14 na roho ya wivu+ imempata mume wake, naye ameutilia shaka uaminifu wa mke wake, na mwanamke huyo kwa kweli amejitia unajisi, au roho ya wivu imempata mume wake, naye ameutilia shaka uaminifu wa mke wake, lakini yeye kwa kweli hajajitia unajisi;
15 basi mwanamume huyo lazima amlete mke wake kwa kuhani+ na kuleta toleo lake pamoja naye, sehemu ya kumi ya efa ya unga wa shayiri. Hatamimina mafuta juu yake wala kuweka ubani+ juu yake, kwa sababu ni toleo la nafaka la wivu, toleo la ukumbusho linaloleta kosa kwenye kumbukumbu.