BIBLIOTEKE YA KU ENTERNETE Watchtower
Watchtower
BIBLIOTEKE YA KU ENTERNETE
Swahili (Katanga)
  • BIBLE
  • BITABU
  • MA RENION
  • w25 Octobre pp. 18-23
  • Ni nini inezi kutusaidia kumufunguria Jeova roo yetu

Akuna video nju ya iyi selection.

Pardon, kurikuwa erreur mu chargement ya video.

  • Ni nini inezi kutusaidia kumufunguria Jeova roo yetu
  • Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
  • Sous-titres
  • Ya kufanana na iyi
  • USHONGOPE KUSALI KWA JEOVA
  • NI NINI ITATUSAIDIA KUMUFUNGURIA JEOVA ROO YETU
  • WAZA SANA NJU YA MA SALA YA KUTOKA KU ROO YA BATUMISHI BA MUNGU ILE IKO MU BIBLE
  • ENDELEA KUWA KARIBU NA JEOVA
  • Kumbuka kusali nju ya bengine
    Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
w25 Octobre pp. 18-23

ABARI YA KUFUNDA YA 42

MWIMBO 44 Sala ya Mutu wa Hali ya Chini

Ni nini inezi kutusaidia kumufunguria Jeova roo yetu

“ Minakwita na roo yangu yote. Jeova wangu, unijibuko.”​—ZB. 119:145.

MU KIFUPI

Ma sala ya batumishi ba nzamani ba Jeova ile iko mu Bible inezi kutusaidia tufanye ma sala yetu ikuwe ya muzuri sana.

1-2. (a) Ni nini inezi kutufanya tushimufungurie Jeova roo yetu? (b) Tunayuwa je asema Jeova anashikiaka ma sala yetu?

ESKE saa moya unonaka asema unamwambiaka Jeova paka bintu bimoya-bimoya na aumufunguriake roo yako? Bya vile binatufikiaka shiye bote. Nju tuko na bya mingi bya kufanya, saa moya inatufikiaka tu kusali bya yulu-yulu na tunakosa kumwambia Jeova byote bile tuko nabyo ku roo. Saa ingine atumufunguriake Jeova roo yetu, nju tunonaka asema atustaili kushimama kumbele yake na kusumburia naye.

2 Bible inatufundisha asema kintu kya lazima aina kupanga sala yetu muzuri, lakini ni kumufunguria Jeova roo yetu yote. Anashikiaka “maombi ya bapole.” (Zb. 10:17) Nju anatuangaikiaka, anashikiaka byote bile tunekalaka tuko namonesha.​—Zb. 139:1-3.

3. Mu iyi abari tutajibu ku maulizo kani?

3 Sasa tunezi kujiuliza ivi: Nju ya nini atupashwe kuongopa kumwambia Jeova bile biko ku roo yetu? Ni nini inezi kutusaidia kumufunguria Jeova roo yetu? Ma sala ya batumishi ba Jeova ile iko mu Bible, inezi kutusaidia je twanze kumufunguria Jeova roo yetu? Kama tuko na mangaiko sana na atuyuwe ata kile tunezi kumwambia Jeova, nini inezi kutusaidia? Acha tupate majibu ku iyi maulizo.

USHONGOPE KUSALI KWA JEOVA

4. Nini itatusaidia tushongope kusali kwa Jeova? (Zaburi 119:145)

4 Kama tunayuwa asema Jeova ni rafiki muzuri ule anatutakia bizuri, atutongopa kumwambia mawazo yetu na vile tuko najishikia. Njo vile ule arianjikaka Zaburi 119 arianzaka kumuona Jeova, na njo pale arianzaka kumwambia vile arianza kujishikia. Arikuwaka na magumu ya mingi mu maisha. Bantu barimulandiaka mambo ya bongo. (Zb. 119:23, 69, 78) Na saa ingine arianzaka kujishikia mubaya nju ya mankosa yake. (Zb. 119:5) Ata vile, ashikwanzake kuongopa kumufunguria Jeova roo yake.​—Soma Zaburi 119:145.

