BIBLIOTEKE YA KU ENTERNETE Watchtower
Watchtower
BIBLIOTEKE YA KU ENTERNETE
Swahili (Katanga)
  • BIBLE
  • BITABU
  • MA RENION
  • w25 Décembre pp. 20-25
  • Namna ya kutayarisha mariage ile itamuletea Jeova eshima

Akuna video nju ya iyi selection.

Pardon, kurikuwa erreur mu chargement ya video.

  • Namna ya kutayarisha mariage ile itamuletea Jeova eshima
  • Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
  • Sous-titres
  • NJU YA NINI MUNAPASHWA KUMULETEA JEOVA ESHIMA?
  • MUNEZI KUFANYA NINI NJU MUMULETEE JEOVA ESHIMA?
  • NAMNA YA KWEPUKA MAGUMU
Munara ya Mulinzi Inatangaza Ufalme ya Jeova (ya kufunda)—2025
w25 Décembre pp. 20-25

ABARI YA KUFUNDA YA 51

MWIMBO 132 Sasa Tunakuwa Mwili Mumoja

Namna ya kutayarisha mariage ile itamuletea Jeova eshima

“Lakini mambo yote ifanshike na adabu na ordre.”​—1 KO. 14:40.

MU KIFUPI

Mambo ile bale banapenda kuowana banezi kufanya nju ya kumuletea Jeova eshima shiku ya mariage yabo.

1-2. Jeova anaonaka je mariage?

ESKE uko fiancé? Kama uko fiancé, félicitation! Pengine iyi mashiku uko na bya mingi bya kufanya nju ya kutayarisha mariage. Jeova anapenda shiku ya mariagea yako ipite muzuri. Anapenda ufuraie ile shiku na anapenda mweye bote bawiri mukuwe na furaa mu maisha yenu yote.​—Mez. 5:18; Wim. 3:11.

2 Munapashwa kufanya yenu yote nju mumuletee Jeova eshima shiku ya mariage yenu. Nju ya nini tunasema vile? Na munezi kufanya nini nju ya kumuletea eshima? Iyi abari bariitayarisha mbele nju ya bale beko natayarisha mariage yabo. Lakini, inezi kutusaidia shiye bote tumuletee Jeova eshima kama banatwita ku mariage ao kama banatulomba mashauri nju ya namna ya kutayarisha mariage.

NJU YA NINI MUNAPASHWA KUMULETEA JEOVA ESHIMA?

3. Bakristo bawiri bale beko natayarisha mariage yabo banapashwa kufanya nini?

3 Bakristo bawiri bale banapenda kuowana banapashwa kufwata makanuni ya Jeova saa beko natayarisha mariage yabo. Nju ya nini? Nju Jeova njo arianzishaka mariage. Ye njo arifanyaka Adam na Eve bakuwe ba bibi na bwana. (Mwa. 1:28; 2:24) Nju Jeova njo arianzishaka mariage, bantu bawiri bale banapenda kuowana banapashwa kufanya nguvu yabo yote nju ya kumuletea eshima.

4. Ni rezon kani ingine ile inezi kusukuma bale banapenda kuowana bamuletee Jeova eshima shiku ya mariage yabo?

4 Rezon munene ile itamisaidia mukuwe na mawazo ya Jehova saa muko natayarisha mariage yenu ni iyi: Jeova ni Baba yenu wa ku mbingu na ni rafiki yenu wa karibu sana. (Ebr. 12:9) Kusema tu bya kweri, munapenda kuwa na burafiki bwa karibu pamoya naye, na amupende ata kintu kimoya kibaya kifanshike shiku ya mariage yenu, kile kitamufanya rafiki yenu wa karibu sana ashikie mubaya. (Zb. 25:14) Saa munawaza nju ya mambo ile Jeova ashakumifanshia na ile atamifanshia uku ku mbele, amuone kama ni muzuri mufanye mariage ile itamuletea eshima?​—Zb. 116:12.

MUNEZI KUFANYA NINI NJU MUMULETEE JEOVA ESHIMA?

5. Bible inezi kusaidia je bale beko natayarisha mariage babebe madesizion ya muzuri?

5 Bible aitupachie liste ya mambo ile bale banapenda kufanya mariage banapashwa kufwata, ao ni feti ya je banapashwa kufanya. Njo pale, bale beko napenda kuowana beko libre kutayarisha mariage yabo kupatana na sitwasion ile bekwamo, mambo ile inafanshikaka kule beko naishi, na kupatana na mambo ile banapenda. Tena, bakristo ba bya kweri banapashwa kutii mambo ile sheria ya guvernema inasema nju ya mariage. (Mt. 22:21) Lakini madesizion yote ile bale beko napenda kufanya mariage batabeba inapashwa kupatana na makanuni ya mu Bible. Ile itamuletea Jeova eshima na itamufuraisha. Sasa ni makanuni kani ile munapashwa kuchunga mu akiri?

