-
Mambo ya Walawi 14:10, 11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 “Siku ya nane, ataleta wanakondoo dume wawili wasio na kasoro, mwanakondoo jike wa mwaka mmoja asiye na kasoro,+ na sehemu tatu za kumi za kipimo cha efa* ya unga laini uliochanganywa na mafuta kuwa toleo la nafaka,+ na logi moja* ya mafuta;+ 11 na kuhani anayemtangaza kuwa safi atamleta mtu huyo anayejitakasa na matoleo hayo mbele za Yehova kwenye mlango wa hema la mkutano.
-