5. Nju ya nini atupashwe kushikia boka kusali kwa Jeova? Leta mufano.

5 Jeova anapenda ata bale bashakumukosea sana basali kwake. (Isa. 55:6, 7) Njo pale atupashwe kwacha ata kintu kimoya kitushindishe kusali. Tubebe mufano: Muntu ule eko nafunda kushona manguo anajua asema anezi kusumburia na mwarimu yake nju ashone muzuri, sasa atafanya je kama anashona nguo mubaya? Ata kama atashikia aya atauliza mwarimu yake nju amusaidie! Njo pamoya na shiye, ata kama tushakumukosea Mungu ao turifanya nzambi, tushongope kusali kwake.​—Zb. 119:25, 176.

NI NINI ITATUSAIDIA KUMUFUNGURIA JEOVA ROO YETU

6-7. Ni nini njo itatusaidia tumufungurie Jeova roo yetu? Leta mufano. (Angaria na esplikasion ingine.)

6 Tutakuwa karibu sana na Jeova, kama tunamwambia mawazo yetu na vile tuko najishikia. Sasa, ni nini njo itatusaidia kufanya vile?

7 Waza nju ya masifa ya Jeova.a Kama tunawaza sana nju ya masifa ya muzuri ya Jeova, bitakuwa teketeke kwetu kumwambia mawazo yetu na vile tuko najishikia. (Zb. 145:8, 9, 18) Tuone mufano ya Kristine. Baba yake arikuwaka makari sana. Kristine anasema ivi: “Vile baba yangu arikuwaka makari sana, birikuwaka nguvu kwangu kumuona Jeova sa vile baba yangu ule ananipenda na kusali kwake. Mirianzaka kuwaza asema vile mishikamilike nikifanye tu nzambi Jeova ataniacha.” Ni sifa kani ya Jeova ile irimusaidiaka? Anasema tena ivi: “Kukumbuka asema Jeova eko na mapendo ya bya kweri kurinisaidia nikuwe sire asema ashitaniachaka na atendelea tu kunipenda. Miriyuwa asema ata kama minanguka atanilamusha. Kukumbuka vile kunanisaidiaka nimuoneshe byote bile biko ku roo yangu ikuwe niko mu furaa ao mu magumu.”

8-9. Kuwaza nju ya mambo ile tutamwambia Jeova mbele ya kusali kunezi kutusaidia je? Leta mufano.

8 Waza bile utasema. Mbele ya kusali, inalomba kwanza kujiulizako maulizo sa vile: ‘Ni mambo kani njo iko naniangaisha apa? Kuko muntu ule arinikosea ule minapashwa kurumia? Ni nini ayendeke tena mu maisha yangu ile Jeova anezi kunisaidia?’ (2 Fal. 19:15-19) Tunezi tena kufwata mufano ya Yesu ile aritwachiaka nju ya namna ya kusali, kwa mufano kusali nju ya njina ya Jeova, Ufalme yake na mapenzi yake.​—Mt. 6:9, 10.

9 Bwana yake ya dada Aliska arikuwaka na malari ya kanser ya servo ile irikuwaka karibu kumuuwa. Shiku ile dada Aliska ariyuwaka vile arishindaka ata na kusali. Anasema ivi: “Kichwa kirinijungulukaka sana, mirishindaka ata bile minezi kumwambia Jeova mu sala.” Nini njo irimusaidia? Ye moya anasema ivi: “Mbele ya kusali mirianzaka kuwaza sana nju ya bile ntamwambia Jeova, ile irifanyaka nishanze kumwambia paka tu nju ya mambo yangu ao nju ya malari ya bwana yangu. Ile irinisaidiaka nitulizane na nimwambie Jeova mambo ya kwachana-achana.”