6. Nju ya nini bantu bawiri bale banapenda kuowana banapashwa kufwata masheria ya guvernema nju ya mariage?

6 Mufwate masheria ya guvernema. (Ro. 13:1, 2) Mu ma pays ingine, guvernema inekalaka na masheria ile bale banapenda kuowana banapashwa kufwata. Bale banapenda kuowana banapashwa kuyuwa muzuri masheria ya fashi kule beko nekala. Kama uko na maulizo nju ya ile masheria ushikose kuuliza bazee.b

7. Mariage ya bakristo inapashwa kufanshika je?

7 Mufanye nguvu nju mambo ipite muzuri. (1 Ko. 10:31, 32) Mufanye nguvu nju mariage yenu ishipite sa ya bantu ba mu dunia, lakini ifanshike sa ya bantu bale beko naonesha masifa ya ntunda ya roo ya Mungu. (Gal. 5:19-26) Nju bwana njo atakuwa shefu wa famiye, ni ye njo wa kufanya yake yote nju mariage ipite muzuri na imuletee Jeova eshima. Ni nini njo inezi kufanya mariage ipite muzuri? Ni diskur ya mariage ile banafanya na eshima na mapendo na kivukutu. Nju ile itasaidia bantu bakomprandre asema mariage ni kado ile inatoka kwa Jeova. Na bale batakuwa ku ile diskur batakomprandre asema mariage ni kintu kimoya kya maana sana. Tena, bakristo ba mingi banapendaka babafanshie diskur ku salle du royaume. Kama inawezekana na kama banapenda, banapashwa kwanjikia bazee mukanda mbele ya wakati nju ya kulomba salle du royaume.

8. Ni mambo kani ile inezi kusaidia feti ya mariage ipite muzuri? (Waroma 13:13)

8 Soma Waroma 13:13. Kama mutafanya feti ya mariage, munezi kufanya nini nju ishikuwe sa ya bantu ba mu dunia? Mu kigrek, misemo “mafeti ya kupita kipimo” ni mafeti mule bantu banakunywaka sana na mule munekalaka miziki ya kwenda tii paka na bushiku sana. (Angaria “fêtes débridées” mu notes d’études ya mu Bible d’étude ya français pa Waroma 13:13.) Kama mutapachia bantu mpombe ku feti yenu ya mariage, muwaze kile mutafanya mbele ya wakati nju ata muntu moya ashikunywe sana.c Kama mutaweka miziki, mufanye nguvu nju volume ya miziki yenu ishikuwe yulu sana ifanye bantu bashinde kusumburia. Tena mujiulize ivi : Ni miziki ya je njo tutaweka, na iko na misemo kani? Mufanye nguvu yenu yote nju miziki ile mutaweka ishikwaze bengine.

9. Kama kutakuwa bya kusema ao mambo ingine ya kujifuraisha, bale beko naowana banapashwa kufanya nini?

9 Mu mafashi ingine, pa feti ya mariage banapachiaka sauti bantu ba mu famiye ya bwana ao ya bibi ao barafiki nju basemeko mambo fulani nju ya bale beko naowana. Na mu mafashi ingine, banaoneshaka video ao mafoto ya bale beko naowana ao kintu kingine nju ya kufuraisha. Bile bintu binezi kufanya tena feti ikuwe muzuri sana. Lakini, mufanye nguvu nju ile mambo yote ikuwe ya kujenga. (Flp. 4:8) Mujiulize ivi: ‘Eske ile mambo yote italetea bengine eshima? Itafanya mariage ionekane sa kintu kya valere?’ Na ulizo ya lazima sana ni iyi: ‘Eske itamuletea Jeova eshima?’ Kama mutasema ao kufanya mambo ya kuchekesha, ishikuwe ya kushushia bantu eshima ao ile itafanya baanze kuwaza nju ya busharati. (Efe. 5:3) Kama bantu ba mu famiye yenu ao barafiki yenu batakuwa na kya kusema, mubaoneshe waji-waji mambo ile abapashwe kusema.

