ABARI YA KUFUNDA YA 50
MWIMBO 48 Tutembee na Yehova Kila Siku
Turishushe sa vile Jeova anarishushaka
“Njo pale, sa vile muko batoto ya Mungu bale anapendaka sana, mwanze kumufwatirisha.”—EFE. 5:1.
MU KIFUPI
Jeova anarishushaka sana. Iyi abari itatuonesha mambo 4 ile tunezi kufanya nju ya kumufwatirisha.
1. Nju ya nini inashangaisha kuona vile Jeova anarishushaka sana?
SAA UNANGARIA bantu bale beko na mamlaka mu dunia ya leo, eske unezi kusema kama banarishushaka? Bantu ba mingi abarishushake ata. Lakini, ata kama Jeova eko yulu ya bote, yeye anarishushaka. (Zb. 113:5-8) Akuna ata muntu moya ule anarishushaka sa Jeova. Ashikalake ata na ka kiburi kaloko. Njo pale tutaona mambo 4 ile inaonesha asema Jeova anarishushaka. Na tutaona vile na shiye tunezi kumufwatirisha. Kufanya vile kutatusaidia sana. Tena tutaona vile Yesu na ye aririshushaka sa Baba yake. Saa tutanza kufunda ile mambo 4, tutaona vile inezi kutusaidia tukuwe karibu sana na Jeova na twanze kurishusha sana sa vile yeye.
JEOVA ANAFANYAKA TURISHIKIE KUWA KARIBU NAYE
2. Sa vile Zaburi 62:8 inaonesha, Jeova anekalaka Mungu wa je? (Angaria na foto ya pa couverture.)
2 Inekalaka nguvu kuchofea muntu ule anapendaka bya kuripandisha. Bantu bale banaripandishaka, abaonake bengine kuwa ba maana. Abekalake bien na benzabo nju banaonaka asema bo beko ba maana sana kubapita, njo pale bantu abapendake kubachofea. Lakini Jeova yeye ashikalake vile! Yeye anarishushaka sana, njo maana anatulomba tumuchofee na tumwambie mambo ile iko natwangaisha mu akiri na mu roo yetu. (Soma Zaburi 62:8.) Sa vile baba ule eko na mapendo ashichokake kushikia mambo ile iko namwangaisha mutoto yake, Jeova na ye ashichokake kushikia maombi ya batumishi bake. Kusema tu bya kweri, anabalombaka ata basali kwake. Njo pale arianjikishaka mu Bible ma sala ya mingi ya batumishi bake. Ile inaonesha asema anapendaka sana tukuwe karibu naye. (Yos. 10:12-14; 1 Sa. 1:10-18) Lakini, saa moya tunezi kuwaza asema atuwezi kumuchofea Mungu nju tunamukoseaka sana. Kama tunakuwa na mawazo ya vile, tunezi kufanya nini?
Mutoto arivunja kinkopo kya fleur saa arianza kucheza. Sasa anaenda kumwespliké baba yake vile mambo irikuwa. Baba yake anafwatirisha vile Jeova anarishushaka saa eko namushikia mutoto yake (Angaria mu paragrafe 2)
3. Nju ya nini uko sire asema Jeova anapenda ushiache ata shiku moya kusali kwake?
3 Yesu ariletaka mufano ya mutoto mupotevu. Mu ile mufano arimufananishaka Jeova na baba wa mapendo. Mutoto wa ule baba arifanyaka mankosa ya mingi na ariwazaka asema baba yake ashiwezi tena kumupokelea mu famiye yake. Ule baba arifanyaka nini saa mutoto yake arirudiaka ku nyumba? Yesu arisemaka kama, saa tu baba yake arimuonaka, ariendaka mbio kumupokelea na furaa. (Lu. 15:17-20) Jeova eko sa ule baba. Saa tu anaona tunanza kusali kwake nju tunarishikia mubaya nju ya mankosa ile turifanya, mala moya anapendaka sana kutushikia. Ile inaonesha asema ata kama tushakumukosea Jeova na tunawaza asema atupashwe kumuchofea, tukuwe sire asema anatupenda na anapenda tushiache ata shiku moya kusali kwake. (Omb. 3:19, 20) Jeova anatushikiriaka buluma sana, njo pale anakuyaka mbio kutupokelea nju ya kutupachia nguvu na kutufanya tukuwe sire asema anaturumia na anatupenda. (Isa. 57:15) Leo, Jeova anakuyaka je mbio nju ya kutupokelea? Mala mingi anatumikishaka bazee, bantu ba mu famiye yetu bale ni bakristo, na bakristo bengine nju ya kutusaidia. (Yak. 5:14, 15) Kama Jeova anafanyaka vile, ni nju anapenda tukuwe karibu naye.