10. Nju ya nini tunapashwa kufanya nguvu nju tushanze kusali bya yulu-yulu? (Angaria na mafoto.)

10 Apana tu kusali bya yulu-yulu. Ata ma sala ya mufupi inezi kufanya tukuwe karibu na Jeova. Lakini nju ya kumwambia Jeova mambo ya mingi na vile tukonajishikia tunapashwa kubeba wakati ya mingi nju ya kusali.b Elijah, bwana yake ya dada Aliska, anasema ivi: “Minafanyaka nguvu nju nianze kusali mala ya mingi pa shiku, na kama minafanya sala ya mulefu minajishikiaka sa niko karibu sana na Jeova. Jeova ashitukachiake ma minite ya kusali kwake, njo pale minabebaka wakati yote ile minapenda nju ya kumwambia mambo yote ile niko nayo ku roo.” Pima kufanya ivi: Tafuta saa ya muzuri na fashi ya kimya pale unezi kutosha sauti nju ya kusali na pale abatakuderanjé. Na ufanye nguvu nju wanze kufanya vile kila shiku.

Foto: 1. Mbele jua itoke, nduku moya ashakwikala kumbele ya meza. Eko na nkopo ya kafé, pa meza peko Bible ya waji na eko nawaza sana. 2. Kisha jua kutoka, anabakia ashakwikala paka pale na anasali wakati mulefu.

Tafuta saa ya muzuri na fashi ya kimya pale unezi kusumburia na Baba yako wa ku mbingu pashipo muntu wa kukuderanjé (Angaria paragrafe 10)


WAZA SANA NJU YA MA SALA YA KUTOKA KU ROO YA BATUMISHI BA MUNGU ILE IKO MU BIBLE

11. Ma sala ya kutoka ku roo ya batumishi ba Mungu ile iko mu Bible inezi kukusaidia je? (Angaria na ankadré “Uko najishikia sa vile barijishikiaka?”)

11 Ma sala ya kutoka ku roo na mimbo ao ma zaburi ya batumishi ba nzamani ba Jeova ile iko mu Bible, inezi kukusaidia. Kama unasoma vile batumishi ba nzamani ba Jeova barianzaka kumufunguria ma roo yabo, ile inezi kukusukuma na weye umufungurie Jeova roo yako. Ma sala yabo inezi kukusaidia uvumbule misemo ile na weye unezi kuweka mu sala yako. Na unezi kupata ma sala ile inapatana na sitwasion yako.

Uko najishikia sa vile barijishikiaka?

Barimufunguriaka Jeova ma roo yabo mu ma sitwasion ya kwachana-achana. Na weye ushakujishikiaka vile barijishikia?

  • Saa Yakobo arikuwa mu mangaiko ya nguvu, ashikumwambiake Jeova nju paka ya mangaiko yake, lakini arimupikiaka tena Jeova merci nju ya bizuri bile arianzaka kumufanshia.​—Mwa. 32:9-12.

  • Saa barimweka Salomon kuwa mufalme arijiona sa eko mutoto sana na ashitaweza ile kaji, njo maana arimulomba Jehova amusaidie.​—1 Fa. 3:7-9.

  • Kisha David kufanya busharati na Bath-sheba, arimuriria Jeova ‘amusafishe roo.’​—Zb. 51:9-12.

  • Ile saa Jeova arimupachia Maria kaji ya sasa ya kufanya, Maria arimutukuza Jeova.​—Lu. 1:46-49.

Mambo ile unezi kufunda: Funda ma sala ya batumushi ba Jeova ile iko mu Bible, na angaria vile Jeova arijibu ku ile ma sala na tumikisha mu sitwasion yako bile unafunda.

12. Tunezi kujiuliza maulizo kani saa tuko nasoma ma sala ile iko mu Bible?

12 Saa uko nasoma ma sala ile iko mu Bible, ujiulize ivi: ‘Nani njo arisali ivi na arikuwa mu sitwasion kani? Nju ya nini arisali ivi? Na miye minezi kusali ivi? Iyi sala inanifundisha nini?’ Pengine itakulomba ufanye ma reshershe ingine nju ya kupata majibu ku iyi maulizo, lakini kufanya vile kutakusaidia sana. Tuone mifano kiloko.

