-
1 Wafalme 13:2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Kisha kwa neno la Yehova akapaza sauti dhidi ya madhabahu hiyo na kusema: “Ee madhabahu, madhabahu! Hivi ndivyo Yehova anavyosema, ‘Tazama! Mwana anayeitwa Yosia,+ atazaliwa katika nyumba ya Daudi! Na juu yako atawatoa dhabihu makuhani wa mahali pa juu, wanaofukiza moshi wa dhabihu juu yako, naye atateketeza mifupa ya wanadamu juu yako.’”+
-
-
2 Wafalme 23:8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Kisha akawaondoa makuhani wote katika majiji ya Yuda, naye akafanya mahali pa juu ambapo makuhani walifukizia moshi wa dhabihu pasifae kwa ibada, kuanzia Geba+ mpaka Beer-sheba.+ Alibomoa pia mahali pa juu palipokuwa kwenye malango yaliyokuwa katika njia ya kuingia kwenye lango la Yoshua mkuu wa jiji, malango yaliyokuwa upande wa kushoto mtu anapoingia katika lango la jiji.
-