ABARI YA KUFUNDA YA 46
MWIMBO 17 “Ninataka”
Yesu ni pretre mukubwa ule anajiwekaka pa fashi yetu
“Atuna na pretre mukubwa ule ashiwezi kushikiria buluma ma buzaifu yetu.”—EBR. 4:15.
MU KIFUPI
Yesu ni pretre mukubwa muzuri sana ule anajiwekaka pa fashi yetu na kutusaidia mu manjia ya kwachana-achana.
1-2. a) Nju ya nini Jeova arimutuma Mutoto yake pa dunia? b) Tutafunda nini mu iyi abari? (Waebrania 5:7-9)
KUSHAKUPITA miaka 2 000 na bya yulu, Jeova aritumaka pa dunia mutoto yake ule anapendaka sana. Nju ya nini? Nju ya ma rezon ya mingi. Rezon moya ni kukombola bantu mu nzambi na lufu na kutengeneza mambo yote ile Shetani arialabisha. (Yoh. 3:16; 1 Yo. 3:8) Rezon ingine njo iyi: Jeova ariyuwa asema kama Yesu anakuwa muntu na anaishi pa dunia, atakuwa pretre mukubwa muzuri ule atajiweka pa fashi ya bantu. Yesu arianza kaji yake ya bu pretre mukubwa mu mwaka ya 29, kisha kupata bateme.a
2 Mu iyi abari, tutaona namna kuishi pa dunia kurimusaidia Yesu akuwe pretre mukubwa ule anajiweka pa fashi ya bengine. Ni kintu kya lazima sana kukomprandre vile, nju kuyuwa vile kutafanya ikuwe teketeke kwetu kusali kwa Jeova na kuwa karibu naye ata kama tuko najishikia mubaya nju ya mankosa yetu.—Soma Waebrania 5:7-9.
MUTOTO WA MUNGU ANAKUYA PA DUNIA
3-4. Maisha ya Yesu irikuwa je saa ariamia pa dunia?
3 Saa moya, kutoka fashi moya na kwamia fashi ingine aikalake teketeke, nju tunapashwa kwacha nyumba yetu ile tunapendaka sana, barafiki na bantu ba mu famiye yetu. Lakini, akuna ata muntu moya ule ashakupataka magumu sa ile Yesu aripataka saa ariamaka kutoka ku mbingu na kuya apa pa dunia. Ku mbingu ye njo arikuwa malaika wa kwanza na wa yulu sana kupita bote. Jeova arikuwa ashakumupenda sana na Yesu arikuwa na furaa sana nju arikuwa eko natumika ku “mukono ya droite” ya Baba yake. (Zb. 16:11; Mez. 8:30) Lakini, Wafilipi 2:7 inaonesha asema Yesu ariachaka byote bile arikuwa nabyo ku mbingu nju ya kuya kuishi apa pa dunia pamoya na bantu bashipo kukamilika.
4 Tena, waza vile mambo irikuwaka saa Yesu arikuwaka mutoto. Sakrifise ile bazazi yake baritowaka kisha yeye kuzarika, inaonesha asema Yesu arizarika mu famiye ya bamasikini. (Law. 12:8; Lu. 2:24) Saa mufalme mubaya Hérode aripata abari asema Yesu anazarika, aritafuta kumuuwa. Nju Yesu abakie mujima, famiye yake irikimbiria mu Egypte na kule barikuwa ba réfugié. (Mt. 2:13, 15) Maisha ya Yesu pa dunia iriachana sana na ile arikuwaka nayo ku mbingu!
5. Yesu ariona nini pa dunia, na namna kani ile irimutayarisha nju ya kaji yake ya bu pretre mukubwa? (Angaria na foto.)
5 Saa Yesu arikuwa pa dunia, ariona bantu ba mingi beko nateswa. Yesu anayuwa muzuri buchungu bule muntu anashikiaka saa anafisha, nju na ye arifishaka bantu bale anayuwa. Pengine, baba yake Joseph na ye arikuwa mu bale bantu arifisha. Saa Yesu arianza kuubiri, arikutana na bale barikuwa na malari ya bukoma, bipofu, bantu ba kupoza, na bazazi bale barifisha batoto; na aribashikiria buluma sana. (Mt. 9:2, 6; 15:30; 20:34; Mk. 1:40, 41; Lu. 7:13) Ni kweri, tangu ku mbingu saa arikuwaka ku mpembeni ya Baba yake, arianzaka kuona bantu beko nateswa pa dunia. Lakini, saa arikuwa pa dunia, arikomprandre muzuri vile bantu banarishikiaka saa beko nateswa. (Isa. 53:4) Maisha ya Yesu pa dunia irimusaidia akomprandre muzuri mateso ya bantu. Na ye arianzaka kujishikia sa vile bantu bote banajishikiaka. Na ye arichokaka, arikuwaka na mangaiko na arikuwaka na uzuni.