10. Nju ya nini bibi na bwana abapashwe kupanga feti ya mariage ile itafanya barioneshe? (1 Yo. 2:15-17)

10 Mushifanye mambo nju ya kurionesha. (Soma 1 Yohana 2:15-17.) Jeova ashipendake kama batumishi bake bananza kurionesha, kuriko kumuletea yeye eshima. Njo pale, bakristo abapashwe kutumikisha makuta ya mingi sana nju tu ya kupenda ‘kurionesha.’ Kama munafanya tu feti ile iko simple, ile itamisaidia je? Nduku Mike wa mu Norvège anasema ivi: “Kisha feti, atukubakie na mandeni na turiweza kwendelesha kaji ya bu painia. Mariage yetu irikuwaka simple, lakini iripitaka muzuri na turibakiaka na ma souvenir ya muzuri.” Dada Tabitha wa mu Inde, na ye anasema ivi: “Nju feti yetu irikuwaka simple, atukwangaikake sana. Atukukuwe na bintu bya mingi bya kupanga, na ile irifanya nishikosane na fiancé wangu, na bantu ba mu mafamiye yetu.”

Mafoto: Mu dunia yote, banduku na badada beko nafurai ku mafeti ya marriage. 1. Bibi na bwana bashakwikala ku mbele ya nduku ule eko nabafanshia diskur mu salle du royaume. 2. Bibi na bwana beko na félicité bale beko nafanshia feti yabo ya mariage inje. 3. Bibi na bwana bashakuripanga mu mustari na beko nabeba byakurya pamoya na bantu bale bariita ku feti yabo. 4. Bibi na bwana bashakushimama inje ku mbele ya nduku ule eko nabafanshia diskur ya mariage.

Ata kama beko naishi wapi, Mariage ya bakristo inezi kuwa ya muzuri, yashipo mambo mingi, na ile bantu batakumbuka na furaa (Angaria paragrafe 10 na 11)


11. Bale banapenda kuowana, abapashwe kusabu nini saa beko napanga bile batavwala na vile bataonekana? (Angaria na mafoto.)

11 Mushakudesidé nju ya manguo ile mutavwala? Kusema tu bya kweri, ile shiku mutapendaka kuvwala muzuri sana. Na aina mubaya. Ata mu wakati ya nzamani bibi na bwana barianzaka kwangaikia sana manguo ile batavwala na vile bataonekana. (Isa. 61:10) Kusema tu bya kweri, manguo ile utavwala shiku ya mariage yako itachana sana na ile unavwalaka kila shiku. Lakini aipashwe kuwa manguo ya kurionesha ao ya kukwaza bengine. (1 Ti. 2:9) Ushiache manguo ile utavwala ao vile utaonekana njo bikuwe bintu bya lazima sana bya mariage yako.​—1 Pe. 3:3, 4.

12. Nju ya nini bale banapenda kuowana banapashwa kwepuka sana ma coutume ya bapagani?

12 Achana na ma coutume ao madesturi ya bapagani. (Ufu. 18:4) Leo, ku mafeti mingi ya mariage, mala mingi kunafanshikaka mambo ile inapatana na mafundisho ya makanisa ya bongo na mambo ya buloji. Jeova anatukataza sana tushiringishe mu ile mambo ya buchafu. (2 Ko. 6:14-17) Kama uko na ma doute nju ya coutume fulani ile inafanshikaka kule uko naishi, fanya ma recherche nju ya kuyuwa vile ile coutume irianzaka na utafute makanuni ya mu Bible ile itakusaidia uyuwe kama utaingisha ile coutume mu feti yako ya mariage ao apana.

13. Bale beko nafanya mariage banezi kumufwatirisha je Jeova saa bengine banapenda kubapachia makado?

13 Eske fashi kule uko naishi bantu banekalaka na zoezi ya kupachia bale beko nafanya mariage makado? Muntu analetaka kado kupatana na bwingi bwa makuta ile eko nayo. Ata vile, Bible inankurajé bakristo kupachia bengine. Na kufanya vile kunabaleteaka furaa. (Mez. 11:25; Mdo. 20:35) Lakini, bale beko nafanya mariage abapashwe kufanya ba invité babo bawaze kama banapashwa tu kubapachia makado, ao kubafanya bajishikie mubaya nju abakubapachie kado ya bei. Jeova anafuraiaka saa muntu anatoa na roo yake yote. Bale beko nafanya mariage banapashwa kumufwatirisha Jeova. Banapashwa kufuraia makado ile bengine banabapachia na roo moya, apana nju baripashwa kufanya vile.​—2 Ko. 9:7.

