-
Mambo ya Walawi 16:5, 6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 “Anapaswa kuchukua kutoka kwa Waisraeli+ wanambuzi dume wawili kwa ajili ya dhabihu ya dhambi na kondoo dume mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa.
6 “Kisha Haruni atamtoa yule ng’ombe dume wa dhabihu ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe, naye atatoa dhabihu ya kufunika dhambi zake mwenyewe+ na za nyumba yake.
-
-
Mambo ya Walawi 16:18, 19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 “Kisha atatoka nje na kwenda kwenye madhabahu+ iliyo mbele za Yehova, naye atatoa dhabihu ya kufunika dhambi kwa ajili ya madhabahu hiyo, kisha atachukua kiasi fulani cha damu ya yule ng’ombe dume na kiasi fulani cha damu ya yule mbuzi na kupaka pembe za madhabahu pande zote. 19 Pia atainyunyizia madhabahu kiasi fulani cha damu hiyo mara saba kwa kidole chake na kuisafisha na kuitakasa kwa sababu ya uchafu wa Waisraeli.
-