13. Sala ile Hana arifanyaka inezi kutufundisha nini? (1 Samweli 1:10, 11) (Angaria na foto ya pa kuvertire.)

13 Soma 1 Samweli 1:10, 11. Saa Hana arisemaka misemo ya mu iyi sala, arikuwaka na mambo mbiri ya munene ile irianzaka kumwangaisha. Mbele ashikwanzake kuzala, na tena mbanda yake arianzaka kumuteswa sana. (1 Sa. 1:4-7) Na weye kama uko na mambo ile iko nendelea kukwangaisha, sala ile Hana arifanyaka inezi kukufundisha nini? Hana arifanya sala ya mulefu. Mu ile sala arimutupia Jeova bujito bote bule arikuwa nabo ku roo na ile irimupachia nguvu. (1 Sa. 1:12, 18) Na shiye kama “tunamutupia Jeova bujito bote” bule tuko nabo ku roo, ni kusema kumwambia waji-waji magumu yetu na vile tuko najishikia, tutapata nguvu.​—Zb. 55:22.

Foto: 1. Hana eko nangaria ku mpembeni na eko naria saa Elkana eko nacheza na batoto yake bawiri. 2. Penina eko nacheka saa eko namubembelesha bebe wake. 3. Hana eko naria saa eko nasali sana. 4. Pretre mukubwa Eli ashakwikala na ashakukunja mikono na eko namwangaria Hana na mancho ya makari.

Hana ashikwanzake kuzala na mbanda yake arianzaka kumwangaisha sana, lakini arimutupia Jeova bujito bote bule arikuwa nabo ku roo (Angaria paragrafe 13)


14. (a) Mufano ya Hana inezi kutufundisha tena nini? (b) Kusoma na kuwaza sana nju ya Bible kunezi kutusaidia je tupate mambo ya mingi ya kumwambia Jeova? (Angaria na esplikasion ingine.)

14 Miaka kiloko kisha Hana kumuzala Samweli, arimupeleka kwa pretre mukubwa Eli. (1 Sa. 1:24-28) Hana arifanya sala ya kutoka ku roo. Mu ile sala arimupikia Jeova merci nju arijioneya asema Jeova anachungaka na kwangaikia batumishi bake baminifu.c (1 Sa. 2:1, 8, 9) Pengine magumu yote ya mu nyumba ya Hana aikwishake, lakini ariendelea kuwaza nju ya vile Jeova arikuwa ashakumubariki. Ile inatufundisha nini? Kama na shiye tuko na magumu ile iko nendelea, tunezi kuivumiria kama tunakumbuka vile Jeova eko natusaidia kuanzia nzamani tii paka na leo.

15. Kama tunaona mambo ya mubaya na ile mambo inanza kutwangaisha, mufano ya Yeremia inezi kutusaidia je? (Yeremia 12:1)

15 Soma Yeremia 12:1. Yeremia arikuwaka dekurajé sana, saa arianzaka kuona bantu bale beko nafanya bintu bibaya beko na maisha ya muzuri. Na tena arishikiaka mubaya sana saa bantu bengine ba mu Israel barianza kumucheka. (Yer. 20:7, 8) Na shiye tunezi kujishikia sa yeye, saa tunaona bantu babaya beko na furaa mu maisha ao kama bantu bengine beko natucheka. Yeremia arijishikiaka mubaya sana. Arimwambiaka Jeova ile mambo yote, lakini ashikusemake asema nkosa ni ya Jeova. Saa ariona vile Jeova aritendea bale abakukuwe baminifu, ile irimusaidia endelee kutumainia asema Jeova anafanyaka paka mambo ya kunyoloka. (Yer. 32:19) Na shiye kama kuko mambo ile iko natwangaisha, tumwambieyo Jeova na twendelee kuwa sire asema atatengeneza mambo mu wakati ile ashakupanga.