Yesu ariangaikia sana bantu bale barikuwa karibu naye, ariona mateso yabo na vile barianza kujishikia (Angaria paragrafe 5)
YESU ARIJIWEKA PA FASHI YA BENGINE
6. Bile profete Isaïe arisemaka nju ya Yesu, binatufundisha nini nju ya namna yake ya kujiweka pa fashi ya bengine? (Isaya 42:3)
6 Saa Yesu arianza kufanya kaji yake apa pa dunia, ariona bantu bale barianza kujishikia mubaya nju benzabo barianza kubaonea na kubatendea mubaya, na aribashikiria buluma sana. Ile mambo Yesu arifanya, inapatana na ile Jeova arisemaka kupitia profete Isaïe. Mu mandiko ya kiebrania, mala mingi banafananishaka bale beko na imani ya nguvu kwa Jeova na jardin ya muzuri ile bintu biko naotamo muzuri, ao banabafananishaka na michi ya muzuri na ya mulefu sana. (Zb. 92:12; Isa. 61:3; Yer. 31:12) Lakini bamasikini na bale abana na muntu wa kubasaidia, banabafananisha na nkamba ya lampi ile iko karibu kujimika. (Soma Isaya 42:3; Mt. 12:20) Jeova aritumikisha ile mufano nju ya kuonesha vile Yesu atatendea bantu ba nivo ya chini na mapendo na atajiweka pa fashi yabo.
7-8. Namna kani Yesu aritimiza profesi ile iko mu kitabu kya Isaya?
7 Kitabu kya Matayo kinaonesha asema Yesu aritimizaka iyi misemo ya profete Isaïe: “Ashitavunja matete ile iko karibu kuvunjika, na ashitajima nkamba ya lampi ile iko karibu kujimika.” Kuko miujiza ya Yesu ile irisaidiaka bantu bale barianza kuonekana sa ni ba nivo ya chini, bale barianza kujishikia sa matete ile iko karibu kuvunjika ao bale abakukuwe na kitumaini bale barianza kujishikia sa nkamba ya lampi ile iko karibu kujimika. Kwa mufano, Yesu ariponeshaka mwanaume moya ule arikuwa na malari ya bukoma maungu mujima. Pengine ule mwanaume ashikukuwake ata na tumaini ya kiloko, ya kusema ataponaka na atafuraia tena kuwa pamoya na bantu ba famiye yake na barafiki yake. (Lu. 5:12, 13) Mufano ingine ni ya muntu ule arikuwaka kiziwi, ule ashikwanzake kusema muzuri, ule Yesu ariponeshaka. Wazia vile ule muntu arianzaka kujishikia saa arianzaka kuona bantu bengine beko nasumburia, lakini ye ashikwanzake kubishikia. (Mk. 7:32, 33) Na kuko mifano ingine ya mingi.
8 Mu wakati ya Yesu, Bayaudi ba mingi barianza kwamini asema bantu bale barikuwa malari ao ba bilema, barikuwa vile nju ya manzambi ile barifanyaka ao nju ya manzambi ile bazazi yabo barifanyaka. (Yoh. 9:2) Nju barikuwa na mawazo ya vile, barianza kuona ba bilema na bantu ba malari sa bantu ba bule sana. Lakini Yesu ye aritimiza profesi ile iko mu kitabu kya Isaya. Ariponesha bale bantu na aribasaidia baone kama beko ba valere ku mbele ya Mungu. Ile inatufanya tukuwe sire asema Yesu anatuonaka je leo?
9. Namna kani Waebrania 4:15, 16 inaonesha asema Yesu, pretre wetu mukubwa, anajiwekaka pa fashi ya bantu bale abakamilike?
9 Soma Waebrania 4:15, 16. Tunezi kuwa sire asema kila shiku Yesu atendelea tu kujiweka pa fashi yetu. Njo kusema nini? Kujiweka pa fashi ya bengine ni kukomprandre mateso yabo na vile beko najishikia na kupenda kubasaidia. “Kujiweka pa fashi ya bengine” kunatoka mu maneno ya kigreke ile inapenda kuonesha, kupitia mu mateso ile muntu mwingine ekwamo na kujishikia vile eko najishikia. (Angaria na Waebrania 10:34, mule Paulo anatumikisha paka ile musemo ya kigreke.) Miujiza ile Yesu arifanya inaonesha vile arijishikia mubaya sana nju ya mateso ya bengine. Yesu ashikukuwe tu eko naponesha bantu nju tu aripashwa kufanya vile. Aribangaikia bya kweri na aripenda kubasaidia. Kwa mufano, saa ariponeshaka ule muntu arikuwa na malari ya bukoma, arikuwaka na nguvu ya kumuponesha ata lwa mbari, lakini aripenda kumuchofea na kumubamba. Pengine Yesu njo arikuwa muntu wa kwanza kumubamba mu miaka yote ile arikuwa na ile malari! Nju ya kuponesha mwanaume ule arikuwa kiziwi, Yesu arimutosha mu makelele ya bantu, na kwenda naye ku mpembeni nju ya kumuponesha. Na waza nju ya mwanamuke ule arinawishaka mikulu ya Yesu na machozi yake na kuipangusha na nywele yake. Ule mwanamuke arianzaka kufanya bibaya, lakini aritubu. Bafarisayo barianza kusema mubaya sana nju yake, lakini Yesu arimusemelea na aripenda bafarisayo bashikuwe na ile mawazo ya mubaya. (Mt. 8:3; Mk. 7:33; Lu. 7:44) Yesu ashikwanzake kukimbia bale barikuwaka na malari ao bale barifanyaka manzambi ya nguvu. Lakini, aripendaka bakuye kwake na bajishikie kama anabapenda. Tunezi kuwa sire asema njo vile Yesu anajiwekaka na pa fashi yetu.
TUMUFWATIRISHE PRETRE WETU MUKUBWA
10. Ni bintu kani bile tuko nabyo leo nju ya kusaidia biziwi na bipofu? (Angaria na mafoto.)
10 Nju tuko badisiple ba Yesu, na shiye tuko nafanya nguvu yetu yote nju tuoneshe mapendo na tujiweke pa fashi ya bengine sa vile Yesu arifanyaka. (1 Pe. 2:21; 3:8) Ata kama shiye atutaweza kuponesha biziwi na bipofu, tunezi kubasaidia bamuyuwe Jeova na bakuwe barafiki yake. Kwa mufano, leo tuko na bitabu bile binasemea nju ya Bible mu ma langue de signe ya kwachana-achana 100 na bya yulu. Na nju ya kusaidia bale abaonake muzuri, tuko na bitabu bya braille bile biko mu maluga 60 na bya yulu. Tunafanyaka ma audiodescription ya bitabu byetu mu maluga 100 na bya yulu. Bile byote ni nju ya kusaidia ba biziwi na ba bipofu bakuwe barafiki ba Jeova na ba Mutoto yake Yesu.
Bitabu byetu bile binasemea Bible biko mu maluga 1 000 na bya yulu
Ku gauche: Ma langue de signe 100 na bya yulu
Ku droite: Mu braille ya maluga 60 na bya yulu
(Angaria paragrafe 10)
11. Yesu arionesha asema eko nangaikia bantu ba mafashi yote. Namna kani organizasion ya Jeova iko nafwata mufano yake? (Matendo 2:5-7, 33) (Angaria na mafoto.)
11 Organizasion ya Jeova iko nafanya nguvu yake yote nju ya kusaidia bantu ba mafashi yote bamuyuwe Jeova na bakuwe barafiki yake. Kumbuka asema kisha Yesu kufufuka, aripachiaka bantu roo takatifu nju baweze kusema mu maluga ya kwachana na nju bale bote barikutana nju ya feti ya pantekoste bashikie abari njema kila muntu “mu luga yake.” (Soma Matendo 2:5-7, 33.) Nju ya kufwata mufano ya Yesu, organizasion ya Jeova iko natosha bitabu bile biko nasema nju ya Bible mu maluga 1 000 na bya yulu. Na mu ile maluga, muko ile ni bantu kiloko tu njo banaisemaka. Kwa mufano, kuko maluga ile ni bantu kiloko tu bale banekalaka ku nord na ku sud ya Amérique njo banaisemaka. Lakini, organizasion ya Jeova iko natosha bitabu mu ile maluga kiloko-kiloko 160 na bya yulu nju ya kusaidia bantu ba mingi bapate abari njema. Organizasion yetu inatoshaka tena bitabu mu maluga ya ba Roms 20 na bya yulu. Bantu ba mingi bale banasemaka ile maluga barifunda Bible na bashakwanza kumutumikia Jeova.
Ku gauche: Mu maluga ya kiloko-kiloko 160 na bya yulu ile banasemaka ku nord na ku sud ya Amérique
Ku droite: Mu maluga 20 na bya yulu ya ba Roms
(Angaria paragrafe 11)
12. Organizasion ya Jeova inafanyaka tena nini nju ya kusaidia bantu?
12 Organizasion ya Jeova inafanyaka mambo ya mingi nju ya kusaidia bantu bakuwe barafiki yake ya Jeova. Lakini tena inasaidiaka bale baripata ma catastrophes naturelles. Njo maana, banduku na badada ba mingi banajitoaka nju ya kusaidia bale baripata ma catastrophes naturelles. Tena, organizasion inayengaka mafashi ile itasaidia bantu bamwabudu Jeova na bafunde nju ya mapendo yake.
