Zaburi
118 Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+
Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.
2 Watu wa Israeli na waseme sasa:
“Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.”
3 Watu wa nyumba ya Haruni na waseme sasa:
“Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.”
4 Wale wanaomwogopa Yehova na waseme sasa:
“Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.”
6 Yehova yuko upande wangu; sitaogopa.+
Mwanadamu atanifanya nini?+
8 Ni bora kumkimbilia Yehova
Kuliko kuwatumaini wanadamu.+
9 Ni bora kumkimbilia Yehova
Kuliko kuwatumaini wakuu.+
11 Yalinizingira, naam, yalinizingira kabisa,
Lakini katika jina la Yehova,
Niliyafukuza.
12 Yalinizingira kama nyuki,
Lakini yalizimwa haraka kama moto unaoteketeza miiba.
Katika jina la Yehova,
Niliyafukuza.+
13 Nilisukumwa kwa nguvu* ili nianguke,
Lakini Yehova alinisaidia.
14 Yah ni mahali pangu pa kujificha na nguvu zangu,
Naye amekuwa wokovu wangu.+
15 Sauti ya shangwe na wokovu*
Imo katika mahema ya waadilifu.
Mkono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu zake.+
16 Mkono wa kuume wa Yehova unajikweza;
Mkono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu zake.+
17 Sitakufa, hapana, nitaishi,
Ili nizitangaze kazi za Yah.+
19 Nifungulieni malango ya uadilifu;+
Nitaingia humo na kumsifu Yah.
20 Hili ndilo lango la Yehova.
Waadilifu wataingia humo.+
21 Nitakusifu, kwa maana ulinijibu+
Nawe ukawa wokovu wangu.
24 Hii ndiyo siku ambayo Yehova ameifanya;
Tutaishangilia na kuifurahia.
25 Yehova, tuokoe, tafadhali, tunakusihi!
Yehova, tupe ushindi, tafadhali!
26 Amebarikiwa yule anayekuja katika jina la Yehova;+
Tunakubariki kutoka katika nyumba ya Yehova.
27 Yehova ni Mungu;
Hutupatia nuru.+
28 Wewe ni Mungu wangu, nami nitakusifu;
Mungu wangu, nitakukweza.+