16. Kama atuna na namna ya kumwabudu Jeova pamoya na bengine, mufano ya mulawi inezi kutufundisha nini? (Zaburi 42:1-4) (Angaria na mafoto.)

16 Soma Zaburi 42:1-4. Ni mulawi moya ule ashikukuwake na namna ya kumwabudu Jeova ku tample pamoya na benzake njo arianjikaka iyi mwimbo. Iyi Zaburi inaonesha vile arianzaka kujishikia. Kama na shiye atuna na namna ya kutoka ku nyumba nju tuko malari ao bashakutufunga mu prizon nju ya imani yetu, pengine na shiye tunezi kujishikia sa ule mulawi. Saa moya tunezi kujishikia muzuri na saa ingine tunezi kujishikia mubaya. Lakini itakuwa muzuri kama tunamufunguria Jeova roo yetu mu sala. Ile itatusaidia tukomprandre muzuri vile tuko najishikia, na tuoneko mambo ingine ile iko nendeka mu sitwasion yetu. Kwa mufano, ule mulawi arifikiaka kuvumbula asema atapataka tena okazion ya kumwabudu Jeova pamoya na bengine. (Zb. 42:5) Tena arikumbuka vile Jeova arianza kumusaidia. (Zb. 42:8) Kumufunguria Jeova roo yetu mu sala kutatusaidia na shiye tuyuwe muzuri vile tuko najishikia, tutulizane mu akiri, na tupate nguvu ya kwendelea kuvumiria.

Foto: 1. Mulawi moya eko nasali sana saa eko mu dezere. 2. Nduku ashakwikala mu kitanda kya opitalo, eko nasali na eko na Bible ya waji pa mikulu.

Mulawi ule arianjikaka Zaburi 42 arimufunguriaka Jeova roo yake. Na shiye kama tunamwambia Jeova vile tuko najishikia, tunezi kuona vile eko natusaidia (Angaria paragrafe 16)


17. (a) Sala ya Yona inatufundisha nini? (Yon. 2:1, 2) (b) Kama tuko mu magumu, nju ya nini ni muzuri kukumbuka misemo ya kwachana-achana ile iko mu Zaburi? (Angaria esplikasion ingine.)

17 Soma Yona 2:1, 2. Ile saa profete Yona arifanyaka iyi sala arikuwaka mu ntumbo ya kinsamaki kinene. Ata kama arikuwaka ashakumukosea Jeova, Yona arikuwaka sire asema Jeova atashikia sala yake. Mu ile sala, Yona aritumikishaka misemo ya mingi ile tunakuta mu Zaburi.d Ile inaonesha asema arikuwaka ashakuyuwa ile ma Zaburi muzuri sana. Kuikumbuka na kuwaza sana nju yayo, kurimusaidia akuwe sire asema Jeova atamusaidia. Na shiye kama tunabamba ma versé mu kichwa, saa tuko nasali mu wakati ya magumu tutaikumbuka na itatusaidia tutulizane.

ENDELEA KUWA KARIBU NA JEOVA

18-19. Waroma 8:26, 27 inatufanya tukuwe sire na nkintu kani? Leta mufano.

18 Soma Waroma 8:26, 27. Saa moya magumu inezi kutupitia na tunashinda ata bya kumwambia Jeova mu sala. Ata mu ile sitwasion, solision ikwako. Mu wakati ya vile roo takatifu inekalaka iko ‘natuombea.’ Inafanyaka vile je? Jeova aritumikishaka roo yake takatifu nju ya kusukuma batumishi bake banjike ma sala ya mingi mu Bible. Kama tunashinda kusali, Jeova anezi kubeba misemo ya kwachana-achana ya ma sala ile iko mu Bible, ile inapatana na sitwasion yetu na kufanya saa vile shiye njo tuko namulombayo, na kisha anatujibu.

