BIBLIOTEKE YA KU ENTERNETE Watchtower
Watchtower
BIBLIOTEKE YA KU ENTERNETE
Swahili (Katanga)
  • BIBLE
  • BITABU
  • MA RENION
  • w25 Novembre pp. 10-15
  • Endelea kuwa na furaa saa uko nachunga muntu wa malari ao wa kuzeka

Akuna video nju ya iyi selection.

Pardon, kurikuwa erreur mu chargement ya video.

  • Endelea kuwa na furaa saa uko nachunga muntu wa malari ao wa kuzeka
  • Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
  • Sous-titres
  • Ya kufanana na iyi
  • KWANGAIKIA MUNTU KUNEZI KUKUPOTESHEA FURAA
  • MAMBO YA KUFANYA NJU WENDELEE KUWA NA FURAA
  • NAMNA BENGINE BANEZI KUSAIDIA
  • Endelea kuwa na furaa ata kama unazeka
    Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
  • Jeova anezi kutusaidia tukuwe na “furaa ya bya kweri”
    Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
w25 Novembre pp. 10-15

ABARI YA KUFUNDA YA 45

MWIMBO 111 Mambo Yenye Kufanya Tukuwe na Furaha

Endelea kuwa na furaa saa uko nachunga muntu wa malari ao wa kuzeka

“Bale beko napanda mbeko na machozi batavuna na bikelekele bya furaa.”​—ZB. 126:5.

MU KIFUPI

Iyi abari inatwambia mambo ya kufanya nju twendelee kuwa na furaa saa tuko nachunga muntu wa kuzeka ao wa malari.

1-2. Jeova anaonaka je ule eko nangaikia muntu wa kuzeka ao wa malari? (Mezali 19:17) (Angaria na mafoto.)

NDUKU Jin-yeol wa mu Corée anasema ivi: “Miye na bibi yangu tushakufanya miaka 32 na bya yulu tangu tuoane. Lakini mu miaka iyi inapita, bibi yangu analukula sana na eko na lazima nimusaidie. Eko na malari ya nguvu ile inafanya ikuwe nguvu kwake kutenka. Minamupendaka sana na minapendaka kumwangaikia. Bushiku bote, anapashwa kulala pa kitanda kimoya ivi kile tusha kweka mu nyumba yetu. Minalalaka ku mpembeni yake na tunabambanaka ku mikono saa tunalala.”

2 Eske uko nachunga muntu ule unapendaka? Pengine ni muzazi yako, bwana ao bibi yako, mutoto yako ao rafiki yako. Kama ni vile, unafuraiaka sana kumusaidia nju unamupendaka. Na nju uko nangaikia ule muntu, unaonesha asema unamupenda Jeova. (1 Ti. 5:4, 8; Yak. 1:27) Ata vile, kuko magumu ile unapataka ile bantu bengine abaonake. Saa moya unezi kuona sa bengine abaone mateso yako. Unezi kuonekana na furaa saa uko pa bantu, lakini saa uko pa we moya unashikia uzuni na unanza ata kuria. (Zb. 6:6) Ata kama bengine abaone magumu ile uko nayo, Jeova yeye anaona. (Komparé na Kutoka 3:7.) Anaonaka byote bile unafanyaka nju ya kusaidia muntu ule uko nachunga ata kama uko na uzuni na machozi. (Zb. 56:8; 126:5) Jeova anaonaka kila kintu, na ye moya anaonaka asema eko na ndeni yako nju ya bile uko nafanya, na analaka asema atakuripa.​—Soma Mezali 19:17.

Mafoto: Bale banachungaka muntu mwingine beko mu masitwasion ya kwachana-achana. 1. Dada eko namukunyisha mama yake wa kuzeka ule ashitokake mu kitanda. 2. Dada eko namuvwarisha bwana yake bilato. Bwana yake eko mu kankinga ka ba bilema. 3. Mama moya eko navwarisha mutoto yake casque mbele acheze kabumbu na baba yake. 4. Nduku moya anatembelea nduku wa kuzeka na anasali pamoya naye.

Banduku na badada ba mingi banachungaka muntu wa malari ao wa kuzeka (Angaria mu paragrafe 2)


3. Pengine Abraham na Sara baripata magumu kani saa barianza kumwangaikia Téra?

3 Mu Bible muko maabari ya banaume na banamuke ba mingi bale nabo barichungaka muntu wa kuzeka ao wa malari. Tubebe mufano ya Abraham na Sara. Saa baritoka Our nju ya kwenda Harân, baba yabo Téra arienda pamoya nabo. Téra arikuwa na miaka karibu 200 na barifanya safari ya karibu 960 kilometre. (Mwa. 11:31, 32) Ni kweri, Abraham na Sara barimupenda Téra. Lakini, wazia namna biripashwa kuwa nguvu kwabo kumwangaikia mu ile safari yote. Mu ile safari baripashwa kupanda pa ba chameau ao pa bampunda, na ile iripashwa kuwa nguvu sana kwa Téra nju arikuwa ashakukomea. Kumwangaikia Téra kuripashwa kuchokesha sana Abraham na Sara. Lakini ata kama mambo irikuwa je, Jeova aribapachia nguvu ile barikuwa nayo lazima. Sa vile tu Jeova arisaidia Abraham na Sara, atakusaidia na weye na kukupachia nguvu ile uko nayo lazima.​—Zb. 55:22.

4. Tutafunda nini mu iyi abari?

4 Kama uko na furaa itakuwa teketeke kwako kwendelea kwangaikia muntu. (Mez. 15:13) Kumbuka asema unezi kwendelea kuwa na furaa ata kama mambo iko nguvu. (Yak. 1:2, 3) Unezi kufanya nini nju wendelee kuwa na furaa? Kintu kile kitakusaidia ni kumutumainia Jeova na kusali kwake, kumulomba akusaidie kwendelea kuwa na mawazo ya muzuri. Mu iyi abari tutaona mambo ingine ile bale beko nangaikia muntu wa kuzeka ao wa malari banezi kufanya nju baendelee kuwa na furaa. Tena, tutaona namna bengine banezi kubasaidia. Mbele ya yote, tuone nju ya nini ni muzuri kwa bale beko nachunga muntu wa kuzeka ao wa malari kuwa na furaa na ni magumu kani inezi kubapoteshea furaa yabo.

KWANGAIKIA MUNTU KUNEZI KUKUPOTESHEA FURAA

5. Nju ya nini muntu ule eko nachunga muntu mwingine anapashwa kwendelea kuwa na furaa?

5 Kama ule eko nachunga muntu wa kuzeka ao wa malari anapotesha furaa, anezi kuchoka sana. (Mez. 24:10) Na saa ashakuchoka, itakuwa nguvu kwake kwangaikia muzuri muntu ule eko nachunga. Sasa ni magumu kani inezi kukupoteshea furaa kama uko nachunga muntu mwingine?

6. Nju ya nini bale banachungaka muntu mwingine banezi kujishikia sa banachoka sana?

6 Unezi kuchoka sana. Dada Leah anasema ivi: “Ata saa mambo iko muzuri, minekalaka na mangaiko sana, na mangaribi minarishikiaka wa kuchoka sana. Saa moya minashindaka ata nguvu ya kujibu ku message.” Kwa bengine, saa beko nangaikia muntu mwingine, inekalaka nguvu kwabo kulala saa ya kwenea ao kupata ata wakati ya kupumujika. Dada Inés anasema ivi: “Inekalaka nguvu kwangu kulala saa ya kwenea. Bushiku minapashwa kulamuka kisha kila saa mbiri nju ya kwangaria mama yangu muko, ule niko nachunga. Na kushakupita miaka mingi miye na bwana yangu tushakushinda ata kwenda fashi ile tunapenda nju ya kujifuraisha.” Bengine banakatalaka ma invitation ingine ao makaji ingine mu organizasion nju bakuyepo saa yote nju ya kuchunga banduku yabo. Bale banachungaka muntu mwingine, banezi kujishikia mubaya nju abawezi kufanya byote bile banapenda.

7. Nju ya nini saa moya bale banachungaka muntu wa kuzeka ao wa malari banashikiaka uzuni?

7 Unezi kujishikia mubaya nju kuko bile autaweza kufanya ao nju ya bile biko namufikia mwenye uko nachunga. Dada Jessica anasema ivi: “Mala mingi minawazaka asema minapashwa kufanya bya mingi nju ya kusaidia muntu ule niko nachunga. Na saa moya kama minabeba ka saa ka kupumujika, minarishikiaka sa niko nariangaikia tu mi moya.” Bengine banajishikia mubaya nju saa moya banawazaka asema maisha ya vile inabachokesha. Bengine banawazaka asema abafanye bya mingi nju ya kusaidia muntu ule beko nachunga. Bengine banajishikiaka mubaya nju saa moya nju ya makari barisema mubaya ule muntu beko nachunga. (Yak. 3:2) Bengine nabo, banashikiaka mubaya sana kuona vile sitwasion ya ule beko nachunga iko naendelea kwalabika. Dada Barbara anasema ivi: “Kintu kimoya kya nguvu sana kwangu ni kuona vile sitwasion ya muntu ule minapenda iko naendelea kwalabika kila shiku.”

