Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 107
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Zaburi—Yaliyomo

      • Mshukuruni Mungu kwa sababu ya kazi zake zinazostaajabisha

        • Aliwaongoza katika njia inayofaa (7)

        • Aliwatosheleza wenye kiu na wenye njaa (9)

        • Aliwatoa gizani (14)

        • Alituma neno lake kuwaponya (20)

        • Huwalinda maskini ili wasikandamizwe (41)

Zaburi 107:1

Marejeo

  • +Lu 18:19
  • +1Nya 16:34; Zb 103:17

Zaburi 107:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “walionunuliwa.”

  • *

    Au “katika nguvu za.”

Marejeo

  • +Isa 35:10; Yer 15:21; Mik 4:10

Zaburi 107:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Kutoka mapambazuko ya jua na kutoka machweo ya jua.”

Marejeo

  • +Zb 106:47; Yer 29:14
  • +Isa 43:5, 6; Yer 31:8

Zaburi 107:6

Marejeo

  • +Ho. 5:14, 15
  • +Isa 41:17

Zaburi 107:7

Marejeo

  • +Isa 30:21
  • +Ne 11:3

Zaburi 107:8

Marejeo

  • +1Nya 16:8
  • +Zb 40:5

Zaburi 107:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “amezitosheleza nafsi zilizokauka.”

  • *

    Au “kuzishibisha nafsi zenye njaa.”

Marejeo

  • +Zb 34:10; Isa 55:2; Lu 1:53

Zaburi 107:11

Marejeo

  • +Zb 106:43; Omb 3:42

Zaburi 107:12

Marejeo

  • +Law 26:21

Zaburi 107:14

Marejeo

  • +Zb 68:6; 146:7; Isa 49:8, 9; 61:1

Zaburi 107:15

Marejeo

  • +Omb 3:22

Zaburi 107:16

Marejeo

  • +Isa 45:1, 2

Zaburi 107:17

Marejeo

  • +Yer 2:19
  • +Omb 3:39

Zaburi 107:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Walichukia kabisa vyakula vyote.”

Zaburi 107:20

Marejeo

  • +Zb 147:3

Zaburi 107:22

Marejeo

  • +Law 7:12; Zb 50:14

Zaburi 107:23

Marejeo

  • +2Nya 9:21; Eze 27:9

Zaburi 107:24

Marejeo

  • +Mwa 1:21; Zb 104:25

Zaburi 107:25

Marejeo

  • +Zb 135:7; Yer 10:13; Yon 1:4

Zaburi 107:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Nafsi yao.”

Zaburi 107:27

Marejeo

  • +Yon 1:4, 13

Zaburi 107:28

Marejeo

  • +Yon 1:14

Zaburi 107:29

Marejeo

  • +Zb 65:7; 89:9; Yon 1:15

Zaburi 107:31

Marejeo

  • +Zb 105:5

Zaburi 107:32

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kwenye kiti cha.”

Marejeo

  • +Zb 111:1

Zaburi 107:33

Marejeo

  • +1Fa 17:1, 7; Isa 42:15; Amo 4:7

Zaburi 107:34

Marejeo

  • +Mwa 13:10; Kum 29:22, 23

Zaburi 107:35

Marejeo

  • +2Fa 3:17; Isa 35:7; 41:18

Zaburi 107:36

Marejeo

  • +Zb 146:7; Lu 1:53
  • +Zb 107:7

Zaburi 107:37

Marejeo

  • +Isa 65:21
  • +Mdo 14:17

Zaburi 107:38

Marejeo

  • +Kum 7:13, 14

Zaburi 107:40

Marejeo

  • +Ayu 12:21, 24

Zaburi 107:41

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “huwainua juu,” yaani, ili wasifikiwe.

Marejeo

  • +1Sa 2:8

Zaburi 107:42

Marejeo

  • +Zb 58:10
  • +Kut 11:7; Zb 63:11

Zaburi 107:43

Marejeo

  • +Zb 64:9; Ho. 14:9
  • +Zb 77:12; 143:5; Yer 9:24

Jumla

Zab. 107:1Lu 18:19
Zab. 107:11Nya 16:34; Zb 103:17
Zab. 107:2Isa 35:10; Yer 15:21; Mik 4:10
Zab. 107:3Zb 106:47; Yer 29:14
Zab. 107:3Isa 43:5, 6; Yer 31:8
Zab. 107:6Ho. 5:14, 15
Zab. 107:6Isa 41:17
Zab. 107:7Isa 30:21
Zab. 107:7Ne 11:3
Zab. 107:81Nya 16:8
Zab. 107:8Zb 40:5
Zab. 107:9Zb 34:10; Isa 55:2; Lu 1:53
Zab. 107:11Zb 106:43; Omb 3:42
Zab. 107:12Law 26:21
Zab. 107:14Zb 68:6; 146:7; Isa 49:8, 9; 61:1
Zab. 107:15Omb 3:22
Zab. 107:16Isa 45:1, 2
Zab. 107:17Yer 2:19
Zab. 107:17Omb 3:39
Zab. 107:20Zb 147:3
Zab. 107:22Law 7:12; Zb 50:14
Zab. 107:232Nya 9:21; Eze 27:9
Zab. 107:24Mwa 1:21; Zb 104:25
Zab. 107:25Zb 135:7; Yer 10:13; Yon 1:4
Zab. 107:27Yon 1:4, 13
Zab. 107:28Yon 1:14
Zab. 107:29Zb 65:7; 89:9; Yon 1:15
Zab. 107:31Zb 105:5
Zab. 107:32Zb 111:1
Zab. 107:331Fa 17:1, 7; Isa 42:15; Amo 4:7
Zab. 107:34Mwa 13:10; Kum 29:22, 23
Zab. 107:352Fa 3:17; Isa 35:7; 41:18
Zab. 107:36Zb 146:7; Lu 1:53
Zab. 107:36Zb 107:7
Zab. 107:37Isa 65:21
Zab. 107:37Mdo 14:17
Zab. 107:38Kum 7:13, 14
Zab. 107:40Ayu 12:21, 24
Zab. 107:411Sa 2:8
Zab. 107:42Zb 58:10
Zab. 107:42Kut 11:7; Zb 63:11
Zab. 107:43Zb 64:9; Ho. 14:9
Zab. 107:43Zb 77:12; 143:5; Yer 9:24
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
  • 41
  • 42
  • 43
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Zaburi 107:1-43

Zaburi

KITABU CHA TANO

(Zaburi 107-150)

107 Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+

Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+

 2 Wale waliokombolewa* na Yehova na waseme jambo hilo,

Wale aliowakomboa kutoka mikononi mwa* adui,+

 3 Wale aliowakusanya pamoja kutoka katika nchi mbalimbali,+

Kutoka mashariki na kutoka magharibi,*

Kutoka kaskazini na kutoka kusini.+

 4 Walitangatanga nyikani, jangwani;

Hawakupata njia ya kwenda katika jiji ambamo wangeweza kuishi.

 5 Walikuwa na njaa na kiu;

Walidhoofika kwa sababu ya uchovu.

 6 Waliendelea kumlilia Yehova walipokuwa wakitaabika;+

Aliwaokoa kutoka katika dhiki yao.+

 7 Aliwaongoza kutembea katika njia inayofaa+

Ili wafike katika jiji ambamo wangeweza kuishi.+

 8 Watu na wamshukuru Yehova+ kwa sababu ya upendo wake mshikamanifu

Na kwa sababu ya kazi zake zinazostaajabisha anazowatendea wanadamu.+

 9 Kwa maana amewatosheleza wenye kiu*

Na kuwashibisha wenye njaa* kwa vitu vyema.+

10 Baadhi yao walikuwa wakiishi katika giza zito sana,

Wafungwa walioteseka na kufungwa kwa vyuma.

11 Kwa maana walikuwa wameliasi neno la Mungu;

Waliudharau ushauri wa Aliye Juu Zaidi.+

12 Kwa hiyo aliinyenyekeza mioyo yao kupitia taabu;+

Walijikwaa, na hakukuwa na yeyote wa kuwasaidia.

