- 
	                        
            
            Mambo ya Walawi 4:8-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
 - 
                            
- 
                                        
8 “‘Kisha ataondoa mafuta yote ya huyo ng’ombe dume wa dhabihu ya dhambi, pamoja na mafuta yanayofunika matumbo na mafuta yanayozunguka matumbo, 9 na figo zake mbili pamoja na mafuta yake yaliyo karibu na kiuno. Ataondoa pia figo pamoja na mafuta yaliyo juu ya ini.+ 10 Ataondoa sehemu zilezile zinazoondolewa katika ng’ombe dume wa dhabihu ya ushirika.+ Na kuhani ataviteketeza kwenye madhabahu ya dhabihu za kuteketezwa ili vifuke moshi.
 
 - 
                                        
 
- 
	                        
            
            1 Samweli 2:16, 17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
 - 
                            
- 
                                        
16 Mtu huyo alipomwambia, “Acha kwanza wahakikishe kwamba mafuta yamefuka moshi,+ kisha ujichukulie chochote upendacho,”* alisema: “Hapana, nipe sasa hivi; la sivyo, nitaichukua kwa nguvu!” 17 Kwa hiyo dhambi ya watumishi hao ikawa kubwa sana mbele za Yehova,+ kwa maana watu hao hawakuheshimu dhabihu ya Yehova.
 
 -