4. Yesu arionesha je asema aripenda bantu bamuchofee?
4 Yesu arimufwatirisha Baba yake. Yesu anarishushaka sa tu Baba yake. Njo pale, saa arikuwa pa dunia, bantu barianzaka kupenda kumuchofea. Abakwanzake kushikia boka kumuuliza maulizo. (Mk. 4:10, 11) Njo pale saa arianzaka kubauliza mawazo yabo, barianzaka kumwambia waji-waji mambo ile barikuwaka nayo ku roo. (Mt. 16:13-16) Na saa barianzaka kufanya mankosa, abakwanzake kuongopa asema Yesu atabashirikia, nju bariyuwaka asema Yesu arikuwa muntu muzuri, arikuwa na buluma, na arikuwa muvumilivu. (Mt. 17:24-27) Nju Yesu arianzaka kumufwatirisha Baba yake, ile irisaidia banafunzi bake bafikie kumuyuwa Jeova muzuri sana. (Yoh. 14:9) Barifikia kuvumbula asema Jeova anarishushaka na anapendaka bantu bakuwe karibu naye. Ashikalake sa bashefu ba makanisa ba mu wakati ya Yesu bale barikuwaka ba makari, ba kuripandisha, na bale bantu abakwanzake kuchofea.
5. Kama tunarishusha, ile itafanya je bantu batuchofee?
5 Tunezi kumufwatirisha je Jeova? Kama tunafanya nguvu nju ya kuwa bantu ba kurishusha, bantu batapenda kutuchofea. Kama atuna bantu ba kurishusha tunezi kwanza kutamania bengine, kuwaza asema tuko ba maana kubapita, na tunezi ata kushinda kubarumia kama banatukosea. Kama tunakuwa vile, bantu batashinda kwanza kutuchofea. Lakini kama tunarishusha, tutatendea bengine muzuri, tutabavumilia, na tutabarumia kama banatukosea. Tukifanye vile, bengine batapenda kutuchofea. (Kol. 3:12-14) Surtout bazee banapashwa kufanya nguvu yabo yote nju banduku na badada mu kutaniko bashanze kushikia boka kubachofea. Na nju banduku na badada babachofee, bazee banapashwa kuwa karibu nabo. Njo maana kila wakati ile inawezekana, bazee banapashwa kufanya nguvu yabo yote nju ya kukutana na banduku na badada yabo ku Salle du Royaume nju ya kufwata marenion kuriko kuifwatia ku vidéoconférence. Na kila wakati inawezekana, banapashwa kufanya nguvu yabo yote nju ya kufanya maubiri ya nyumba na nyumba pamoya na banduku na badada yabo. Kama banduku na badada banakuwa karibu sana na bazee, itakuwa teketeke kwabo kubaambia mambo ile beko nayo ku roo saa yoyote ile banapenda kufanya vile.
JEOVA ANEKALAKA TAYARI KUSHANJÉ DESIZION YAKE
6-7. Leta mifano ile inaonesha asema Jeova anekalaka tayari kushikia batumishi bake na kushanjé desizion yake.
6 Bantu ba mingi bale banaripandishaka, banawazaka asema bo njo banayuwa byote na banawazaka asema abezi kushanjé desizion yabo. Kile bashakusema njo paka kile. Lakini Jeova ye ashikalake vile. Ata kama anayuwa byote, anarishushaka. Njo pale, anekalaka tayari kushikia mawazo ya bengine na kushanjé desizion ile ashakubeba. Kwa mufano, Miriam na nduku yake Aaron barianzaka kumusema Moïse mubaya. Barifanyaka mubaya sana nju mambo ile Moïse arianzaka kusema irianzaka kutoka kwa Jeova. Mambo ile Miriam arifanyaka irikuwa sa kumukosea Jeova eshima. Njo pale, Jeova arimushirikiaka sana Miriam na arimupika malari ya bukoma. Lakini saa Moïse na Aaron barimuriria Jeova nju aponeshe dada yabo, Jeova arifanya je? Mungu ashikuseme: ‘Kile nishakusema njo paka kile.’ Nju Jeova anarishushaka, arimushikia Moïse na arimuponesha Miriam.—Hes. 12:1-15.
