3 Kuhani atatoka nje ya kambi na kumchunguza. Ikiwa mtu mwenye ukoma amepona, 4 kuhani atamwamuru alete ndege safi wawili walio hai, tawi la mwerezi, kitambaa cha rangi nyekundu, na tawi la hisopo ili atakaswe.+
6 Halafu kuhani atachukua tawi la mwerezi, tawi la hisopo,+ na kitambaa chekundu na kutupa vitu hivyo katika moto unaomteketeza ng’ombe huyo. 7 Kisha kuhani atafua mavazi yake na kuoga kwenye maji, halafu anaweza kurudi kambini; lakini kuhani huyo hatakuwa safi mpaka jioni.