BIBLIOTEKE YA KU ENTERNETE Watchtower
Watchtower
BIBLIOTEKE YA KU ENTERNETE
Swahili (Katanga)
  • BIBLE
  • BITABU
  • MA RENION
  • w25 Décembre pp. 8-13
  • Kitabu kya Yobu kinezi kukusaidia saa unapenda kuleta shauri

Akuna video nju ya iyi selection.

Pardon, kurikuwa erreur mu chargement ya video.

  • Kitabu kya Yobu kinezi kukusaidia saa unapenda kuleta shauri
  • Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
  • Sous-titres
  • Ya kufanana na iyi
  • NAMNA BARAFIKI BATATU BA YOBU BARIMUSHAURIA
  • ÉLIHOU ARIMUSHAURIAKA JE YOBU?
  • KITABU KYA YOBU KIENDELEE KUKUFUNDISHA MAMBO YA MINGI
  • Kitabu kya Yobu kinezi kukusaidia saa uko mu magumu
    Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
w25 Décembre pp. 8-13

ABARI YA KUFUNDA YA 49

MWIMBO 44 Sala ya Mutu wa Hali ya Chini

Kitabu kya Yobu kinezi kukusaidia saa unapenda kuleta shauri

“Lakini sasa, Yobu, shikiako misemo yangu.”​—YOBU 33:1.

MU KIFUPI

Namna kitabu kya Yobu kinezi kutusaidia kuleta mashauri ya muzuri

1-2. Ni nini irifanya ikuwe nguvu kwa bale banaume batatu na kwa Élihou kumusaidia Yobu?

ABARI inazambalala mbio sana sa miumbi ya kirio! Yobu ule arikuwa na mari mingi, anapotesha bintu byake byote. Saa Élifaz, Bildad, na Zofar, barafiki yake ya Yobu baripata ile abari, barifanya safari ya kwenda Ouz nju ya kumupachia nguvu. Saa barifika, barishangaa sana kumukuta Yobu mu ile sitwasion.

2 Waza vile mambo irikuwa. Yobu aripotesha karibu bintu byake byote: Bangombe, ba chameaux, bankondolo, byote biripotea. Batoto yake bote barimukufwa, barimuwia batumishi bake ba mingi, na nyumba mule batoto yake barikufwia iripomoka. Magumu aikwishie paka pale, na Yobu mwenyewe arilukula sana. Maungu yake yote iriyala bivimbo. Bale barafiki yake batatu, barimuona Yobu ashakwikala mu maivu na eko na uzuni. Batafanya nini sasa? Banafanya mashiku 7 pashipo kumwambia Yobu ata kintu kimoya, ata kama banamuona vile eko nateswa sana. (Yob. 2:12, 13) Kisha, kiyana moya arifika pale, ule kiyana arikuwa Élihou, na ye ariikala ku mpembeni ya bale banaume. Ku mwisho, Yobu ananza kusema. Anasema kama aripashwaka ata kufwa, ashikupashwake ata kuzarika. (Yob. 3:1-3, 11) Kusema tu bya kweri, Yobu arikuwa na lazima benzake bamusaidie! Lakini, kumusaidia aikukuwe teketeke. Bile bale banaume batasema, bitaonesha asema beko barafiki bazuri bale banamwangaikia ao apana. Tuone kile batafanya.

3. Tutafunda nini mu iyi abari?

3 Jeova arimuongoza Moïse anjike mambo ile barafiki batatu ba Yobu na Élihou barifanya na kusema. Élihou arisema mambo ile iripatana na mapenzi ya Jeova. Lakini Elifaz yeye arisema mambo ya mubaya, na pengine ni mpepo mubaya njo irimusukuma aseme vile. (Yob. 4:12-16; 33:24, 25) Njo maana, mu kitabu kya Yobu tunezi kupatamo mashauri ya muzuri sana sa ile Élihou ariletaka, na mashauri ya mubaya sana sa ile barafi batatu ba Yobu bariletaka. Kitabu kya Yobu kinezi kutusaidia tuyuwe namna ya muzuri ya kuleta mashauri. Tutaona mbele mufano mubaya ya barafiki batatu ba Yobu, na kisha tutasemea nju ya mufano ya muzuri ya Élihou. Mu kila mufano, tutaona namna kitabu kya Yobu kiripashwa kusaidia batoto ba Israel na namna kinezi kutusaidia na shiye leo.

NAMNA BARAFIKI BATATU BA YOBU BARIMUSHAURIA

4. Nju ya nini bale barafiki batatu ya Yobu barishinda kumwankurajé? (Angaria na foto.)

4 Bible inaonesha asema barafiki batatu ba Yobu, baripenda “kumufishako Yobu na kumupachia nguvu” nju ya mambo yote ile irimupata. (Yob. 2:11) Lakini barishinda kufanya vile. Nju ya nini? Nju ya mambo tatu. Ya kwanza, abakubebe wakati ya kumushikia na ya kukomprandre sitwasion yake. Kwa mufano, bariwaza asema ni Jeova njo arimuletea Yobu ile mateso nju ya mankosa ile arifanyaka.a (Yob. 4:7; 11:14) Ya piri, mambo mingi ile barimwambia Yobu aikumusaidie, ata kama irionekana sa ni ya muzuri. Kusema tu bya kweri, mambo ile barimwambia irifanya ajishikie mubaya sana. (Yob. 13:12) Kwa mufano, mala mbiri Bildad arimonesha Yobu asema ‘eko nasema mingi.’ (Yob. 8:2; 18:2) Na saa moya bale banaume barisema maneno ile iko naumisha roo. Kwa mufano, Zofar arimwambia Yobu asema ‘eko bumbafu.’ (Yob. 11:12) Ya tatu, ata kama pengine abakumufokee Yobu, misemo yabo irionesha asema abakumweshimie, na abakumupende. (Yob. 15:7-11) Bale banaume, bariendelea tu kumwambia Yobu asema arifanya nzambi na abakumwankurajé.

Rafiki moya wa Yobu eko namutombokea, na bale bengine bawiri beko nangaria. Yobu ashakwikala chini na eko nashikia. Eko na maumivu nju ya bivimbo bile eko nabyo maungu mujima.

Saa uko nashauria muntu, ushimufanye arione sa eko wa chini. Ukuwe pale nju ya kumusaidia (Angaria paragrafe 4)


5. Kisha barafiki batatu ba Yobu kumushauria, mambo irikuwa je?

5 Saa Élifaz, Bildad na Zofar barisha kusema, Yobu arishikia mubaya sana kupita ata na vile barimukuta. (Yob. 19:2) Nju baripenda kumuonesha asema nkosa ni yake, Yobu na ye aripenda kuonesha asema ashina na nkosa, na njo pale arianza sasa kusema mambo yashipo mu njia. (Yob. 6:3, 26) Mambo ile bale barafiki batatu ba Yobu barisema aikupatane na mawazo ya Jeova. Na mambo ile barifanya irionesha asema abakuriweke pa fashi ya Yobu. Na pashipo ata bo kupenda, Shetani aribatumikisha nju ya kumulekesha Yobu. (Yob. 2:4, 6) Pengine iyi abari irisaidia je batoto ba Israel? Na inezi kutusaidia je leo?

6. Mufano mubaya ya barafiki ya Yobu iripashwaka kufundisha nini bazee ba Israel?

6 Namna abari ya Yobu iripashwa kusaidia batoto ba Israel. Saa Jeova aripachiaka batoto ba Israel Sheria, aribapachiaka na bazee bale baripashwa kubaongoza na kubasaidia bafwate ile Sheria. (Kum. 1:15-18; 27:1) Bale bazee, baripashwa kushikia muzuri mambo mbele ya kuleta mashauri ao mbele ya kuukumu. (2 Ny. 19:6) Tena, baripashwa kuuliza maulizo nju ibasaidie kukomprandre mambo muzuri, kuriko kuwaza asema banayuwa mambo yote. (Kum. 19:18) Saa bantu barianza kubatafuta nju babasaidie, bale bazee baripashwa kusema na bupole. Nju ya nini? Nju kufanya vile, kuripashwa kusaidia muntu abaambie mambo ile eko nayo ku roo. (Kut. 22:22-24) Iyi ni mambo ingine ile bazee ba Israel baripashwaka kufunda mu abari ya Yobu.

