-
Kutoka 22:20Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
20 “Mtu yeyote anayetoa dhabihu kwa miungu mingine isipokuwa kwa Yehova peke yake lazima auawe.+
-
-
Kutoka 32:25Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
25 Musa akaona kwamba watu wanafanya watakavyo, kwa sababu Haruni aliwaacha wafanye watakavyo, hivi kwamba wakajiletea aibu mbele ya wapinzani wao.
-
-
Kutoka 32:27Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
27 Basi Musa akawaambia: “Yehova Mungu wa Israeli amesema, ‘Kila mmoja wenu na ajifunge upanga wake na kupita kotekote kambini, kutoka lango mpaka lango, amuue ndugu yake, jirani yake, na rafiki yake wa karibu.’”+
-
-
Kumbukumbu la Torati 13:6-9Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
6 “Ikiwa ndugu yako, mwana wa mama yako, au mwana wako au binti yako au mke wako mpendwa au rafiki yako wa karibu sana* atajaribu kukushawishi kwa siri, akisema, ‘Twende tukaabudu miungu mingine,’+ miungu ambayo wewe wala mababu zako hamwijui, 7 kutoka miongoni mwa miungu ya mataifa yanayowazunguka, yaliyo karibu nanyi au mbali nanyi, kutoka mwisho mmoja wa nchi mpaka mwisho mwingine wa nchi, 8 usikubali ushawishi wake wala kumsikiliza,+ wala usimsikitikie wala kumhurumia wala kumlinda; 9 badala yake, ni lazima umuue.+ Mkono wako unapaswa kuwa wa kwanza kumuua, kisha mikono ya watu wote itafuata.+
-