Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 25
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Yeremia—Yaliyomo

      • Kesi ya Yehova dhidi ya mataifa (1-38)

        • Mataifa yatatumikia Babiloni kwa miaka 70 (11)

        • Kikombe cha divai ya ghadhabu ya Mungu (15)

        • Msiba kutoka taifa moja hadi lingine (32)

        • Wale ambao Yehova atawaua (33)

Yeremia 25:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.

Marejeo

  • +2Fa 24:1; Yer 36:1; 46:2; Da 1:1

Yeremia 25:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “aliwaambia hivi.”

Yeremia 25:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kuamka mapema na kusema.”

Marejeo

  • +Yer 1:2
  • +Yer 7:13; 13:10

Yeremia 25:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “akiamka mapema na kuwatuma.”

Marejeo

  • +Yer 29:19

Yeremia 25:5

Marejeo

  • +2Fa 17:13; Isa 55:7; Yer 18:11; 35:15; Eze 18:30; 33:11

Yeremia 25:7

Marejeo

  • +Kum 32:21; Ne 9:26

Yeremia 25:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.

Marejeo

  • +Law 26:25; Isa 5:26; Yer 1:15
  • +Yer 27:6; 43:10
  • +Kum 28:49, 50; Yer 5:15; Eze 7:24
  • +Eze 26:7; 29:19; Hab 1:6

Yeremia 25:10

Marejeo

  • +Isa 24:7; Eze 26:13
  • +Yer 7:34

Yeremia 25:11

Marejeo

  • +2Nya 36:20, 21; Da 9:2; Zek 1:12; 7:5

Yeremia 25:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nitamwadhibu mfalme wa Babiloni.”

Marejeo

  • +Kum 30:3; Ezr 1:1, 2; Yer 29:10
  • +Isa 47:1; Yer 51:1; Da 5:26, 30
  • +Isa 13:1, 19; 14:4, 23

Yeremia 25:14

Marejeo

  • +Yer 50:9; 51:27
  • +Isa 14:2; Hab 2:8
  • +Zb 137:8; Yer 50:29; 51:6, 24; Ufu 18:6

Yeremia 25:16

Marejeo

  • +Yer 51:7; Omb 4:21; Eze 23:32-34; Nah 3:7, 11

Yeremia 25:17

Marejeo

  • +Yer 1:10

Yeremia 25:18

Marejeo

  • +Isa 51:17
  • +Yer 24:9

Yeremia 25:19

Marejeo

  • +Yer 46:2

Yeremia 25:20

Marejeo

  • +Yer 47:1
  • +Yer 47:5

Yeremia 25:21

Marejeo

  • +Yer 49:17; Omb 4:21
  • +Yer 48:1
  • +Yer 49:1

Yeremia 25:22

Marejeo

  • +Yer 27:2, 3; 47:4

Yeremia 25:23

Marejeo

  • +Yer 49:8
  • +Yer 9:25, 26; 49:32

Yeremia 25:24

Marejeo

  • +Yer 49:31, 32

Yeremia 25:25

Marejeo

  • +Yer 49:34
  • +Yer 51:11

Yeremia 25:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Inaonekana hili ni jina la siri la Babeli (Babiloni).

Marejeo

  • +Yer 51:41

Yeremia 25:27

Marejeo

  • +Isa 63:6; Hab 2:16

Yeremia 25:29

Marejeo

  • +1Fa 9:7; Yer 7:12, 14; Da 9:18; Ho. 12:2; Mik 6:2
  • +Yer 49:12; Oba 16

Yeremia 25:31

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wote wenye mwili wa nyama.”

Marejeo

  • +Yoe 3:2

Yeremia 25:32

Marejeo

  • +Isa 34:2, 3; Yer 25:17
  • +Sef 3:8

Yeremia 25:38

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mwanasimba mwenye manyoya marefu shingoni.”

Marejeo

  • +Ho. 5:14

Jumla

Yer. 25:12Fa 24:1; Yer 36:1; 46:2; Da 1:1
Yer. 25:3Yer 1:2
Yer. 25:3Yer 7:13; 13:10
Yer. 25:4Yer 29:19
Yer. 25:52Fa 17:13; Isa 55:7; Yer 18:11; 35:15; Eze 18:30; 33:11
Yer. 25:7Kum 32:21; Ne 9:26
Yer. 25:9Law 26:25; Isa 5:26; Yer 1:15
Yer. 25:9Yer 27:6; 43:10
Yer. 25:9Kum 28:49, 50; Yer 5:15; Eze 7:24
Yer. 25:9Eze 26:7; 29:19; Hab 1:6
Yer. 25:10Isa 24:7; Eze 26:13
Yer. 25:10Yer 7:34
Yer. 25:112Nya 36:20, 21; Da 9:2; Zek 1:12; 7:5
Yer. 25:12Kum 30:3; Ezr 1:1, 2; Yer 29:10
Yer. 25:12Isa 47:1; Yer 51:1; Da 5:26, 30
Yer. 25:12Isa 13:1, 19; 14:4, 23
Yer. 25:14Yer 50:9; 51:27
Yer. 25:14Isa 14:2; Hab 2:8
Yer. 25:14Zb 137:8; Yer 50:29; 51:6, 24; Ufu 18:6
Yer. 25:16Yer 51:7; Omb 4:21; Eze 23:32-34; Nah 3:7, 11
Yer. 25:17Yer 1:10
Yer. 25:18Isa 51:17
Yer. 25:18Yer 24:9
Yer. 25:19Yer 46:2
Yer. 25:20Yer 47:1
Yer. 25:20Yer 47:5
Yer. 25:21Yer 49:17; Omb 4:21
Yer. 25:21Yer 48:1
Yer. 25:21Yer 49:1
Yer. 25:22Yer 27:2, 3; 47:4
Yer. 25:23Yer 49:8
Yer. 25:23Yer 9:25, 26; 49:32
Yer. 25:24Yer 49:31, 32
Yer. 25:25Yer 49:34
Yer. 25:25Yer 51:11
Yer. 25:26Yer 51:41
Yer. 25:27Isa 63:6; Hab 2:16
Yer. 25:291Fa 9:7; Yer 7:12, 14; Da 9:18; Ho. 12:2; Mik 6:2
Yer. 25:29Yer 49:12; Oba 16
Yer. 25:31Yoe 3:2
Yer. 25:32Isa 34:2, 3; Yer 25:17
Yer. 25:32Sef 3:8
Yer. 25:38Ho. 5:14
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Yeremia 25:1-38

Yeremia

25 Neno lililomjia Yeremia kuhusu watu wote wa Yuda katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kwanza wa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni. 2 Nabii Yeremia alisema hivi kuhusu* watu wote wa Yuda na wakaaji wote wa Yerusalemu:

3 “Tangu mwaka wa 13 wa utawala wa Yosia+ mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda, mpaka leo hii, miaka hii 23, neno la Yehova limenijia, nami niliendelea kuwaambia tena na tena,* lakini hamkusikiliza.+ 4 Na Yehova aliwatuma kwenu watumishi wake wote manabii, aliwatuma tena na tena,* lakini hamkusikiliza, wala kutega sikio lenu ili msikie.+ 5 Walikuwa wakisema, ‘Tafadhali, geukeni kila mmoja wenu kutoka katika njia zenu za uovu na matendo yenu maovu;+ nanyi mtaendelea kukaa kwa muda mrefu katika nchi ambayo Yehova aliwapa ninyi na mababu zenu zamani. 6 Msiifuate miungu mingine na kuiabudu na kuiinamia, na kunikasirisha kwa kazi ya mikono yenu; la sivyo nitawaletea msiba.’

7 “‘Lakini hamkunisikiliza,’ asema Yehova, ‘Badala yake mlinikasirisha kwa kazi ya mikono yenu, na kujiletea msiba.’+

8 “Kwa hiyo Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘“Kwa sababu hamkuyatii maneno yangu, 9 ninaziita familia zote za kaskazini,”+ asema Yehova, “ninamwita Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni, mtumishi wangu,+ nami nitawaleta dhidi ya nchi hii+ na dhidi ya wakaaji wake na dhidi ya mataifa haya yote yanayozunguka.+ Nitawaangamiza na kuwafanya kuwa kitu cha kutisha na kitu cha kupigiwa mluzi na magofu ya kudumu. 10 Nitakomesha sauti ya furaha na sauti ya shangwe ndani yao,+ sauti ya bwana harusi na sauti ya bibi harusi,+ sauti ya jiwe la kusagia na nuru ya taa. 11 Na nchi hii yote itakuwa magofu na kitu cha kutisha, na mataifa haya yatalazimika kumtumikia mfalme wa Babiloni kwa miaka 70.”’+

12 “‘Lakini miaka 70 itakapotimia,+ nitamfanya mfalme wa Babiloni awajibike* na pia taifa hilo kwa sababu ya kosa lao,’+ asema Yehova, ‘nami nitaifanya nchi ya Wakaldayo kuwa mahame na ukiwa daima.+ 13 Nitatimiza maneno yangu yote niliyosema dhidi ya nchi hiyo, yote yaliyoandikwa katika kitabu hiki ambayo Yeremia ametabiri dhidi ya mataifa yote. 14 Kwa maana mataifa mengi na wafalme wakuu+ watawafanya kuwa watumwa,+ nami nitawalipa kulingana na matendo yao na kazi ya mikono yao wenyewe.’”+

