Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 42
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Yeremia—Yaliyomo

      • Watu wamwomba Yeremia asali ili wapate mwongozo (1-6)

      • Yehova ajibu hivi: “Msiende Misri” (7-22)

Yeremia 42:1

Marejeo

  • +Yer 40:13, 14

Yeremia 42:2

Marejeo

  • +Kum 28:62

Yeremia 42:8

Marejeo

  • +Yer 41:16

Yeremia 42:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nitahuzunika.”

Marejeo

  • +Kum 32:36; Yer 18:7, 8; Mik 7:18

Yeremia 42:11

Marejeo

  • +Yer 41:17, 18

Yeremia 42:12

Marejeo

  • +Kut 34:6

Yeremia 42:14

Marejeo

  • +Yer 43:4, 7

Yeremia 42:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mwende kukaa huko kwa muda.”

Yeremia 42:16

Marejeo

  • +Kum 28:45; Yer 44:12-14, 27, 28

Yeremia 42:18

Marejeo

  • +2Fa 25:8-10; 2Nya 34:24, 25; 36:16, 17; Omb 2:4
  • +Yer 29:18

Yeremia 42:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi zenu.”

Marejeo

  • +Yer 42:1, 2

Yeremia 42:21

Marejeo

  • +2Nya 24:19; Ne 9:26; Zek 7:11

Yeremia 42:22

Marejeo

  • +Yer 43:10, 11

Jumla

Yer. 42:1Yer 40:13, 14
Yer. 42:2Kum 28:62
Yer. 42:8Yer 41:16
Yer. 42:10Kum 32:36; Yer 18:7, 8; Mik 7:18
Yer. 42:11Yer 41:17, 18
Yer. 42:12Kut 34:6
Yer. 42:14Yer 43:4, 7
Yer. 42:16Kum 28:45; Yer 44:12-14, 27, 28
Yer. 42:182Fa 25:8-10; 2Nya 34:24, 25; 36:16, 17; Omb 2:4
Yer. 42:18Yer 29:18
Yer. 42:20Yer 42:1, 2
Yer. 42:212Nya 24:19; Ne 9:26; Zek 7:11
Yer. 42:22Yer 43:10, 11
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Yeremia 42:1-22

Yeremia

42 Kisha wakuu wote wa jeshi, na Yohanani+ mwana wa Karea, Yezania mwana wa Hoshaya, na watu wote, kuanzia mdogo zaidi mpaka mkubwa zaidi, wakakaribia 2 na kumwambia nabii Yeremia: “Tafadhali, sikia ombi letu la kutaka kibali nawe usali kwa ajili yetu kwa Yehova Mungu wako, kwa ajili ya watu hawa wote waliobaki, kwa maana kati ya watu wengi, wachache ndio waliobaki,+ kama unavyoona. 3 Yehova Mungu wako na atuambie njia tunayopaswa kuifuata na jambo tunalopaswa kufanya.”

4 Nabii Yeremia akawajibu: “Nimewasikia, nami ninasali kwa Yehova Mungu wenu kulingana na ombi lenu; na kila neno ambalo Yehova atawajibu, nitawaambia. Sitawaficha neno lolote.”

5 Wakamjibu Yeremia: “Yehova na awe shahidi wa kweli na mwaminifu dhidi yetu ikiwa hatutafanya sawasawa kama anavyotuagiza Yehova Mungu wako kupitia wewe. 6 Iwe ni jambo jema au baya, tutaitii sauti ya Yehova Mungu wetu ambaye tunakutuma kwake, ili mambo yatuendee vema kwa sababu tunaitii sauti ya Yehova Mungu wetu.”

7 Baada ya siku kumi neno la Yehova likamjia Yeremia. 8 Basi akamwita Yohanani mwana wa Karea na wakuu wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye na watu wote, kuanzia mdogo zaidi mpaka mkubwa zaidi.+ 9 Akawaambia: “Yehova Mungu wa Israeli, ambaye mlinituma kwake ili kupeleka ombi lenu la kutaka kibali mbele zake, anasema hivi: 10 ‘Ikiwa kwa kweli mtakaa katika nchi hii, basi nitawajenga nami sitawabomoa, nitawapanda nami sitawang’oa, kwa maana nitaghairi* kuhusu msiba ambao nimewaletea.+ 11 Msimwogope mfalme wa Babiloni, mnayemwogopa.’+

“‘Msimwogope,’ asema Yehova, ‘kwa maana niko pamoja nanyi, ili kuwaokoa na kuwakomboa kutoka mikononi mwake. 12 Nami nitawaonyesha rehema,+ naye atawaonyesha rehema na kuwarudisha kwenye nchi yenu wenyewe.

13 “‘Lakini mkisema, “Hapana, hatutakaa katika nchi hii!” nanyi mkose kuitii sauti ya Yehova Mungu wenu 14 kwa kusema: “Hapana, badala yake tutaenda katika nchi ya Misri,+ ambako hatutaona vita wala kusikia sauti ya pembe wala kuwa na njaa kwa kukosa mkate; huko ndiko tutakakoishi,” 15 basi sikieni neno la Yehova, enyi watu wa Yuda mliobaki. Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Ikiwa mmeazimia kabisa kwenda Misri nanyi mwende kukaa huko,* 16 ndipo upanga uleule ambao mnaogopa utawafikia huko katika nchi ya Misri, na njaa ileile ambayo mnaogopa itawafuata huko Misri, nanyi mtafia huko.+ 17 Na watu wote walioazimia kwenda Misri ili kukaa huko watakufa kwa upanga, kwa njaa kali, na kwa ugonjwa hatari. Hakuna yeyote kati yao atakayeokoka au kuponyoka msiba nitakaowaletea.”’

18 “Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Kama hasira yangu na ghadhabu yangu ilivyomwagwa juu ya wakaaji wa Yerusalemu,+ ndivyo ghadhabu yangu itakavyomwagwa juu yenu ikiwa mtaenda Misri, nanyi mtakuwa laana, kitu cha kutisha, matusi, na shutuma,+ nanyi hamtapaona tena kamwe mahali hapa.’

19 “Yehova amewakataza, enyi watu wa Yuda mliobaki. Msiende Misri. Mnapaswa kujua kwa hakika kwamba nimewaonya leo, 20 kwamba kosa lenu litawagharimu uhai wenu.* Kwa maana mlinituma kwa Yehova Mungu wenu, mkisema, ‘Sali kwa ajili yetu kwa Yehova Mungu wetu, nawe utuambie kila jambo ambalo Yehova Mungu wetu anasema, nasi tutalifanya.’+ 21 Nami nimewaambia leo, lakini hamtaitii sauti ya Yehova Mungu wenu wala kufanya jambo lolote alilonituma niwaambie.+ 22 Kwa hiyo, jueni kwa hakika kwamba mtakufa kwa upanga, kwa njaa kali, na kwa ugonjwa hatari mahali mnapotamani kwenda kuishi.”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki