1 Haya ndiyo maneno ambayo Musa aliwaambia Waisraeli wote walipokuwa nyikani katika eneo la Yordani, katika jangwa tambarare mbele ya Sufi, kati ya Parani, Tofeli, Labani, Haserothi, na Dizahabu. 2 Ni safari ya siku 11 kutoka Horebu mpaka Kadesh-barnea+ kupitia njia ya Mlima Seiri.