Ayubu
34 Kwa hiyo, Elihu akaendelea kusema:
2 “Sikilizeni maneno yangu, ninyi mlio na hekima;
Nisikilizeni, ninyi mnaojua mambo mengi sana.
3 Kwa maana sikio hupima maneno
Kama ulimi unavyoonja* chakula.
4 Acheni tuchanganue wenyewe yaliyo sawa;
Acheni tuamue miongoni mwetu yaliyo mema.
6 Je, ninaweza kusema uwongo kuhusu hukumu ninayostahili?
Kidonda changu hakiponi, ingawa sina kosa.’+
7 Ni nani aliye kama Ayubu,
Anayekunywa dharau kama maji?
8 Yeye ni rafiki ya watenda dhambi
Naye hushirikiana na waovu.+
9 Kwa maana amesema, ‘Mwanadamu hafaidiki
Kwa kujitahidi kumpendeza Mungu.’+
10 Kwa hiyo nisikilizeni, ninyi watu wenye uelewaji:*
11 Kwa maana atamlipa mwanadamu kulingana na matendo yake+
Na kumletea matokeo ya njia zake.
13 Ni nani aliyempa mamlaka ya kusimamia dunia,
Na ni nani aliyemweka asimamie ulimwengu mzima?*
14 Akiwakazia fikira,*
Akijikusanyia roho yao na pumzi yao,+
15 Wanadamu wote wataangamia* pamoja,
Nao watarudi mavumbini.+
16 Basi ikiwa mna uelewaji, sikilizeni mambo haya;
Sikilizeni kwa makini ninayosema.
17 Je, mtu anayechukia haki anapaswa kuongoza,
Au je, mtamhukumu mwenye nguvu ambaye ni mwadilifu?
18 Je, mtamwambia mfalme, ‘Wewe hufai kitu,’
Au viongozi, ‘Ninyi ni waovu’?+
19 Kuna Yule asiyewapendelea wakuu
Na ambaye hawapendelei matajiri na kuwapuuza maskini,*+
Kwa maana wote ni kazi ya mikono yake.+
20 Wanaweza kufa ghafla,+ katikati ya usiku;+
Wanatikisika kwa nguvu na kufa;
Hata wenye nguvu huondolewa, lakini si kwa mikono ya wanadamu.+
21 Kwa maana macho ya Mungu hutazama njia za mwanadamu,+
Naye huziona hatua zake zote.
22 Hakuna giza wala kivuli kizito
Ambamo watenda maovu wanaweza kujificha.+
23 Kwa maana Mungu hajaweka wakati hususa wa mwanadamu yeyote
Kufika mbele zake ili ahukumiwe.
24 Huwapondaponda wenye nguvu bila kuhitaji kufanya uchunguzi
Na kuwaweka wengine mahali pao.+
26 Huwapiga kwa sababu ya uovu wao,
Mahali ambapo watu wote wanaweza kuona,+
27 Kwa sababu wameacha kumfuata+
Nao hawaheshimu yoyote kati ya njia zake;+
28 Wanasababisha maskini wamlilie,
Hivi kwamba anasikia kilio cha wasio na uwezo.+
29 Mungu akikaa kimya, ni nani anayeweza kumshutumu?
Akiuficha uso wake, ni nani anayeweza kumwona?
Iwe ni kwa taifa au mtu mmoja, matokeo ni yaleyale,
30 Ili mtu anayemkataa Mungu* asitawale+
Au kuwawekea wengine mitego.
31 Je, kuna yeyote anayeweza kumwambia Mungu,
‘Nimeadhibiwa, ingawa sijafanya kosa lolote;+
32 Nifundishe jambo ambalo nimeshindwa kuona;
Ikiwa nimetenda kosa lolote, sitalirudia tena’?
33 Je, akuthawabishe kwa masharti yako wakati unakataa hukumu yake?
Amua mwenyewe, si mimi.
Basi niambie mambo unayojua vema.
34 Watu wenye uelewaji* wataniambia
—Mtu yeyote mwenye hekima anayenisikiliza—
35 ‘Ayubu anazungumza bila ujuzi,+
Na maneno yake hayana ufahamu.’
36 Acha Ayubu ajaribiwe* kikamili
Kwa sababu majibu yake ni kama ya watu waovu!