Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 35
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Yeremia—Yaliyomo

      • Warekabu waonyesha utii wa pekee (1-19)

Yeremia 35:1

Marejeo

  • +2Fa 23:34; 2Nya 36:5; Da 1:1

Yeremia 35:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “vile vyumba.”

Marejeo

  • +2Fa 10:15; 1Nya 2:55

Yeremia 35:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Yonadabu,” ufupisho wa jina Yehonadabu.

Marejeo

  • +2Fa 10:15

Yeremia 35:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Yonadabu,” ufupisho wa jina Yehonadabu.

Yeremia 35:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.

Marejeo

  • +2Nya 36:5, 6; Da 1:1

Yeremia 35:13

Marejeo

  • +Yer 32:33

Yeremia 35:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “niliamka mapema na kuzungumza nanyi.”

Marejeo

  • +Yer 35:8
  • +2Nya 36:15, 16; Ne 9:26, 30; Yer 25:3

Yeremia 35:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nikiamka mapema na kuwatuma.”

Marejeo

  • +Yer 7:24, 25
  • +Isa 1:16; Yer 25:5; Eze 18:30; Ho. 14:1
  • +Yer 7:5-7

Yeremia 35:16

Marejeo

  • +Yer 35:8

Yeremia 35:17

Marejeo

  • +Kum 28:15; 29:26, 27; Yos 23:15, 16; 2Fa 23:27
  • +Isa 65:12; 66:4; Yer 7:13, 14

Yeremia 35:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Yonadabu,” ufupisho wa jina Yehonadabu.

Jumla

Yer. 35:12Fa 23:34; 2Nya 36:5; Da 1:1
Yer. 35:22Fa 10:15; 1Nya 2:55
Yer. 35:62Fa 10:15
Yer. 35:112Nya 36:5, 6; Da 1:1
Yer. 35:13Yer 32:33
Yer. 35:14Yer 35:8
Yer. 35:142Nya 36:15, 16; Ne 9:26, 30; Yer 25:3
Yer. 35:15Yer 7:24, 25
Yer. 35:15Isa 1:16; Yer 25:5; Eze 18:30; Ho. 14:1
Yer. 35:15Yer 7:5-7
Yer. 35:16Yer 35:8
Yer. 35:17Kum 28:15; 29:26, 27; Yos 23:15, 16; 2Fa 23:27
Yer. 35:17Isa 65:12; 66:4; Yer 7:13, 14
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Yeremia 35:1-19

Yeremia

35 Neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova katika siku za Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda likisema: 2 “Nenda katika nyumba ya Warekabu+ na uzungumze nao na kuwaleta katika nyumba ya Yehova, katika mojawapo ya vyumba vya kulia chakula;* nawe uwape divai wanywe.”

3 Basi nikampeleka Yaazania mwana wa Yeremia mwana wa Habasinia, ndugu zake, wanawe wote, na nyumba yote ya Warekabu 4 kwenye nyumba ya Yehova. Niliwapeleka katika chumba cha kulia chakula cha wana wa Hanani mwana wa Igdalia, mtu wa Mungu wa kweli, kilichokuwa kando ya chumba cha kulia chakula cha wakuu ambacho kilikuwa juu ya chumba cha kulia chakula cha Maaseya mwana wa Shalumu mlinzi wa mlango. 5 Kisha nikaweka vikombe na bilauri zilizojaa divai mbele ya watu wa nyumba ya Warekabu na kuwaambia: “Kunyweni divai.”

6 Lakini wakasema: “Hatutakunywa divai, kwa sababu Yehonadabu*+ mwana wa Rekabu, babu yetu, alituamuru hivi: ‘Ninyi wala wana wenu hampaswi kamwe kunywa divai. 7 Nanyi hampaswi kujenga nyumba, kupanda mbegu, au kupanda shamba la mizabibu au kulimiliki. Badala yake, mnapaswa kukaa katika mahema sikuzote, ili mwishi kwa muda mrefu katika nchi mnayoishi ndani yake mkiwa wageni.’ 8 Basi tunaendelea kuitii sauti ya Yehonadabu mwana wa Rekabu babu yetu kuhusu mambo yote aliyotuamuru, kwa kutokunywa kamwe divai—sisi, wake zetu, wana wetu, na mabinti wetu. 9 Nasi hatujengi nyumba za kuishi humo, wala hatuna mizabibu wala mashamba wala mbegu. 10 Tunaendelea kuishi katika mahema na kutii mambo yote ambayo babu yetu Yehonadabu* alituamuru. 11 Lakini Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni alipoishambulia nchi,+ tukasema, ‘Njooni, tuingie ndani ya Yerusalemu ili kuepuka jeshi la Wakaldayo na la Wasiria, na sasa tunaishi Yerusalemu.’”

12 Na neno la Yehova likamjia Yeremia likisema: 13 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Nenda uwaambie watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu: “Je, hamkuendelea kuhimizwa myatii maneno yangu?”+ asema Yehova. 14 “Yehonadabu mwana wa Rekabu aliwaamuru wazao wake wasinywe divai, nao wamefuata maneno yake kwa kutokunywa divai mpaka leo hii, na hivyo wameitii amri ya babu yao.+ Hata hivyo, nimezungumza nanyi tena na tena,* lakini hamjatii.+ 15 Nami niliendelea kuwatuma kwenu watumishi wangu wote manabii, nikiwatuma tena na tena,*+ na kusema, ‘Tafadhali geukeni, kila mmoja wenu kutoka kwenye njia zenu za uovu,+ nanyi mfanye yaliyo sawa! Msifuate miungu mingine na kuiabudu. Ndipo mtakapoendelea kukaa katika nchi niliyowapa ninyi na mababu zenu.’+ Lakini hamkutega sikio lenu wala hamkunisikiliza. 16 Wazao wa Yehonadabu mwana wa Rekabu wamefuata agizo ambalo babu yao aliwapa,+ lakini watu hawa hawajanisikiliza.”’”

17 “Kwa hiyo Yehova, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Ninawaletea watu wa Yuda na wakaaji wote wa Yerusalemu msiba wote niliowaonya kuuhusu,+ kwa maana nimezungumza nao, lakini walikataa kusikiliza, nami nikaendelea kuwaita, lakini walikataa kujibu.’”+

18 Naye Yeremia akawaambia hivi watu wa nyumba ya Warekabu: “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Kwa sababu mmetii agizo la babu yenu Yehonadabu nanyi mnaendelea kufuata maagizo yake yote, na kufanya sawasawa na alivyowaagiza, 19 Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Hatakosekana kamwe mzao wa Yehonadabu* mwana wa Rekabu atakayetumikia mbele zangu.”’”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki