-
Yoshua 23:6, 7Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
6 “Basi iweni jasiri sana mshike na kutekeleza mambo yote yaliyoandikwa katika kitabu cha Sheria+ ya Musa, msiiache kamwe na kwenda kulia wala kushoto,+ 7 na msishirikiane kamwe na mataifa haya+ yaliyobaki kati yenu. Hampaswi hata kutaja majina ya miungu yao+ wala kuapa kwa majina hayo, na hampaswi kamwe kuiabudu au kuiinamia.+
-
-
Yeremia 2:11Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
11 Je, taifa limewahi kubadili miungu yake kwa ajili ya miungu ambayo si miungu?
Lakini watu wangu mwenyewe wamebadili utukufu wangu kwa ajili ya kitu kisicho na maana.+
-
-
Yeremia 12:16Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
16 “Na wakihakikisha kwamba wanajifunza njia za watu wangu na kuapa kwa jina langu, ‘Kwa hakika kama Yehova anavyoishi!’ kama walivyowafundisha watu wangu kuapa kwa jina la Baali, ndipo watakapojengwa miongoni mwa watu wangu.
-
-
Sefania 1:4, 5Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
4 “Nitaunyoosha mkono wangu dhidi ya watu wa Yuda
Na dhidi ya wakaaji wote wa Yerusalemu,
Nami nitafutilia mbali kutoka mahali hapa kila kitu kinachohusiana na* Baali,+
Jina la makuhani wa miungu ya kigeni pamoja na makuhani wenyewe,+
5 Na wale wanaoliinamia jeshi la mbinguni wakiwa juu ya paa,+
Na wale wanaoinama chini na kuapa kwamba watakuwa washikamanifu kwa Yehova+
Na wakati uleule wakiapa kwamba watakuwa washikamanifu kwa Malkamu;+
-