19 Kuyuwa vile njo kurisaidiaka dada Yelena wa mu Russie. Barimubambaka nju arianzaka kusali na kusoma Bible. Ariangaikaka sana mu akiri na arishindaka ata kusali. Anasema ivi: “Kisha mirianzaka kukumbuka asema saa niko na mangaiko, na mishiyuwe ata bile minezi kumwambia, Jeova atabeba ma sala ya batumishi bake ba nzamani ile iko mu Bible na ateifanya sa vile ni miye njo niko naomba na ataijibu. . . . Ile irianzaka kunipachia nguvu mu ile wakati ya nguvu sana.”

20. Saa tuko na magumu namna kani tunezi kujitayarisha nju ya kusali?

20 Kama tuko mu magumu tunezi kujitayarisha je mbele ya kusali? Saa tuko na mangaiko inezi kuwa nguvu kwetu kujinkosantré, nju tunezi kuwa tuko nawaza mambo ingine. Sasa, tunezi kufanya nini nju ya kujitayarisha mu akiri mbele ya kusali? Tunezi kushikia audio ya kitabu kya Zaburi. Tunezi ata kwanjika pa papier vile tuko najishikia sa vile mufalme David arifanyaka. (Zb. 18, 34, 142; misemo ya ku mwanzo.) Akuna sheria ile tunezi kuweka nju ya namna ya kujitayarisha mbele ya kusali, weye fanya tu kile kitakusaidia.

21. Nju ya nini atupashwe kuongopa kumufunguria Jeova roo yetu?

21 Kujua asema Jehova anatukomprandraka ata kama atuyasema kintu, kunatufanyaka muzuri sana, kunatupachiaka nguvu. (Zb. 139:4) Ata vile, Jeova anapendaka tumwambie vile tukonajishikia na tuoneshe asema tunamutumainia. Njo pale, ushongope ata kiloko kusali kwa Baba yako wa ku mbingu. Soma ma sala ya batumishi ba Jeova ba nzamani ile iko mu Bible, umufungurie Jeova roo yako yote. Umwambie furaa yako na magumu yako. Sa vile rafiki wa muzuri anekalaka, Jeova ashitakwachaka ata shiku moya!

UTAJIBU JE?

  • Ni nini itakusaidia umufungurie Jeova roo yako saa uko nasali?

  • Ni mambo kani ile unezi kufanya nju umufungurie Jehova roo yako mu sala?

  • Kusoma na kuwaza sana nju ya ma sala ile iko mu Bible kunezi kukusaidia je?

MWIMBO 45 Mawazo ya Moyo Wangu

a Angaria mu kitabu Maandiko ya Kutusaidia mu Maisha ya Kikristo chini ya titre “Sifa fulani za muzuri za Yehova” pa titre kiloko “Yehova.”

b Ma sala ile tunafanyaka kumbele ya kutaniko inapashwa kuwa ya mufupi.

c Pale arianzaka kusali, Hana aritumikishaka misemo ya kufanana na ile iko mu bitabu bile Musa arianjikaka. Ile inaonesha asema arianzaka kuwaza sana nju mandiko. (Kum. 4:35; 8:18; 32:4, 39; 1 Sa. 2:2, 6, 7) Kisha miaka ya mingi Maria mama yake ya Yesu naye aritumikisha misemo ya kufanana na ile Hana arisemaka nju ya kumusifu Jeova.​—Lu. 1:46-55.

d Nju ya kuona mifano fulani, komparé Yona 2:3-9 na Zaburi 69:1; 16:10; 30:3; 142:2, 3; 143:4, 5; 18:6; na 3:8, nju uone vile Yona aripangaka sala yake.

    Swahili (Katanga) Publications (2020-2026)
    Toka
    Ingia
    • Swahili (Katanga)
    • Partajé
    • Preferanse
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni ya kutumikisha
    • Règles de confidentialité
    • Paramètres de confidentialité
    • JW.ORG
    • Ingia
    Partajé