Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 3:16, 17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Kuhani ataviteketeza vitu hivyo kwenye madhabahu kama chakula* ili vifuke moshi, ni dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayopendeza.* Mafuta yote ni ya Yehova.+

      17 “‘Ni sheria ya kudumu kwa vizazi vyenu, katika makao yenu yote: Msile mafuta yoyote wala damu+ yoyote.’”

  • Mambo ya Walawi 4:8-10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 “‘Kisha ataondoa mafuta yote ya huyo ng’ombe dume wa dhabihu ya dhambi, pamoja na mafuta yanayofunika matumbo na mafuta yanayozunguka matumbo, 9 na figo zake mbili pamoja na mafuta yake yaliyo karibu na kiuno. Ataondoa pia figo pamoja na mafuta yaliyo juu ya ini.+ 10 Ataondoa sehemu zilezile zinazoondolewa katika ng’ombe dume wa dhabihu ya ushirika.+ Na kuhani ataviteketeza kwenye madhabahu ya dhabihu za kuteketezwa ili vifuke moshi.

  • 1 Samweli 2:16, 17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Mtu huyo alipomwambia, “Acha kwanza wahakikishe kwamba mafuta yamefuka moshi,+ kisha ujichukulie chochote upendacho,”* alisema: “Hapana, nipe sasa hivi; la sivyo, nitaichukua kwa nguvu!” 17 Kwa hiyo dhambi ya watumishi hao ikawa kubwa sana mbele za Yehova,+ kwa maana watu hao hawakuheshimu dhabihu ya Yehova.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki