Zaburi
Muziki wa Daudi, alipokuwa katika nyika ya Yuda.+
63 Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, ninaendelea kukutafuta.+
Nina kiu kwa ajili yako.+
2 Kwa hiyo nimekutazama mahali patakatifu;
Nimeziona nguvu zako na utukufu wako.+
4 Basi nitakusifu maisha yangu yote;
Katika jina lako nitaiinua mikono yangu.
5 Nimeridhika na fungu bora ambalo ni zuri kabisa,*
Kwa hiyo kinywa changu kitakusifu kwa midomo yenye shangwe.+
6 Ninakukumbuka wewe nikiwa kitandani mwangu;
Ninatafakari kukuhusu katika makesha ya usiku.+
8 Ninashikamana nawe;
Mkono wako wa kuume hunishika kwa nguvu.+
9 Lakini wale wanaotaka kuniua*
Watashuka katika sehemu zenye kina zaidi za dunia.
10 Watatiwa katika nguvu za upanga;
Watakuwa chakula cha mbwamwitu.*
11 Lakini mfalme atashangilia kwa sababu ya Mungu.
Kila mtu anayeapa katika jina la Mungu atashangilia,*
Kwa maana kinywa cha wale wanaosema uwongo kitanyamazishwa.