15 Kwa maana Yehova Mungu wa Israeli aliniambia hivi: “Chukua kikombe hiki cha divai ya ghadhabu kutoka mkononi mwangu, nawe uyanyweshe mataifa yote ambayo ninakutuma kwao. 16 Nao watakunywa na kupepesuka na kutenda kama wendawazimu kwa sababu ya upanga ninaotuma miongoni mwao.”+

17 Basi nikakichukua kile kikombe kutoka mkononi mwa Yehova na kuyanywesha mataifa yote ambayo Yehova alinituma kwao:+ 18 kuanzia Yerusalemu na majiji ya Yuda,+ wafalme wake na wakuu wake, ili kuyafanya kuwa magofu, kitu cha kutisha, kitu cha kupigiwa mluzi na laana,+ kama ilivyo leo; 19 kisha mfalme Farao wa Misri na watumishi wake, wakuu wake, na watu wake wote,+ 20 na watu wa mataifa mbalimbali waliochangamana nao; wafalme wote wa nchi ya Usi; wafalme wote wa nchi ya Wafilisti,+ Ashkeloni,+ Gaza, Ekroni, na watu waliobaki wa Ashdodi; 21 Edomu,+ Moabu,+ na Waamoni;+ 22 wafalme wote wa Tiro, wafalme wote wa Sidoni,+ na wafalme wa kisiwa kilicho baharini; 23 Dedani,+ Tema, Buzi, na wale wote wanaonyoa nywele pembeni mwa vichwa vyao;+ 24 wafalme wote wa Waarabu+ na wafalme wote wa watu wa mataifa mbalimbali wanaokaa nyikani; 25 wafalme wote wa Zimri, wafalme wote wa Elamu,+ na wafalme wote wa Wamedi;+ 26 na wafalme wote wa kaskazini walio karibu na walio mbali, mmoja baada ya mwingine, na falme nyingine zote za dunia zilizo juu ya ardhi; na mfalme wa Sheshaki*+ atakunywa baada yao.

27 “Nawe unapaswa kuwaambia, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Kunyweni, mlewe, mtapike na kuanguka hivi kwamba msiweze kusimama+ kwa sababu ya upanga ninaotuma miongoni mwenu.”’ 28 Nao wakikataa kukichukua kikombe kutoka mkononi mwako ili wanywe, waambie, ‘Yehova wa majeshi anasema hivi: “Lazima mnywe! 29 Kwa maana tazama! ikiwa ninaleta msiba kwanza juu ya jiji linaloitwa kwa jina langu,+ je, ninyi pia hampaswi kuadhibiwa?”’+

“‘Hamtakosa kuadhibiwa, kwa maana ninauita upanga dhidi ya wakaaji wote wa dunia,’ asema Yehova wa majeshi.

30 “Nawe unapaswa kuwatabiria maneno haya yote, uwaambie,

‘Yehova atanguruma kutoka juu,

Kutoka katika makao yake matakatifu atafanya sauti yake isikike.

Atanguruma kwa sauti kubwa dhidi ya makao yake yanayodumu.

Atapaza sauti kama watu wanaokanyaga shinikizo la divai,

Ataimba kwa ushindi dhidi ya wakaaji wote wa dunia.’

31 ‘Kelele zitasikika mpaka kwenye miisho ya dunia,

Kwa maana Yehova ana kesi dhidi ya mataifa.

Yeye binafsi atawahukumu wanadamu wote.*+

Naye atawaangamiza waovu kwa upanga,’ asema Yehova.

32 Yehova wa majeshi anasema hivi:

‘Tazameni! Msiba unaenea kutoka taifa mpaka taifa,+

Na tufani kubwa itaachiliwa kutoka sehemu za mbali zaidi za dunia.+

33 “‘Na wale ambao Yehova atawaua siku hiyo watatapakaa kutoka mwisho mmoja wa dunia mpaka mwisho wa pili wa dunia. Hawataombolezewa, wala kukusanywa wala kuzikwa. Watakuwa kama mbolea juu ya ardhi.’

34 “Ombolezeni, enyi wachungaji, na mlie kwa sauti!

Mgaegae, enyi watu mashuhuri wa kundi,

Kwa sababu wakati wenu wa kuchinjwa na kutawanywa umefika,

Nanyi mtaanguka kama chombo chenye thamani!

35 Wachungaji hawana mahali pa kukimbilia,

Na watu mashuhuri wa kundi hawawezi kuponyoka.

36 Sikilizeni! Kilio cha wachungaji

Na kuomboleza kwa watu mashuhuri wa kundi,

Kwa maana Yehova anaharibu malisho yao.

37 Na makao yenye amani yamefanywa yasiwe na uhai

Kwa sababu ya hasira ya Yehova inayowaka.

38 Ametoka katika pango

lake kama mwanasimba,*+

Kwa maana nchi yao imekuwa kitu cha kutisha

Kwa sababu ya upanga wenye ukatili

Na kwa sababu ya hasira yake inayowaka.”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki