-
Mambo ya Walawi 22:18-20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 “Waambie hivi Haruni na wanawe na Waisraeli wote: ‘Mwanamume Mwisraeli au mgeni katika Israeli anapomtolea Yehova dhabihu ya kuteketezwa+ ili kutimiza nadhiri zake au kutoa toleo la hiari,+ 19 anapaswa kutoa ng’ombe dume asiye na kasoro,+ wanakondoo dume, au mbuzi ili apate kibali. 20 Hampaswi kutoa kitu chochote chenye kasoro,+ kwa sababu hamtapata kibali mkifanya hivyo.
-