NAMNA YA KWEPUKA MAGUMU

14. Bale beko natayarisha mariage banapataka magumu kani?

14 Munezi kupata magumu saa unapenda kufanya mariage ile itamuletea Jeova eshima. Kwa mufano, binezi kuwa nguvu kwenu kutayarisha mariage ile ailombe mambo ya mingi. Nduku Charlie, wa mu Îles Salomon, anasema ivi: “Birikuwa nguvu sana kudesidé ni nani njo tutaita ku feti. Turikuwa na barafiki ba mingi, na mu culture yetu kila muntu anapendaka bamwite ku feti!” Dada Tabitha ule turitaya, anasema ivi: “Fashi kule niko naishi, bantu banazobeleaka kufanya mafeti ya munene sana. Irilomba wakati nju bazazi baichike desizion ile turibeba ya kwita tu bantu kiloko.” Dada Sarah wa mu Inde, anasema ivi: “Bantu bengine banapendaka kufanya mariage ya munene nju ya kurionesha. Ba cousin bangu barifanyaka ma mariage ya munene sana. Na miye mirionaka asema minapashwa kufanya ya munene kupita na pale.” Ni nini inezi kumisaidia kwepuka ile magumu na magumu ingine?

15. Nju ya nini ni muzuri sana kusali saa muko natayarisha mariage?

15 Mushikose kusali kwa Jeova. Munezi kumwambia Jeova mu sala nju ya desizion yoyote ile munapenda kubeba ao nju ya vile muko narishikia saa muko natayarisha mariage yenu. (Flp. 4:6, 7) Munezi kumulomba amisaidie mubebe madesizion ya muzuri, mutulizane saa muko na mangaiko, na mukuwe na nguvu saa inalomba kubeba desizion ile inachana na ya bengine. (1 Pe. 5:7) Saa muko naona vile Jeova eko najibu sala yenu, ile itamisaidia mwendelee kumutumainia. Dada Tabitha ule turitaya anasema ivi: “Miye na fiancé wangu turianza kuongopa kukosana ao kukosana na bantu ba mu mafamiye yetu. Njo maana, kila wakati turianza kutayarisha mariage yetu, turianza mbele kufanya sala. Turiona vile Jeova aritusaidia. Turifurai nju miye na fiancé wangu atukukosane, na tena atukukosane na bantu ba mu mafamiye yetu.”

16-17. Kusumburia waji-waji na eshima kutamisaidia je saa muko napanga feti ya mariage?

16 Musumburie waji-waji na eshima. (Mez. 15:22) Saa vile mutaoana, muko na lazima ya kubeba madesizion ya mingi nju ya mariage yenu. Mutabeba desizion nju ya date ya mariage yenu, bwingi bwa makuta ile mutatumikisha, liste ya bantu bale mutaita ku feti, na mambo ingine ya mingi. Mbele ya kubeba desizion, murudirie mambo ile muripanga pamoya, na muone ni makanuni kani ya mu Bible ile mutatumikisha, na mashauri ya banduku na badada bale bashakukomea kiroo ile munezi kutumikisha. Saa muko nasumburia na bantu ba mu mafamiye yenu nju ya mambo ile muripenda kufanya, mukuwe na eshima na mukuwe tayari kwichika mawazo yabo kama inalomba kufanya vile. Kwa mufano, kama bazazi yenu banalomba muongezeko mambo ingine ile inaonekana kuwa ya muzuri saa muko natayarisha mariage yenu, mupime kufanya vile barilomba. Ile ni okazion ya muzuri sana kwabo ya kuleta mawazo ile beko nayo. Kama amutafanya bile barimilomba, mubaoneshe na eshima nju ya nini amutafanya vile. (Kol. 4:6) Muoneshe waji-waji bantu ba mu famiye yenu asema munapenda mariage yenu ikuwe ya furaa na imuletee Jeova eshima.

17 Abikalake teketeke kwambia bazazi nju ya madesizion yenu surtout kama abana Batemwe, lakini mutaweza kufanya vile. Nduku Santhosh wa mu Inde anasema ivi: “Mafamiye yetu iripendaka twingishe ma coutume ya kwachana-achana ya ba Hindu mu feti yetu. Iritubeba wakati ya mingi miye na fiancée wangu nju tubaespliké nju ya nini atutengisha ile ma coutume mu feti ya mariage yetu. Lakini, turiichika kufanya bintu bingine bile baritulomba saa turiona asema abitamushirikisha Jeova. Kwa mufano, turishanjé byakurya bile turikuwa tushakupanga nju ya kuweka byakurya bile bitabafuraisha. Tena turidesidé kushikuwe miziki ao ma danse, nju bile bantu ba mu famiye yetu ababizobelee.”

