31 Malkia+ wa kusini atasimamishwa katika hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki naye atawahukumu kuwa wenye hatia; kwa sababu yeye alikuja kutoka miisho ya dunia ili aisikie hekima ya Sulemani, lakini, tazameni! Aliye mkuu+ kuliko Sulemani yupo hapa.
32 Watu wa Ninawi watasimama katika hukumu pamoja na kizazi hiki nao watakilaumu; kwa maana walitubu kutokana na mahubiri ya Yona;+ lakini, tazameni! Aliye mkuu+ kuliko Yona yupo hapa.