7. Kutoshako bazee ba Israel, ni ba nani bengine baripashwa kuleta mashauri? Na abari ya Yobu iripashwaka kubasaidia je? (Mezali 27:9)

7 Aina paka bazee mu Israel njo barikuwaka na kaji ya kupachia bengine mashauri. Kila muntu, ni kusema, mutoto, mukubwa, mwanaume ao mwanamuke, arikuwa na kaji ya kushauria mwenzake nju akuwe na burafiki bwa muzuri pamoya na Jeova na nju akatale kufanya mambo ya mubaya. (Zb. 141:5) Barafiki ba bya kweri banapendaka kushauriana. (Soma Mezali 27:9.) Mufano mubaya ya barafiki batatu ba Yobu, irisaidia batoto ba Israel bayuwe mambo ile abapashwe kusema ao ile abapashwe kufanya saa beko naleta mashauri.

8. Ni mambo kani tunapashwa kufanya saa tunapenda kushauria muntu? (Angaria na mafoto.)

8 Namna abari ya Yobu inezi kutusaidia. Na shiye nju tuko bakristo, tunapendaka kusaidia banduku na badada yetu saa beko mu magumu. Nju tuweze kufanya vile, tunapashwa kwepuka mambo ile barafiki babaya batatu ba Yobu barifanyaka. Kya kwanza, atupashwe kwanza kuwazia-wazia mambo. Tunapashwa kuyuwa muzuri abari yote mbele ya kuleta shauri. Kya piri, mashauri yetu inapashwa kutoka mu Sauti ya Mungu. Atupashwe kuwa sa Élifaz, ule arileta mashauri ya kutoka mu kichwa kyake. (Yob. 4:8; 5:3, 27) Na kya tatu, atupashwe kutumikisha misemo ya kuumisha muntu roo ao ile inaonesha asema atuna na mapendo. Kumbuka asema, saa moya Élifaz na barifiki yake barisemaka mambo ya bya kweri. Ata Paulo aritayaka maneno ya Elifaz. (Komparé Yobu 5:13 na 1 Wakorinto 3:19.) Lakini mambo ya mingi ile Élifaz, Bildad na Zofar barisema nju ya Mungu, irikuwa ya bongo na irimuuma sana Yobu ku roo. Njo pale Jeova arisema kama mambo yote ile barisema aikukuwe ya bya kweri. (Yob. 42:7, 8) Saa tuko napachia bengine mashauri, tunapashwa kufanya nguvu nju bile tutasema bishifanye bantu bamuone Jeova asema ni Mungu wa roo mubaya, ule ashipendake batumishi bake. Sasa, tuone mambo ile mufano ya Élihou inezi kutufundisha.

Mafoto: Nduku moya eko namushauria nduku mwingine ule eko na uzuni. Na eko nafanya vile na roo ya mapendo. 1. Nduku moya eko namushikia mwenzake saa eko namwambia magumu yake. Bote bawiri bashakwikala inje na beko nakunywa jus. 2. Ule nduku arianza kushikia anafungula Bible. 3. Ule nduku ananza kumupachia mashauri ya mu Bible. Ule nduku mwingine eko namushikia.

Saa uko naleta mashauri, (1) yuwa mambo muzuri, (2) tumikisha Sauti ya Mungu, na (3) sema mu namna ile inaonesha asema unamupenda ule muntu (Angaria paragrafe 8)


ÉLIHOU ARIMUSHAURIAKA JE YOBU?

9. a) Nju ya nini Yobu arikuwa na lazima ya muntu wa kumupachia nguvu kisha kusumburia na bale barafiki yake batatu? Espliké. b) Jeova arifanya nini nju ya kumusaidia?

9 Yobu na bale barafiki yake batatu baribishana sana, na bile barisema biriyaja mashapitre 28 ya mu kitabu kya Yobu. Na bya mingi bile barisema, baribisema mu makari. Njo maana Yobu arikuwa dekurajé sana! Arikuwa tu na lazima ya muntu wa kumupachia nguvu na kumusaidia. Jeova arimusaidia je Yobu? Aritumikisha Élihou nju ya kumupachia mashauri. Nju ya nini Élihou arichunga bengine baishe kusema nju na ye aseme? Ye moya arisema ivi: “Niko mutoto, na mweye muko bantu bakubwa. Njo pale, nju ya kumieshimia miirikala kimya.” (Yob. 32:6, 7) Élihou ariyuwa asema bantu bale bashakukomea, mala mingi banekalaka na ekima ya mingi nju bashakwishi mashiku ya mingi na bashakurionea mambo ya mingi mu maisha kupita babiyana. Lakini kisha kubashikia bote, Élihou ariona asema aina muzuri aendelee kubakia kimya. Arifikia kusema ivi: “Miaka yo yenyewe aifanyake muntu akuwe na ekima, na aina paka bazee njo banayuwaka mambo ya kunyoloka.” (Yob. 32:9) Élihou arisema tena nini? Na aribisema je?

