-
Hesabu 7:6-9Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
6 Basi Musa akapokea magari hayo pamoja na ng’ombe na kuwapa Walawi. 7 Aliwapa wana wa Gershoni magari mawili na ng’ombe dume wanne kulingana na mahitaji ya kazi yao;+ 8 akawapa wana wa Merari magari manne na ng’ombe dume wanane kulingana na mahitaji ya kazi yao, chini ya usimamizi wa Ithamari mwana wa kuhani Haruni.+ 9 Lakini hakuwapa chochote wana wa Kohathi kwa sababu majukumu yao yalihusisha kutumikia mahali patakatifu,+ nao walibeba vitu vitakatifu mabegani.+
-
-
1 Mambo ya Nyakati 15:2Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
2 Huo ndio wakati ambao Daudi alisema: “Hakuna mtu yeyote anayepaswa kubeba Sanduku la Mungu wa kweli isipokuwa Walawi, kwa maana Yehova amewachagua ili walibebe Sanduku la Yehova na kumhudumia sikuzote.”+
-