-
Mambo ya Walawi 14:15-18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Halafu kuhani atachukua kiasi kidogo cha ile logi ya mafuta+ na kumimina kwenye kiganja chake mwenyewe cha mkono wa kushoto. 16 Kisha kuhani atachovya kidole chake cha kulia katika mafuta yaliyo kwenye kiganja chake cha kushoto, atanyunyiza mara saba kwa kidole chake kiasi kidogo cha mafuta hayo mbele za Yehova. 17 Kisha kuhani atatia kiasi kidogo cha mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake na kupaka ncha ya sikio la kulia la mtu anayejitakasa na kidole gumba cha mkono wake wa kulia na kidole gumba cha mguu wake wa kulia juu ya damu ya dhabihu ya hatia. 18 Kuhani atatia mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake na kumpaka kichwani mtu anayejitakasa, naye kuhani atamtolea mtu huyo dhabihu ya kufunika dhambi yake mbele za Yehova.+
-