8. Espliké namna kusema merci kunezi kusaidia ule anachungaka muntu ule ashakuzeka ao wa malari.

8 Unezi kuona asema kaji ile uko nafanya ni ya bule. Nju ya nini? Nju bantu ba mingi abakupikiake merci nju ya kaji ile unafanyaka. Misemo tu ya kiloko ya kusema merci inezi kusaidia sana. (1 Te. 5:18) Dada Melissa anasema ivi: “Saa moya minariaka nju minachoka, lakini saa bale niko nangaikia bananiambia: ‘Merci nju ya byote bile uko natufanshia,’ minashikiaka furaa sana. Ile misemo inanisaidiaka nipate tena nguvu ya kulamuka tena kesho nju ya kubangaikia.” Nduku Ahmadu anaonesha vile anajishikiaka saa banamupikia merci. Yeye na bibi yake banangaikiaka mwipwa yabo moya ule eko na malari ya kifwafwa. Anasema ivi: “Ata kama ashiyuwe bile byote tunafanyaka nju ya kumwangaikia, minashikiaka furaa sana saa anatupikia merci ao saa anatwanjikia iyi misemo ‘minamipenda.’”

MAMBO YA KUFANYA NJU WENDELEE KUWA NA FURAA

9. Namna kani ule eko nachunga muntu wa malari ao wa kuzeka anezi kuonesha asema anayuwa kama ashitaweza kufanya byote?

9 Yuwa asema autaweza kufanya byote. (Mez. 11:2) Shiye bote atupatake wakati na nguvu ya kufanya byote bile tunapenda. Njo maana tunapashwa kujiwekea mipaka nju ya mambo ile tunaweza kufanya na ile atutaweza kufanya, na saa moya ni muzuri kusema shitaweza. Ni muzuri kufanya vile, nju inaonesha kama unayuwa asema autaweza kufanya byote. Kama bengine banapenda kukusaidia, ichika bakusaidie. Nduku Jay anasema ivi: “Kila shiku tunezi kufanya tu mambo ile inapatana na wakati na nguvu ile tuko nayo. Kuyuwa asema autaweza kufanya mambo yote kutakusaidia wendelee kuwa na furaa.”

10. Saa uko nangaikia muntu, unapashwa kutafuta kujua nini? (Mezali 19:11)

10 Tafuta kuyuwa ni nini inamusukuma ule muntu kufanya bile eko nafanya. (Soma Mezali 19:11.) Kama unafanya vile, utabakia wa kutulizana saa muntu ule uko nachunga anafanya ao anasema bile aufuraie. Nju utakomprandre kile kiko namusukuma kufanya vile. Kuko malari ingine ile inezi kusukuma muntu afanye bintu bile ashikwanzake kufanya. (Muh. 7:7) Kwa mufano, muntu ule murianzaka kusumburia naye bien, anezi kwanza kubishana-bishana na weye ao anezi kuwa wa kujiriria-riria ao wa kushirika-shirika. Kama uko nachunga muntu ule eko na malari ya nguvu, inezi kuwa muzuri ufanye ma recherche nju ya kukomprandre ile malari. Nju kama unakomprandre muzuri malari yake utayuwa asema ni malari njo iko namusukuma kufanya bile eko nafanya, aina asema eko nafanshiamo.​—Mez. 14:29.

11. Bale beko nachunga bantu ba kuzeka ao ba malari banapashwa kujiwekea kila shiku saa ya kufanya mambo kani ya lazima? (Zaburi 132:4, 5)

11 Ujiwekee wakati ya kufanya burafiki bwako pamoya na Jeova bukuwe nguvu. Saa moya, ni muzuri kwacha kufanya mambo ingine na kufanya mambo ile iko “ya lazima sana.” (Flp. 1:10) Mu ile mambo ya lazima sana, muko kufanya burafiki bwako na Jeova bukuwe nguvu. Mufalme David arikuwa na mambo mingi sana ya kufanya, lakini kumwabudu Jeova njo irikuwa kintu kya maana sana mu maisha yake. (Soma Zaburi 132:4, 5.) Na kwa ule eko nachunga muntu wa kuzeka ao wa malari, ni kintu kya lazima sana kujiwekea kila shiku saa ya kusoma Bible na kusali. Dada Elisha anasema ivi: “Kusali na kuwaza sana nju ya mambo ile iko mu Zaburi, kunanisaidiaka niendelee kuwa na furaa. Kusali njo kunanisaidiaka sana. Saa yote minamulombaka Jeova anisaidie nitulizane.”