13 Walimlilia Yehova awasaidie walipokuwa wakitaabika;

Akawaokoa kutoka katika dhiki yao.

14 Aliwatoa katika giza zito sana,

Na kuzikata pingu zao.+

15 Watu na wamshukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mshikamanifu+

Na kwa sababu ya kazi zake zinazostaajabisha anazowatendea wanadamu.

16 Kwa maana ameivunja milango ya shaba

Na kuyakata makomeo ya chuma.+

17 Walikuwa wapumbavu, nao wakateseka+

Kwa sababu ya makosa yao na dhambi zao.+

18 Walipoteza hamu ya kula kila aina ya chakula;*

Waliyakaribia malango ya kifo.

19 Walikuwa wakimlilia Yehova awasaidie walipokuwa wakitaabika;

Naye alikuwa akiwaokoa kutoka katika dhiki yao.

20 Alikuwa akituma neno lake na kuwaponya+

Na kuwaokoa kutoka katika mashimo ambamo walikuwa wamenaswa.

21 Watu na wamshukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mshikamanifu

Na kwa sababu ya kazi zake zinazostaajabisha anazowatendea wanadamu.

22 Na watoe dhabihu za shukrani+

Na kutangaza kazi zake kwa kilio cha shangwe.

23 Wale wanaosafiri kwa meli baharini,

Wanaofanya biashara yao kwenye maji mengi,+

24 Wameziona kazi za Yehova

Na kazi zake zinazostaajabisha zilizo vilindini;+

25 Jinsi dhoruba ya upepo inavyoinuka kwa neno lake,+

Na kuyainua mawimbi ya bahari.

26 Hayo huinuka juu angani;

Hushuka chini kwa nguvu vilindini.

Ujasiri wao* huyeyuka kwa sababu ya msiba unaokaribia.

27 Wao hugaagaa na kupepesuka kama mlevi,

Na ustadi wao wote unakosa manufaa kabisa.+

28 Kisha wanamlilia Yehova kwa sauti wanapotaabika,+

Naye huwaokoa kutoka katika dhiki yao.

29 Yeye huituliza dhoruba ya upepo;

Mawimbi ya bahari hunyamaza.+

30 Wanashangilia yanapotulia,

Naye huwaongoza kwenda kwenye bandari wanayotamani.

31 Watu na wamshukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mshikamanifu

Na kwa sababu ya kazi zake zinazostaajabisha anazowatendea wanadamu.+

32 Na wamkweze katika kutaniko la watu,+

Na wamsifu katika baraza la* wazee.

33 Yeye hubadili mito kuwa jangwa,

Na chemchemi za maji kuwa ardhi iliyokauka,+

34 Nchi inayozaa kuwa nchi iliyoharibika yenye chumvi,+

Kwa sababu ya uovu wa wale wanaokaa humo.

35 Yeye hulibadili jangwa kuwa madimbwi ya maji yenye matete,

Na nchi kavu kuwa chemchemi za maji.+

36 Huwafanya wenye njaa wakae humo,+

Ili wajenge jiji ambamo wanaweza kuishi.+

37 Wanapanda mbegu mashambani na kupanda mashamba ya mizabibu+

Yanayozaa mazao mengi.+

38 Huwabariki, nao huongezeka sana;

Haachi ng’ombe wao wapungue.+

39 Kisha wanakuwa wachache tena na kuaibishwa

Kwa sababu ya ukandamizaji, msiba, na huzuni.

40 Huwamwagia wakuu dharau

Na kuwafanya watangetange jangwani kusiko na njia.+

41 Lakini huwalinda* maskini ili wasikandamizwe+

Na kufanya familia zao ziwe nyingi kama kundi la kondoo.

42 Wanyoofu huona hilo na kushangilia;+

Lakini waovu wote hufunga vinywa vyao.+

43 Yeyote aliye na hekima atayachunguza mambo hayo+

Naye atatafakari kwa makini matendo ya Yehova ya upendo mshikamanifu.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki