-
Hesabu 4:14, 15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
14 Kisha wataweka juu yake vyombo vyake vyote wanavyotumia kuhudumu kwenye madhabahu: vyetezo, nyuma,* sepetu, na mabakuli, vyombo vyote vya madhabahu;+ watatandaza juu yake kifuniko cha ngozi ya sili na kuingiza fito za kuibeba.+
15 “Ni lazima Haruni na wanawe wamalize kufunika mahali patakatifu+ na vyombo vyote vya mahali patakatifu kabla ya watu kuanza safari. Kisha wana wa Kohathi watakuja kuvibeba,+ lakini hawapaswi kugusa vitu vitakatifu, la sivyo watakufa.+ Wana wa Kohathi ndio walio na jukumu la kubeba vitu vya hema la mkutano.
-