dennis Christensen na bibi yake Irina mu Ripoti ya 5 ya 2023 ya Baraza Yenye Kuongoza ile iko ku jw.org.

c Nju ya kuyuwa bya mingi, soma abari: “Uwe na Matarajio Yenye Usawaziko, na Uwe Mwenye Shangwe” ya mu Munara ya Mulinzi ya 15 juillet 2008.

d ESPLIKASION YA FOTO: Dada moya anauza bintu bya mingi lakini ashina na furaa. Anapata furaa saa anamujia fleur mamabo moya ivi wa kukomea ule eko na lazima ya ankurajema.

    Swahili (Katanga) Publications (2020-2026)
    Toka
    Ingia
    • Swahili (Katanga)
    • Partajé
    • Preferanse
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni ya kutumikisha
    • Règles de confidentialité
    • Paramètres de confidentialité
    • JW.ORG
    • Ingia
    Partajé