Ayubu
17 “Roho yangu imevunjwa, siku zangu zimezimwa;
Makaburi yananingojea.+
3 Tafadhali ikubali dhamana yangu, na ukae nayo.
Ni nani mwingine atakayenipa mkono wake na kutoa dhamana kwa niaba yangu?+
4 Kwa sababu umeficha utambuzi mbali na moyo wao;+
Ndiyo maana huwakwezi.
5 Huenda akajitolea kushiriki vitu vyake na rafiki zake,
Huku macho ya watoto wake yakidhoofika.
6 Amenifanya niwe kitu cha kudharauliwa* miongoni mwa mataifa,+
Hivi kwamba nikawa mtu wanayemtemea mate usoni.+
7 Macho yangu yanafifia kwa sababu ya maumivu makali,+
Na viungo vyangu vyote ni kivuli tu.
8 Watu wanyoofu wananitazama kwa mshangao,
Na asiye na hatia anasumbuka kwa sababu ya mtu anayemkataa Mungu.*
10 Hata hivyo, nyote mnaweza kuja na kuendelea kunishambulia kwa hoja zenu,
Kwa maana sijamwona yeyote mwenye hekima miongoni mwenu.+
12 Wanaendelea kufanya usiku uwe mchana,
Wakisema, ‘Bila shaka mwangaza unakaribia kwa sababu kuna giza.’
14 Nitaliambia shimo*+ kwa sauti, ‘Wewe ni baba yangu!’
Na mabuu, ‘Ninyi ni mama yangu na dada yangu!’
15 Basi, tumaini langu liko wapi?+
Ni nani anayeweza kuona tumaini hilo?