18. Munezi kufanya nini nju shiku ya mariage yenu ipite muzuri? (1 Wakorinto 14:40) (Angaria na foto.)

18 Mutayarishe bintu muzuri. Kama munatayarisha bintu muzuri, ile itamisaidia mushangaike sana shiku ya mariage. (Soma 1 Wakorinto 14:40.) Nduku Wayne, wa mu Taïwan, anasema ivi: “Mashiku kiloko mbele ya mariage yetu, turifanya ka renion na bantu bale baripashwa kutusaidia mu makaji ya kwachana-achana. Turisumburia nju ya vile mambo itakuwa, na turifanya ka repetision kaloko nju ya kuwa sire asema mambo yote itapita muzuri.” Nju ya kuonesha asema muneshimia bantu bale muriita, mufanye nguvu yenu yote nju mweshimie wakati.

Ba fiancé beko nasumburia na barafiki yabo bale batabasaidia nju ya bile bashakupanga kufanya feti yabo ya mariage. Nduku ashakubeba tablete nju ya kuonesha vile batapanga bichi ku feti yabo ya mariage.

Kama munapanga bintu muzuri ile itasaidia mariage yenu ipite muzuri (Angaria paragrafe 18)


19. Munezi kufanya nini nju feti ya mariage yenu ipite vile muripanga?

19 Muwaze mbele ya wakati nju ya mambo ile inezi kutokea shiku ya mariage yenu na kile mutafanya. (Mez. 22:3) Kwa mufano, mu mafashi ingine, ata bantu bale amukwite banakuyaka ku feti. Muwaze mbele ya wakati kile munezi kufanya nju bya vile bishikuyeko. Mufanye nguvu yenu yote nju banduku yenu bale abana Batemwe bayuwe kile munezi kupenda bafanye shiku ya feti yenu ya mariage, na musumburie nabo nju ya ma coutume ile amutapenda ikuwe mu feti yenu ya mariage. Munezi kubatumia artikle “Ndoa ya Mashahidi wa Yehova Inakuwaka Namna Gani?” ile iko ku jw.org. Muchakule nduku ule eko na expérience na ule eko na ekima nju ‘ashimamie feti,’ na amisaidie mambo ipite muzuri vile muripenda. (Yoh. 2:8) Kama munamuonesha waji-waji vile muripanga bintu, anezi kumisaidia nju mariage yenu ipite muzuri na ipitikane vile muripanga.

20. Bantu bale banapenda kuowana banapashwa kukumbuka nini nju ya mariage?

20 Kama munawaza nju ya bintu byote bile munapashwa kufanya nju ya kupanga mariage yenu, saa moya binezi ata kumipitia. Lakini, mukumbuke ya kusema mariage ni ya shiku moya tu. Ni mwanzo tu ya maisha ya muzuri sana ya kumutumikia Jeova pamoya. Mufanye yenu yote nju mariage yenu ishikuwe na mambo mingi na imutukuze Jeova. Mumutumainie Jeova. Kama munafwata mashauri yake, mutaweza kupanga mariage yenu muzuri, na saa mutaanza kuikumbuka, amutauzunika ata nju ya kintu kimoya. Lakini mutakuwa tu na furaa nju iripitaka muzuri.​—Zb. 37:3, 4.

UTAJIBU JE?

  • Nju ya nini bantu bale banapenda kuowana banapashwa kumuletea Jeova eshima shiku ya mariage yabo?

  • Bantu bale banapenda kuowana banapashwa kufanya nini nju mariage yabo ipite muzuri na imuletee Jeova eshima?

  • Kama bale beko naowana banafanya mariage ile ailombe bintu bya mingi, ile itabasaidia je?

MWIMBO 107 Tuonyeshe Upendo Kama Mungu

a ESPLIKASION YA MISEMO INGINE: Mu ma culture ya mingi, shiku ya mariage kunekalaka diskur. Bantu bale beko naowana banavwarishanaka ma bague, banalapaka mbele ya Mungu ya kusema batekala pamoya maisha yabo yote. Na kisha kunezi kuwa feti. Lakini mu ma culture ingine bantu abafanyake bile byote. Ata vile, makanuni ile iko mu Bible inezi kubasaidia shiku ya mariage yabo.

b Kama unapenda kuyuwa mambo ya mingi nju ya vile bakristo banaonaka masheria ya guvernema nju ya mariage, angaria mu artikle “Des mariages honorables aux yeux de Dieu et des hommes” mu Munara ya Mulinzi ya français ya le 15 octobre 2006.

c Angaria video Nipatie Watu Pombe? ku jw.org.

    Swahili (Katanga) Publications (2020-2026)
    Toka
    Ingia
    • Swahili (Katanga)
    • Partajé
    • Preferanse
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni ya kutumikisha
    • Règles de confidentialité
    • Paramètres de confidentialité
    • JW.ORG
    • Ingia
    Partajé