10. Élihou arifanya nini mbele ya kumupachia Yobu mashauri? (Yob. 33:6, 7)

10 Mbele Élihou amupachie Yobu mashauri, arimusaidia Yobu atulizane na akuwe tayari kushikia bile atamwambia. Élihou arifanya vile je? Ye moya aritulizana mbele. Tunayuwa vile nju Bible inasema kama ku mwanzo Élihou arikuwa ashakushirika. (Yob. 32:2-5) Ata vile, Élihou ashikuseme naye mu makari. Kuriko kufanya vile, arijishusha na arisumburia na Yobu sa vile rafiki yake. Kwa mufano arimwambia Yobu ivi : “Angaria! Na miye niko tu paka sa weye ku mbele ya Mungu wa bya kweri.” (Soma Yobu 33:6, 7.) Élihou arionesha asema arimushikia Yobu muzuri. Njo maana mbele ya kumupachia Yobu mashauri, Élihou arirudiria mu kifupi mawazo munene ile Yobu arisema. (Yob. 32:11; 33:8-11) Na Élihou arifanya tena vile ile saa arimupachia mashauri ingine.​—Yob. 34:5, 6, 9; 35:1-4.

11. Élihou arimushauria je Yobu? (Yobu 33:1)

11 Saa Élihou arianza kumupachia Yobu mashauri, ashikumufanye Yobu aonekane wa bule, lakini arimweshimia ule mwanaume wa imani. Kwa mufano saa arianza kusumburia na Yobu, aritaya njina yake. Lakini pengine bale barafiki yake bengine batatu abakufanye vile. (Soma Yobu 33:1.) Pengine Élihou arikumbuka namna na ye aripenda kusema ile saa Yobu na bale barafiki yake batatu barianza kubishana. Njo maana arimwachia Yobu wakati ya kusema saa arianza kumushauria. (Yob. 32:4; 33:32) Tena, Élihou arimwambia Yobu waji-waji asema kuko mambo ile arisema ile aikukuwe ya muzuri. Na arimukumbusha asema Jeova eko na akiri mingi, eko na nguvu, eko na aki na eko na mapendo ya bya kweri. (Yob. 36:18, 21-26; 37:23, 24) Inawezekana mashauri ya muzuri ile Élihou arimupachia Yobu irimusaidia akuwe tayari kushikia mashauri ingine ile Jeova aripenda kumupachia. (Yob. 38:1-3) Namna kani mufano ya Élihou iripashwa kusaidia batoto ba Israel? Na namna kani inezi kutusaidia na shiye leo?

12. a) Jeova aritumikisha je baprofete nju ya kusaidia bantu bake? b) Mufano ya Élihou iripashwa kusaidia je batoto ba Israel?

12 Namna abari ya Yobu iripashwa kusaidia batoto ba Israel. Jeova ariwekaka baprofete nju bafundishe na basaidie batoto ba Israel. Kwa mufano, mu wakati ya ba juge, Jeova arimutumikishaka Déborah nju ya kuonesha bantu bake mambo ya kufanya. Tena, Jeova arimutumikishaka Samuel kwanzia wakati arikuwaka mutoto sana nju ya kuonesha batoto ba Israel mambo ya kufanya. (Amu. 4:4-7; 5:7; 1 Sa. 3:19, 20) Mu wakati ya bafalme, Jeova aritumikishaka baprofete ba mingi nju ya kusaidia batoto ba Israel bamwabudu vile anapenda. Na saa bantu abakwanze kufwata bile Jeova anasema, arianza kubatumia baprofete nju babasaidie batengeneze mambo. (2 Sa. 12:1-4; Mdo. 3:24) Mufano ya Élihou ile iko mu kitabu kya Yobu iripashwa kusaidia banaume na banamuke baminifu bayuwe kile batasema na namna ya muzuri ya kukisema saa beko napachia muntu mashauri.

13. Namna kani bakristo banapachiaka bakristo benzabo nguvu leo?

13 Namna mufano ya Yobu inezi kutusaidia na shiye leo. Na shiye nju tuko bakristo, tunaambiaka bantu mambo ile Mungu anapenda saa tuko nabaubiria mambo ile iko mu Bible. Tunatumikishaka tena Sauti ya Mungu nju ya kwankurajé banduku na badada yetu. (1 Ko. 14:3) Kila shiku bazee banapashwa kutumikisha misemo ya muzuri na ya mapendo saa beko nasumburia na muntu ule eko “dekurajé” ao ule anasema “mambo yashipo mu njia.”​—1 Te. 5:14; Yob. 6:3.

14-15. Leta mufano ile inaonesha namna muzee anezi kufwata mufano ya Élihou saa eko naleta mashauri.

14 Tubebe iyi mufano. Muzee anashikia asema dada moya wa mu kutaniko yabo eko dekurajé. Mala moya ule muzee pamoya na nduku mwingine banaenda kumutembelea ule dada nju ya kumwankurajé. Saa beko nasumburia naye, ule dada ananza kusema mambo pashipo kuwaza. Kisha anasema kama, ata kama eko naenda ku ma renion na mu maubiri ashina tu na furaa. Ule muzee atafanya nini?

15 Kya kwanza, ule muzee atapima kukomprandre kile kiko namwangaisha ule dada. Nju ya kufanya vile, ule muzee anapashwa kumuuliza ule dada maulizo na kushikia muzuri bile eko nasema. Eske eko nawaza asema Jeova ashimupende tena na ashina muntu muzuri? Eske ni “mangaiko ya maisha” njo iko namufanya arishikie mubaya? (Lu. 21:34) Kya piri, ule muzee atatafuta namna ya kumwankurajé ule dada nju ya bizuri bile eko nafanya. Kwa mufano, ata kama ule dada eko narishikia mubaya, anaendaka ku marenion na anaendaka mu maubiri. Na kya tatu, saa muzee anakomprandre mambo ile iko namwangaisha ule dada na ile iko namulekesha, atatumikisha Bible nju ya kumusaidia akomprandre asema Jeova anamupendaka.​—Gal. 2:20.

KITABU KYA YOBU KIENDELEE KUKUFUNDISHA MAMBO YA MINGI

16. Namna kani kitabu kya Yobu kinezi kwendelea kutusaidia?

16 Kitabu kya Yobu kinatufundisha mambo ya mingi ya muzuri sana! Sa vile turiona mu abari ile iritanguria, kitabu kya Yobu kinatusaidia kuyuwa nju ya nini Mungu anachaka mateso itupate na namna tunezi kuivumilia. Na sa vile turiona mu iyi abari, nju tupachie bengine mashauri ya muzuri, shiye bote tunapashwa kufwata mufano muzuri ya Élihou, apana mufano mubaya ya barafiki batatu ba Yobu. Auone asema itakuwa muzuri wendelee kukumbuka mambo ile tunafunda mu kitabu kya Yobu saa utapenda kushauria muntu? Kama panakawia tangu usome kitabu kya Yobu, auone asema ni muzuri upange programe ya kukisoma tena? Utavumbula asema muko mambo ya mingi ile unezi kufunda.

UTAJIBU JE?

  • Ni mambo kani atupashwe kusema saa tuko napachia muntu mashauri?

  • Namna Élihou arileta mashauri inatufundisha nini?

  • Namna kani kitabu kya Yobu kinezi kutusaidia?

MWIMBO 125 “Wenye Furaha Ni Wale Wenye Rehema!”

a Pengine ni mpepo mubaya njo irimusukumaka Élifaz awaze asema Jeova ashionake ata muntu moya kuwa mwaminifu, na akuna ata muntu moya ule anezi kumufuraisha. Ile mawazo mbiri ya bongo njo ile Élifaz ariaminia sana. Njo maana, kila wakati arianza kusumburia na Yobu arianza kurudiria ile mawazo ya bongo.​—Yob. 4:17; 15:15, 16; 22:2.

    Swahili (Katanga) Publications (2020-2026)
    Toka
    Ingia
    • Swahili (Katanga)
    • Partajé
    • Preferanse
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni ya kutumikisha
    • Règles de confidentialité
    • Paramètres de confidentialité
    • JW.ORG
    • Ingia
    Partajé