PRETRE WETU MUKUBWA ATAKUSAIDIA
13. Yesu anatusaidiaka je?
13 Nju Yesu ni muchungaji wetu muzuri sana, anangaikiaka ali ya kiroo ya kila muntu. (Yoh. 10:14; Efe. 4:7) Saa moya, tunezi kukutana na ma sitwasion mu maisha ile inezi kutufanya tujishikie sa nkamba ya lampi ile inatafuta kujimika ao matete ile iko karibu kuvunjika. Mambo sa vile malari ya nguvu, mankosa ile tunafanyaka, ao kukosana na muntu mu kutaniko binezi kutulekesha sana. Inezi kuwa nguvu sana kwetu kwacha kuwaza ile mambo na kuweka akiri nju ya tumaini yetu ya wakati ya ku mbele. Kumbuka asema Yesu anayuwa muzuri mambo ile uko napitiamo, na anakomprandre muzuri mawazo ile iko mu roo yako. Yesu anapenda kukusaidia nju eko najiweka pa fashi yako. Kwa mufano anezi kutumikisha roo takatifu nju ya kukusaidia upate tena nguvu. (Yoh. 16:7; Tit. 3:6) Tena Yesu anezi kutumikisha bazee bale beko sa kado ile Jeova aritupachia nju ya kutusaidia na kutupachia nguvu. Na tena anezi kutumikisha ata banduku na badada bengine.—Efe. 4:8.
14. Tunezi kufanya nini saa tuko dekurajé?
14 Kama uko dekurajé, kumbuka asema Yesu ni pretre wetu mukubwa. Na kuwaza sana nju ya ile kunezi kukusaidia. Kumbuka asema Jeova ashikumutumake Yesu apa pa dunia nju tu ya kutukufwia, lakini arimutumaka tena nju aweze kukomprandre muzuri magumu ile bantu bale abakamilike banapataka. Kama tunajishikia mubaya nju ya nzambi ile turifanya ao nju ya buzaifu bwetu, tuyuwe asema Yesu eko pale nju ya kutusaidia na atatusaidia “mu wakati ya muzuri.”—Ebr. 4:15, 16.
15. Leta mufano ile inaonesha kile kirisaidiaka nduku moya arudie tena mu kutaniko.
15 Tena, Yesu anaongozaka bantu bake basaidie bale bashakumwacha Jeova bamurudirie. (Mt. 18:12, 13) Tubebe mufano ya nduku Stefano.b Barimutosha mu kutaniko. Kisha kufanya miaka 12 inje ya kutaniko, aridesidé kwenda ku renion. Anasema ivi: “Aikukuwe teketeke, lakini niripenda tena kurudia mu famiye ya Jeova. Bazee bale nirikutana nabo barinikaribisha muzuri. Miripendaka kubiacha, nju saa moya nirianzaka kujishikia sa wa bule nju nirimwachaka Jeova. Lakini bale banduku barinikumbusha asema Jeova na Yesu banapenda nishirudie ku mukongo. Saa barinirudishaka mu kutaniko, banduku na badada bote barinikaribishaka muzuri miye na famiye yangu. Bibi yangu arichika kwanza kufunda Bible, na leo tuko namutumikia Jeova pamoya.” Pretre wetu mukubwa Yesu anashikiaka furaa sana saa anaona bantu bote mu kutaniko banasaidia muntu ule aritubu arudie tena!
16. Nju ya nini uko na furaa sana nju uko na pretre mukubwa ule anajiwekaka pa fashi yako?
16 Mu maisha yake ya apa pa dunia, Yesu arisaidia bantu ba mingi sana saa barikuwa na lazima ya muntu wa kubasaidia. Leo, tunezi kuwa sire asema atatusaidia saa yoyote ile tunezi kuwa lazima naye. Na mu dunia mupya ile iko karibu sana, atatusaidia shiye bote tukuwe na maisha yashipo nzambi na ya kukamilika. Tunamupikia Jeova merci sana, nju mapendo yake ya nguvu na buluma bwake birimusukuma amuweke Yesu kuwa pretre wetu mukubwa ule anajiwekaka pa fashi yetu!
MWIMBO 13 Kristo Ni Mufano Muzuri
a Nju ya kuyuwa mambo mingi nju ya namna Yesu aribeba fashi ya pretre mukubwa wa wakati ya Bayaudi ba nzamani, soma abari “Furahia Pendeleo Yako ya Kumutumikia Yehova mu Hekalu Yake ya Kiroho” mu Munara ya Mulinzi ya Octobre 2023, paje 26, paragrafe 7-9.
b Turishanjé manjina ingine.