24 “Haruni atakufa na kuzikwa kama watu wake walivyozikwa.*+ Hataingia katika nchi nitakayowapa Waisraeli, kwa sababu ninyi wawili mliasi agizo nililowapa kuhusu maji ya Meriba.+
28 Kisha Musa akamvua Haruni mavazi yake na kumvisha Eleazari mwanawe. Baada ya hayo, Haruni akafa juu ya mlima huo.+ Kisha Musa na Eleazari wakateremka kutoka mlimani.
38 Kisha kuhani Haruni akapanda juu ya Mlima Hori kwa agizo la Yehova, akafa huko siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa 40 tangu Waisraeli walipotoka nchini Misri.+
6 “Kisha Waisraeli wakaondoka Beerothi Bene-yaakani na kwenda Mosera. Haruni akafa na kuzikwa huko,+ na Eleazari mwana wake akaanza kutumikia akiwa kuhani baada yake.+
50 Kisha utakufa juu ya mlima utakaopanda hivi punde, na kuzikwa pamoja na watu wako,* kama Haruni ndugu yako alivyokufa juu ya Mlima Hori+ na kuzikwa pamoja na watu wake,