5 Wana wa Haruni watateketeza vitu hivyo kwenye madhabahu juu ya dhabihu ya kuteketezwa iliyo kwenye kuni zinazowaka moto ili vifuke moshi;+ ni dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova.+
16 Kuhani ataviteketeza vitu hivyo kwenye madhabahu kama chakula* ili vifuke moshi, ni dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayopendeza.* Mafuta yote ni ya Yehova.+