7 Tena, namna Jeova arimutendea Hezekia inaonesha asema anarishushaka. Jeova aritumikisha profete wake nju ya kumuonesha Hezekia asema atakufa. Hezekia arimuriria sana Jeova na arimulomba amuponesheko. Jeova arifanya nini? Arimushikiria buluma na arimuongezea miaka ingine 15. (2 Fa. 20:1, 5, 6) Jeova anarishushaka sana, njo pale anashikiriaka bantu buluma na anekalaka tayari kubashikia na kushanjé desizion yake.
8. Leta mifano ile inaonesha asema Yesu anamufwatirishaka Baba yake? (Marko 3:1-6)
8 Yesu anamufwatirishaka Baba yake. Saa arikuwa pa dunia, Yesu ashikwanze kukatala kufanshia bantu bintu bizuri saa irilomba kufanya vile. Kwa mufano, Yesu ariponeshaka bantu shiku ya sabato ata kama bashefu ba makanisa ba ile wakati barianzaka kuwaza asema aina muzuri kufanya vile. (Soma Marko 3:1-6.) Yesu ashikalake na roo mubaya, lakini anekalaka na buluma na anariwekaka pa fashi ya bantu. Anatendeaka bakristo mu makutaniko na buluma na anariwekaka pa fashi yabo. Kwa mufano, kama muntu mu kutaniko anafanya nzambi ya nguvu sana, Yesu anamuvumiliaka na anamupachiaka ma okazion ya kushanjé.—Ufu. 2:2-5.
9. Tunezi kuonesha je asema tuko namufwatirisha Jeova? (Angaria na mafoto.)
9 Namna kani tunezi kumufwatirisha Jeova? Tunapashwa kufanya nguvu yetu yote nju ya kufwatirisha namna Jeova anawazaka na namna anatendaka. (Yak. 3:17) Kwa mufano, bazazi bale banamufwatirishaka Jeova abalombake batoto yabo bafanye mambo ile abataweza kufanya. Sa vile Mwanzo 33:12-14 inaonesha, Yakobo ariachiaka bazazi mufano muzuri mu ile mambo. Na ile ni mufano muzuri ku bazazi. Bazazi bale banarishushaka na kumufwatirisha Jeova abekalake nakomparé mutoto na mutoto mwingine. Bazee na bo banapashwa kumufwatirisha Jeova. Kwa mufano, muzee ashipashwe kukankamana paka na mawazo yake kama bazee bengine banabeba desizion ya kwachana na yake, na kama ile desizion ayende mpembeni na makanuni ya Jeova. (1 Ti. 3:2, 3) Na ata kama mawazo yetu inachana na ya bengine, shiye bote tunapashwa kufanya nguvu yetu yote nju tuone mambo vile bengine beko naiona. (Ro. 14:1) Njo maana, kila muntu mu kutaniko anapashwa kufanya nguvu yake yote nju bantu bote bayuwe asema ashikalake muntu wa kupenda bantu bafwate paka bile yeye anapenda.—Flp. 4:5.
Baba eko mu maubiri na mutoto yake. Lakini ashimulombe afanye mambo ile ashitaweza (Angaria paragrafe 9)
JEOVA NI MUVUMILIVU
10. Jeova arionesha je asema anekalaka muvumilivu?
10 Pengine na weye ushakuonaka asema bantu bale banekalaka na kiburi abapendake kubachungisha. Kiburi kinabafanyaka bashinde kuwa bavumilivu. Lakini Jeova yeye ashikalake vile. Mu mambo ya kuvumilia akuna ule anamupita! Kwa mufano mu wakati ya Noé, Jeova arisemaka kama atachunga miaka 120 ipite mbele, njo auwe bantu babaya. (Mwa. 6:3) Ile irimusaidia Noé aweze kukomesha batoto, na bale batoto pamoya na mama yabo bamusaidie Noé kuyenga safina. Kisha, Jeova arionesha uvumilivu saa Abraham arianza kumuuliza maulizo kisha kushikia asema Jeova aripenda kwalabisha Sodome na Gomorrhe. Muntu wa kiburi aripashwaka kusema ivi: ‘Weye uko nani nju uniulize ile maulizo yote!’ Lakini nju Jeova anarishushaka, arimuvumilia Abraham.—Mwa. 18:20-33.
11. Sa vile 2 Petro 3:9 inaonesha, nju ya nini Jeova eko naendelea kuchunga?
11 Ata leo Jeova eko naendelea tu kuonesha uvumilivu. Eko nachunga wakati ile ariweka ifike nju alete mwisho. Nju ya nini eko nachunga? “Nju ashipende ata muntu moya apotee. Lakini anapenda bantu bote bafikie kutubu.” (Soma 2 Petro 3:9.) Jeova eko nafanya mubaya kuchunga? Apana! Nju eko nachunga, bantu ba mingi bashakuwa barafiki yake. Na tuko sire asema bantu bengine ba mingi batafanya vile. Lakini uvumilivu ya Jeova iko na mwisho. Jeova anapendaka bantu, lakini ashitabacha baendelee kufanya byote bile banapenda. Ashitacha bantu babaya baendelee milele.—Hab. 2:3.
12. Yesu anafwatirishaka je uvumilivu ya Jeova?
12 Yesu anamufwatirishaka Baba yake. Yesu anafwatirishaka uvumilivu ya Baba yake. Arianzaka kufanya vile tangu nzamani. Mu miaka mingi, Yesu ariona vile Shetani arimulandia Jeova mambo ya bongo, na eko naendelea kuona vile Shetani eko naendelea kulandia batumishi baminifu ba Jeova mambo ya bongo tii na leo. (Mwa. 3:4, 5; Yob. 1:11; Ufu. 12:10) Tena, Yesu ashakurionea vile bantu beko nateswa sana mu dunia. Wazia vile eko nachunga na amu sana “kwalabisha kaji ya Shetani”! (1 Yo. 3:8) Ni nini njo iko namusaidia Yesu aendelee kuchunga Jeova amuoneshe asema ‘wakati inaenea sasa ya kwalabisha mambo yote ile Shetani ashakufanya’? Kintu kimoya kile kinamusaidiaka Yesu ni kurishusha. Anayuwa asema ni Jeova tu njo anapashwa kudesidé wakati ile ataleta mwisho.—Mdo. 1:7.
13. Namna kani Yesu arivumilia ba mitume bake, na nju ya nini arifanya vile?
13 Saa Yesu arikuwa pa dunia, arianzaka kuvumilia sana ba mitume bake. Kwa mufano, saa ba mitume barianzaka kubishana sana nju ya kuyuwa ni nani arikuwa mukubwa, Yesu ashikubachokake na kuwaza asema abezi kushanjé. Lakini ariendelea kubavumilia. (Lu. 9:46; 22:24-27) Ariyuwa tu asema ku mwenda-mashiku batafikia tu paka kushanjé. Bishakukufikiaka na weye kufanya nkosa moya-moya mala na mala? Kama ni vile, unarishikia je kuyuwa asema Yesu, Mufalme wako, anarishushaka na anekalaka muvumilivu?
14. Ni nini njo itatusaidia twendelee kuvumilia bengine?
14 Tunezi kumufwatirisha je Jeova? Nju ya kufwatirisha namna Jeova anawazaka na kutenda, tunapashwa kufunda vile Yesu anawazaka na kutenda. (1 Ko. 2:16) Sasa ni nini njo inezi kutusadia? Pashipo kwenda uku na uku, kya kufanya tu ni kusoma abari ya Yesu ile iko mu kitabu kya Matayo, Marko, Luka, na Yohana. Njo maana kisha kusoma abari nju ya maisha ya Yesu, tunapashwa kuwaza sana nju ya mambo ile Yesu arifanya na kutafuta kuyuwa kile kirimusukuma kuifanya. Kusema tu bya kweri, atutaweza kufanya ile mambo shiye benyewe. Njo maana, tunapashwa kumulomba Jeova atusaidie twanze kurishusha na tukuwe bavumilivu sa vile Yesu. Vile tutaendelea kumufwatirisha Yesu, njo vile tutafikia na kumufwatirisha Jeova, na ile itatusaidia turivumilie shiye benyewe na twendelee kuvumilia banduku na badada yetu.—Mt. 18:26-30, 35.
JEOVA ANAONAKA BANTU BA NIVO YA CHINI
15. Leta mifano ile inaonesha asema Jeova anaonaka bantu ba nivo ya chini kuwa ba maana?
15 Soma Zaburi 138:6. Jeova anekalaka yulu ya bintu byote, lakini anaonaka ata bantu ba nivo ya chini! Kwa mufano, kuko bantu ba mingi bale bengine barianzaka kuona sa ba bule, lakini Jeova ye arianzaka kubaona ba maana. Inawezekana bengine atubayuwe ata muzuri, lakini Jeova arianjikisha abari yabo mu Bible. Kwa mufano, Jeova arisukumaka Moïse anjike abari ya Déborah, mwanamuke ule aritumikiaka famiye ya Isaac na Jacob mu miaka 125! Ata kama bantu ba mingi abamuyuwe ule mwanamuke, Jeova arifanya nguvu yake yote nju Moïse ashikose kwanjika abari nju ya ule mwanamuke Jeova aripendaka sana. (Mwa. 24:59; 35:8) Na miaka mingi kisha pale, Jeova arimuchakulaka David, mutoto kiloko tu ule arianzaka kuchunga bankondolo, nju akuwe mufalme wa Israel. (2 Sa. 22:1, 36) Kisha tu Yesu kuzarika, Jeova arituma bamalaika bake baoneshe banaume bale barianzaka tu kuchunga bankondolo asema Masiya anazarika mu Bethléem. Ile irikuwa kubapachia eshima sana nju bo njo barikuwaka ba kwanza kupata ile abari. (Lu. 2:8-11) Na saa Joseph na Maria barimupelekaka Yesu ku tample, Jeova arifanyaka Siméon na Anne bapate okazion ya kumuona Yesu, mutoto wa Mungu. (Lu. 2:25-30, 36-38) Ile yote inaonesha asema, “ata kama Jeova eko yulu, anaonaka muntu wa nivo ya chini”!
16. Yesu arifwatirisha je namna ile Baba yake anatendeaka bantu?
16 Yesu anamufwatirishaka Baba yake. Sa tu Baba yake, Yesu arianzaka kweshimia sana bantu ba nivo ya chini. Arianzaka kufundisha bantu ‘bale abakufunde sana na bale barikuwa tu sa bantu bote’ kweri nju ya ufalme ya Mungu. (Mdo. 4:13; Mt. 11:25) Tena, Yesu ariponesha ba malari na aribatendea mu namna ile inaonesha asema anabapenda na anabaeshimia. (Lu. 5:13) Na bushiku bwa mwisho mbele akufwe, Yesu aririshushaka sana na arinawishaka mikulu ya banafunzi bake. (Yoh. 13:5) Tena, mbele apande ku mbingu, Yesu arionaka banafunzi bake bote ba mu wakati ya nzamani na ba mu wakati ya leo kuwa bantu ba valere. Arifanyaka vile saa aribapachiaka kaji ya lazima kupita yote, ni kusema, kaji ya kusaidia bantu ba mingi bapate bujima bwa milele.—Mt. 28:19, 20.
17. Tutaonesha je asema tunapenda na kweshimia bengine? (Angaria na foto.)
17 Tutamufwatirisha je Jeova? Tutaonesha asema tunapenda bantu na kubaeshimia saa tunabaubiria abari njema pashipo kwangaria kule banatoka, rangi ya ngoji yabo, ao bwingi bwa masomo ile barifunda. Na tunaonesha asema tunapenda na kweshimia sana banduku na badada yetu saa tunabaona kuwa ba maana kutupita, ata kama tunafanyaka mambo muzuri kubapita ao ata kama tuko na madaraka mu kutaniko ile bo abana nayo. (Flp. 2:3) Kama tunatumikisha mambo ile tunafunda na kama tunafanya mambo ingine nju ya kuonesha kama tunarishusha, tunapenda banduku na badada yetu, na tunabaeshimia, Jeova atashikia furaa sana.—Ro. 12:10; Sef. 3:12.
Tunafwatirisha vile Jeova anarishushaka saa tunaubiria bantu ba namna yote abari njema (Angaria paragrafe 17)a
18. Nju ya nini unapenda kufwatirisha vile Jeova anarishushaka?
18 Kama tunafanya nguvu yetu yote nju ya kufwatirisha vile Baba yetu wa ku mbingu anarishushaka, itakuwa teketeke bantu batuchofee, tutakuwa tayari kushanjé madesizion yetu kama inalomba kufanya vile, tutakuwa bavumilivu sana, na tutapenda na kweshimia bengine sa vile Jeova anafanyaka. Na tukumbuke asema, kama tunafanya nguvu yetu yote nju ya kufwatirisha namna Jeova anarishushaka, Jeova ataendelea kutuona kuwa ba lazima sana!—Isa. 43:4.
MWIMBO 159 Jeova merci
a ESPLIKASION YA FOTO: Badada beko nafwatirisha vile Jeova anarishushaka saa beko naubiria banamuke bale beko mu prizon.