-
2 Samweli 13:10-12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Kisha Amnoni akamwambia Tamari: “Niletee chakula* katika chumba cha kulala, ili nikichukue kutoka mkononi mwako na kukila.” Basi Tamari akachukua keki zenye umbo la moyo ambazo alikuwa ameoka na kumletea Amnoni ndugu yake katika chumba cha kulala. 11 Alipomletea ili ale, Amnoni akamkamata kwa nguvu na kumwambia: “Njoo, ulale nami, dada yangu.” 12 Lakini Tamari akamwambia: “Usifanye hivyo ndugu yangu! Usiniabishe, kwa maana jambo kama hili halipaswi kufanywa katika Israeli.+ Usitende jambo hili la aibu.+
-