12. Nju ya nini ni muzuri kujiwekea saa ya kwangaikia santé yako?

12 Ujiwekee wakati ya kwangaikia santé yako. Bantu bale beko na mambo mingi ya kufanya sa vile bale beko nangaikia muntu wa kuzeka ao wa malari, banekalaka na wakati kiloko nju ya kutafuta na kwipika byakurya bile bitabasaidia ku santé yabo. Kurya byakurya bya muzuri na kufanya sport, kutakusaidia ukuwe na santé ya muzuri na ujishikie muzuri mu maungu na mu akiri. Njo maana, tumikisha muzuri wakati kiloko ile uko nayo nju ya kuzobelea kurya muzuri na kufanya sport. (Efe. 5:15, 16) Kintu kingine ni kulala saa ya kwenea. Bale banafundaka mambo ya kichwa banasema kama kulala kunatengenezaka cerveau. (Muh. 4:6) Kitabu kimoya kinasema kama muntu ule analalaka saa ya kwenea ashitakuwa na mangaiko ya mingi na anezi kubakia wa kutulizana saa anajikuta mu sitwasion ya nguvu. Ni muzuri tena kujiwekea saa ya kujifuraisha. (Muh. 8:15) Dada moya anaonesha kile kinamusaidiaka endelee kuwa na furaa, anasema ivi: “Saa yulu kuko kuzuri na kuko ka mpepo kazuri, minatokaka inje na kwikalako pa ka yuwa. Karibu mala moya kila mweji minapangaka programe ya kwenda kujifuraisha pamoya na barafiki.”

13. Nju ya nini ni muzuri kucheka? (Mezali 17:22)

13 Tafuta bintu bya kukuchekesha. (Soma Mezali 17:22; Muh. 3:1, 4) Kucheka kutakusaidia ushikuwe na mangaiko ya mingi. Saa uko nangaikia muntu, inekalaka nguvu mambo yote ipitikane vile muripenda. Lakini kama unapata bintu bya kukuchekesha ata mu ma sitwasion ya nguvu, ile itakusaidia ushikuwe na uzuni. Na, kucheka pamoya na muntu ule uko nachunga kutamisaidia mukuwe barafiki.

14. Namna kani kusumburia na rafiki ule unatumainia kunezi kukusaidia?

14 Sumburia na rafiki ule unatumainia. Ata kama uko nafanya nguvu yako yote nju wendelee kuwa na furaa, saa moya utashikia tu sa mambo inakupitia. Saa unajishikia vile, kintu kile kitakusaidia ni kusumburia na rafiki muzuri ule atakusadia ushijishikie mubaya nju ya mambo ile uko nasema. (Mez. 17:17) Pengine namna atakushikia na bile atakwambia njo bile uko nabyo lazima nju wendelee kuwa na furaa.​—Mez. 12:25.

15. Namna kani kusumburia nju ya paradi kutakuletea furaa?

15 Wazia namna maisha yako na ya ule uko nachunga itakuwa mu paradi. Kumbuka asema kaji ya kuchunga muntu wa malari ao wa kuzeka ni ya wakati kiloko na aina ile kaji njo Jeova aripachiaka bantu saa aribaumbaka. (2 Ko. 4:16-18) “Maisha ya bya kweri” iko natuchunga ku mbele. (1 Ti. 6:19) Kusumburia na muntu ule unapenda nju ya mambo ile mutafanya pamoya mu paradi kutakuletea furaa sana. (Isa. 33:24; 65:21) Dada Heather anasema ivi: “Mala mingi minambiaka bantu bale niko nachunga asema mu paradi, tutashona pamoya, tutakimbia pamoya, na tutatembesha mankinga pamoya. Tutafanya mikate na kupika byakurya nju ya bale batafufuka. Na pamoya tunamupikiaka Jeova merci nju ya tumaini ile tuko nayo.”

NAMNA BENGINE BANEZI KUSAIDIA

16. Tunezi kusaidia je bantu ba mu kutaniko yetu bale banachungaka muntu wa kuzeeka ao wa malari? (Angaria na foto.)

16 Tubasaidie bapate wakati ya kupumujika. Banduku na badada banezi kulomba kupitisha wakati na muntu ule uko nachunga. Kama banafanya vile, ile itakusaidia upate wakati ya kupumujika na kufanya mambo ingine ile uripenda kufanya. (Gal. 6:2) Banduku na badada bengine banapangaka programe nju kila juma kukuwe muntu moya ule atasaidia ule eko nachunga muntu wa kuzeka ao wa malari. Dada Natalya anachungaka bwana yake ule ashakupoza. Anasema ivi: “Kila juma kuko nduku moya wa mu kutaniko yetu ule anakuyaka. Anakuyaka mala moya ao mala mbiri ku juma nju ya kupitisha wakati pamoya na bwana yangu. Banaubiri pamoya, banasumburia pamoya na banafwata ata mafilme pamoya. Bwana yangu anafuraiaka sana saa ile anapitishaka pamoya na rafiki wa mu kutaniko. Na ile inanisaidiaka nipate wakati ya kupumujika na kufanya mambo ingine ile minapenda.” Saa moya unezi ata kusaidia kuchunga muntu wa kuzeka ao wa malari bushiku, nju ya kusaidia mwenye anamuchungaka alale muzuri.

Badada bawiri banatembelea dada wa kuzeka. Ule anamuchungaka eko natoka na anabapepea na furaa.

Namna kani tunezi kusaidia muntu wa mu kutaniko yetu ule eko nachunga muntu wa malari ao wa kuzeka? (Angaria mu paragrafe 16)a


17. Saa ya marenion tunezi kusaidia je ule anachungaka muntu wa malari ao wa kuzeka?

17 Tubasaidie saa ya marenion. Saa moya inekalaka nguvu kwa bale beko nachunga muntu wa malari ao wa kuzeka kufwata muzuri marenion na maasamblé. Nju saa yote banekalaka beko nangaikia muntu ule beko nachunga. Nju ya kubasaidia, bengine mu kutaniko banezi kwikala ku mpembeni ya muntu ule ashakuzeka ao ule eko malari nju ya kusaidia ule anamuchungaka afwateko ata kipande ao ata renion yote. Kama muntu ule banachungaka ashiwezi kutoka ku nyumba, tunezi kwenda kwake nju ya kufwata naye renion ku visioconférence ao ku zoom nju ya kusaidia ule anamuchungaka ende afwatie marenion ku salle du royaume.

18. Tunezi kufanya nini ingine nju ya kusaidia bale beko nachunga muntu wa kuzeka ao wa malari?

18 Tubaankurajé na tusali nju yabo. Bazee banafanyaka muzuri saa banatembeleaka mala mingi bale banachungaka muntu wa kuzeka ao wa malari nju ya kubapachia nguvu. (Mez. 27:23) Na shiye bote mu kutaniko ata tukuwe mu sitwasion kani, ni muzuri tuzobelee kwankurajé bantu ba vile. Tunezi tena kumulomba Jeova endelee kubapachia nguvu na abasaidie baendelee kuwa na furaa yabo.​—2 Ko. 1:11.

19. Uku ku mbele tuko nachunga nini ifanshike?

19 Mu mashiku kiloko Jeova atatosha byote bile binatuleteaka uzuni. Malari na lufu abitakuyakako tena. (Ufu. 21:3, 4) “Kilema ataluka-luka sa nkasha.” (Isa. 35:5, 6) Mateso ile buzee bunaletaka na magumu ya kwangaikia muntu ule eko malari ao wa kuzeka bitakuwa “mambo ya nzamani . . . ile . . . aitaangaisha tena ku roo.” (Isa. 65:17) Leo, ata kama tungari nachunga ile mambo ifanshike, Jeova ashitatwacha. Kama tunaendelea kumutumainia nju atupachie nguvu atatusaidia ‘kuvumilia na tuko na furaa.’​—Kol. 1:11.

UTAJIBU JE?

  • Ni mambo kani njo inezi kufanya bale beko nachunga muntu wa kuzeka ao wa malari bapoteshe furaa?

  • Ni nini inezi kubasaidia baendelee kuwa na furaa?

  • Namna kani tunezi kubasaidia mu kutaniko yetu?

MWIMBO 155 Furaha Yetu ya Milele Inatoka kwa Yehova

a ESPLIKASION YA FOTO: Badada biyana bawiri banakuya kubakia na dada wa kukomea nju ya kusaidia ule anamuchungaka apate wakati ya kufanya mambo ingine.

    Swahili (Katanga) Publications (2020-2026)
    Toka
    Ingia
    • Swahili (Katanga)
    • Partajé
    • Preferanse
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni ya kutumikisha
    • Règles de confidentialité
    • Paramètres de confidentialité
    • JW.ORG
    • Ingia
    Partajé